< Zaburi 14 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Mpumbavu anasema moyoni mwake, “Hakuna Mungu.” Wameharibika, matendo yao ni maovu kabisa; hakuna hata mmoja atendaye mema.
For the chief musician. A psalm of David. A fool says in his heart, “There is no God.” They are corrupt and have done abominable iniquity; there is no one who does good.
2 Bwana anawachungulia wanadamu chini kutoka mbinguni aone kama wako wenye akili, wowote wanaomtafuta Mungu.
Yahweh looks down from heaven on the children of mankind to see if there are any who understand, who seek after him.
3 Wote wamepotoka, wameharibika wote pamoja, hakuna atendaye mema. Naam, hakuna hata mmoja!
They have all turned away. Together they have become corrupt. There is no one who does good, no, not one.
4 Je, watendao mabaya kamwe hawatajifunza: wale ambao huwala watu wangu kama watu walavyo mkate, hao ambao hawamwiti Bwana?
Do they not know anything, those who commit iniquity, those who eat up my people as they eat bread, but who do not call on Yahweh?
5 Wako hapo, wameingiwa na hofu kuu, maana Mungu yupo pamoja na wenye haki.
They tremble with dread, for God is with the righteous assembly!
6 Ninyi watenda mabaya mnakwamisha mipango ya maskini, bali Bwana ndiye kimbilio lao.
You want to humiliate the poor person even though Yahweh is his refuge.
7 Laiti wokovu wa Israeli ungalikuja kutoka Sayuni! Wakati Bwana arejeshapo wafungwa wa watu wake, Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi!
Oh, that the salvation of Israel would come from Zion! When Yahweh brings back his people from the captivity, then Jacob will rejoice and Israel will be glad!

< Zaburi 14 >