< Zaburi 135 >

1 Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
Let the Lord be praised. O you servants of the Lord, give praise to the name of the Lord.
2 ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
You who are in the house of the Lord, and in the open spaces of the house of our God,
3 Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
Give praise to Jah, for he is good: make melody to his name, for it is pleasing.
4 Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
For the Lord has taken Jacob for himself, and Israel for his property.
5 Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
I know that the Lord is great, and that our Lord is greater than all other gods.
6 Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
The Lord has done whatever was pleasing to him, in heaven, and on the earth, in the seas and in all the deep waters.
7 Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
He makes the mists go up from the ends of the earth; he makes thunder-flames for the rain; he sends out the winds from his store-houses.
8 Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
He put to death the first-fruits of Egypt, of man and of beast.
9 Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
He sent signs and wonders among you, O Egypt, on Pharaoh, and on all his servants.
10 Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
He overcame great nations, and put strong kings to death;
11 Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
Sihon, king of the Amorites, and Og, king of Bashan, and all the kingdoms of Canaan;
12 akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
And gave their land for a heritage, even for a heritage to Israel his people.
13 Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
O Lord, your name is eternal; and the memory of you will have no end.
14 Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
For the Lord will be judge of his people's cause; his feelings will be changed to his servants.
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
The images of the nations are silver and gold, the work of men's hands.
16 Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
They have mouths, but no voice, they have eyes, but they do not see;
17 zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
They have ears, but no hearing; and there is no breath in their mouths.
18 Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
Those who make them are like them; and so is everyone who puts his hope in them.
19 Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
Give praise to the Lord, O children of Israel: give praise to the Lord, O sons of Aaron:
20 ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
Give praise to the Lord, O sons of Levi: let all the worshippers of the Lord give him praise.
21 Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.
Praise be to the Lord out of Zion, even to the Lord whose house is in Jerusalem, Let the Lord be praised.

< Zaburi 135 >