< Zaburi 124 >

1 Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi. Kama Bwana asingalikuwa upande wetu; Israeli na aseme sasa:
[A Song of Ascents. By David.] If it had not been Jehovah who was on our side, let Israel now say,
2 kama Bwana asingalikuwa upande wetu, wakati watu walipotushambulia,
if it had not been Jehovah who was on our side, when men rose up against us;
3 wakati hasira yao ilipowaka dhidi yetu, wangalitumeza tungali hai,
then they would have swallowed us up alive, when their wrath was kindled against us;
4 mafuriko yangalitugharikisha, maji mengi yangalitufunika,
then the waters would have overwhelmed us, the stream would have gone over our soul;
5 maji yaendayo kasi yangalituchukua.
then the proud waters would have gone over our soul.
6 Bwana asifiwe, yeye ambaye hakuruhusu turaruliwe kwa meno yao.
Blessed be Jehovah, who has not given us as a prey to their teeth.
7 Tumeponyoka kama ndege kutoka mtego wa mwindaji; mtego umevunjika, nasi tukaokoka.
Our soul has escaped like a bird out of the fowler's snare. The snare is broken, and we have escaped.
8 Msaada wetu ni katika jina la Bwana, Muumba wa mbingu na dunia.
Our help is in the name of Jehovah, who made heaven and earth.

< Zaburi 124 >