< Zaburi 129 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Wamenionea mno tangu ujana wangu; Israeli na aseme sasa:
Cantique de Maaloth. Ils m'ont fort tourmenté dès ma jeunesse, peut bien dire Israël.
2 wamenionea mno tangu ujana wangu, lakini bado hawajanishinda.
Ils m'ont fort tourmenté dès ma jeunesse, mais ils n'ont pas prévalu sur moi.
3 Wakulima wamelima mgongo wangu, na kufanya mifereji yao mirefu.
Des laboureurs ont labouré mon dos; ils y ont tracé tout au long leurs sillons.
4 Lakini Bwana ni mwenye haki; amenifungua toka kamba za waovu.
L'Éternel est juste; il a coupé les cordes des méchants.
5 Wale wote waichukiao Sayuni na warudishwe nyuma kwa aibu.
Tous ceux qui haïssent Sion seront rendus honteux et repoussés en arrière.
6 Wawe kama majani juu ya paa, ambayo hunyauka kabla hayajakua;
Ils seront comme l'herbe des toits, qui sèche avant qu'elle monte en tuyau;
7 kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake, wala akusanyaye kujaza mikono yake.
Dont le moissonneur ne remplit pas sa main, ni le lieur de gerbes ses bras;
8 Wale wapitao karibu na wasiseme, “Baraka ya Bwana iwe juu yako; tunakubariki katika jina la Bwana.”
Et dont les passants ne disent pas: La bénédiction de l'Éternel soit sur vous! Nous vous bénissons au nom de l'Éternel!

< Zaburi 129 >