< Zaburi 13 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Mpaka lini, Ee Bwana? Je, utanisahau milele? Utanificha uso wako mpaka lini? 2 Nitapambana na mawazo yangu mpaka lini, na kila siku kuwa na majonzi moyoni mwangu? Adui zangu watanishinda mpaka lini? 3 Nitazame, unijibu, Ee Bwana Mungu wangu. Yatie nuru macho yangu, ama sivyo nitalala usingizi wa mauti. 4 Adui yangu atasema, “Nimemshinda,” nao adui zangu watashangilia nitakapoanguka. 5 Lakini ninategemea upendo wako usiokoma; moyo wangu unashangilia katika wokovu wako. 6 Nitamwimbia Bwana, kwa kuwa amekuwa mwema kwangu.

< Zaburi 13 >