< Zaburi 130 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
Canticum graduum. De profundis clamavi ad te Domine:
2 Ee Bwana, sikia sauti yangu. Masikio yako na yawe masikivu kwa kilio changu unihurumie.
Domine exaudi vocem meam: Fiant aures tuæ intendentes, in vocem deprecationis meæ.
3 Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi, Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
Si iniquitates observaveris Domine: Domine quis sustinebit?
4 Lakini kwako kuna msamaha, kwa hiyo wewe unaogopwa.
Quia apud te propitiatio est: et propter legem tuam sustinui te Domine. Sustinuit anima mea in verbo eius:
5 Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea, katika neno lake naweka tumaini langu.
speravit anima mea in Domino.
6 Nafsi yangu inamngojea Bwana kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi, naam, kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi.
A custodia matutina usque ad noctem: speret Israel in Domino.
7 Ee Israeli, mtumaini Bwana, maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma, na kwake kuna ukombozi kamili.
Quia apud Dominum misericordia: et copiosa apud eum redemptio.
8 Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli kutoka dhambi zao zote.
Et ipse redimet Israel, ex omnibus iniquitatibus eius.

< Zaburi 130 >