< Zaburi 129 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Wamenionea mno tangu ujana wangu; Israeli na aseme sasa:
Many a time have they afflicted me from my youth, may Israel now say:
2 wamenionea mno tangu ujana wangu, lakini bado hawajanishinda.
Many a time have they afflicted me from my youth: yet they have not prevailed against me.
3 Wakulima wamelima mgongo wangu, na kufanya mifereji yao mirefu.
The plowers plowed upon my back: they made long their furrows.
4 Lakini Bwana ni mwenye haki; amenifungua toka kamba za waovu.
Yhwh is righteous: he hath cut asunder the cords of the wicked.
5 Wale wote waichukiao Sayuni na warudishwe nyuma kwa aibu.
Let them all be confounded and turned back that hate Zion.
6 Wawe kama majani juu ya paa, ambayo hunyauka kabla hayajakua;
Let them be as the grass upon the housetops, which withereth afore it groweth up:
7 kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake, wala akusanyaye kujaza mikono yake.
Wherewith the mower filleth not his hand; nor he that bindeth sheaves his bosom.
8 Wale wapitao karibu na wasiseme, “Baraka ya Bwana iwe juu yako; tunakubariki katika jina la Bwana.”
Neither do they which go by say, The blessing of Yhwh be upon you: we bless you in the name of Yhwh.

< Zaburi 129 >