< Zaburi 132 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
Cantique de Mahaloth. Ô Eternel! souviens-toi de David, [et] de toute son affliction.
2 Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
Lequel a juré à l'Eternel, [et] fait vœu au Puissant de Jacob, [en disant]:
3 “Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
Si j'entre au Tabernacle de ma maison, [et] si je monte sur le lit où je couche;
4 sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
Si je donne du sommeil à mes yeux, [si je laisse] sommeiller mes paupières,
5 mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
Jusqu’à ce que j'aurai trouvé un lieu à l'Eternel, [et] des pavillons pour le Puissant de Jacob.
6 Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
Voici, nous avons ouï parler d'elle vers Ephrat, nous l'avons trouvée aux champs de Jahar.
7 “Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
Nous entrerons dans ses pavillons, [et] nous nous prosternerons devant son marchepied.
8 inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
Lève-toi, ô Eternel! [pour venir] en ton repos, toi, et l'Arche de ta force.
9 Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
Que tes Sacrificateurs soient revêtus de la justice, et que tes bien-aimés chantent de joie.
10 Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
Pour l'amour de David ton serviteur, ne fais point que ton Oint tourne le visage en arrière.
11 Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
L'Eternel a juré en vérité à David, [et] il ne se rétractera point, [disant]: je mettrai du fruit de ton ventre sur ton trône.
12 kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
Si tes enfants gardent mon alliance, et mon témoignage, que je leur enseignerai, leurs fils aussi seront assis à perpétuité sur ton trône.
13 Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
Car l'Eternel a choisi Sion; il l'a préférée pour être son siège.
14 “Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
Elle est, [dit-il], mon repos à perpétuité; j'y demeurerai, parce que je l'ai chérie.
15 Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
Je bénirai abondamment ses vivres; je rassasierai de pain ses pauvres.
16 Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
Et je revêtirai ses Sacrificateurs de délivrance; et ses bien-aimés chanteront avec des transports.
17 “Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
Je ferai qu'en elle germera une corne à David; je préparerai une lampe à mon Oint.
18 Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”
Je revêtirai de honte ses ennemis, et son diadème fleurira sur lui.

< Zaburi 132 >