< Zaburi 135 >

1 Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
Louez l'Éternel! Louez le nom de l'Éternel; louez-le, serviteurs de l'Éternel!
2 ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
Vous qui vous tenez dans la maison de l'Éternel, dans les parvis de la maison de notre Dieu,
3 Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
Louez l'Éternel, car l'Éternel est bon! Chantez à son nom, car il est clément!
4 Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
Car l'Éternel s'est choisi Jacob et Israël pour sa possession.
5 Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
Car je sais que l'Éternel est grand, et notre Seigneur au-dessus de tous les dieux.
6 Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
L'Éternel fait tout ce qui lui plaît dans les cieux et sur la terre, dans les mers et dans tous les abîmes.
7 Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
C'est lui qui fait monter du bout de la terre les vapeurs; qui produit les éclairs et la pluie; qui tire le vent de ses trésors.
8 Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
C'est lui qui a frappé les premiers-nés d'Égypte, depuis les hommes jusqu'aux bêtes;
9 Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
Qui a envoyé des signes et des prodiges au milieu de toi, Égypte, contre Pharaon et contre tous ses serviteurs;
10 Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
Qui a frappé plusieurs nations, et mis à mort de puissants rois:
11 Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
Sihon, roi des Amoréens, et Og, roi de Bassan, et tous les rois de Canaan;
12 akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
Et qui a donné leur pays en héritage, en héritage à Israël, son peuple.
13 Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
Éternel, ton nom subsiste à toujours; Éternel, ta mémoire est d'âge en âge.
14 Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
Car l'Éternel fera justice à son peuple, et il aura compassion de ses serviteurs.
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
Les idoles des nations sont de l'argent et de l'or, un ouvrage de mains d'homme.
16 Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
Elles ont une bouche, et ne parlent point; elles ont des yeux, et ne voient point;
17 zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
Elles ont des oreilles, et n'entendent point; il n'y a pas non plus de souffle dans leur bouche.
18 Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
Ceux qui les font et tous ceux qui s'y confient leur deviendront semblables!
19 Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
Maison d'Israël, bénissez l'Éternel! Maison d'Aaron, bénissez l'Éternel!
20 ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
Maison de Lévi, bénissez l'Éternel! Vous qui craignez l'Éternel, bénissez l'Éternel!
21 Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.
Béni soit, de Sion, l'Éternel qui réside à Jérusalem! Louez l'Éternel!

< Zaburi 135 >