< Zaburi 116 >

1 Ninampenda Bwana kwa maana amesikia sauti yangu; amesikia kilio changu ili anihurumie.
I love Yahweh because he hears my voice and my pleas for mercy.
2 Kwa sababu amenitegea sikio lake, nitamwita siku zote za maisha yangu.
Because he listened to me, I will call on him as long as I live.
3 Kamba za mauti zilinizunguka, maumivu makuu ya kuzimu yalinipata, nikalemewa na taabu na huzuni. (Sheol h7585)
The cords of death surrounded me, and the snares of Sheol confronted me; I felt anguish and sorrow. (Sheol h7585)
4 Ndipo nikaliitia jina la Bwana: “Ee Bwana, niokoe!”
Then I called on the name of Yahweh: “Please Yahweh, rescue my life.”
5 Bwana ni mwenye neema na haki, Mungu wetu ni mwingi wa huruma.
Yahweh is merciful and fair; our God is compassionate.
6 Bwana huwalinda wanyenyekevu, nilipokuwa katika shida kubwa, aliniokoa.
Yahweh protects the naive; I was brought low, and he saved me.
7 Ee nafsi yangu, tulia tena, kwa kuwa Bwana amekuwa mwema kwako.
My soul can return to its resting place, for Yahweh has been good to me.
8 Kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umeniokoa nafsi yangu na mauti, macho yangu kutokana na machozi, miguu yangu kutokana na kujikwaa,
For you rescued my life from death, my eyes from tears, and my feet from stumbling.
9 ili niweze kutembea mbele za Bwana, katika nchi ya walio hai.
I will serve Yahweh in the land of the living.
10 Niliamini, kwa hiyo nilisema, “Mimi nimeteseka sana.”
I believed in him, even when I said, “I am greatly afflicted.”
11 Katika taabu yangu nilisema, “Wanadamu wote ni waongo.”
In my confusion I said, “All men are liars.”
12 Nimrudishie Bwana nini kwa wema wake wote alionitendea?
How can I repay Yahweh for all his kindnesses to me?
13 Nitakiinua kikombe cha wokovu na kulitangaza jina la Bwana.
I will raise the cup of salvation, and call on the name of Yahweh.
14 Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote.
I will fulfill my vows to Yahweh in the presence of all his people.
15 Kifo cha watakatifu kina thamani machoni pa Bwana.
Precious in the sight of Yahweh is the death of his saints.
16 Ee Bwana, hakika mimi ni mtumishi wako, mimi ni mtumishi wako, mwana wa mjakazi wako; umeniweka huru toka katika minyororo yangu.
Yahweh, indeed, I am your servant; I am your servant, the son of your servant woman; you have taken away my bonds.
17 Nitakutolea dhabihu ya kukushukuru na kuliita jina la Bwana.
I will offer to you the sacrifice of thanksgiving and will call on the name of Yahweh.
18 Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote,
I will fulfill my vows to Yahweh in the presence of all his people,
19 katika nyua za nyumba ya Bwana, katikati yako, ee Yerusalemu. Msifuni Bwana.
in the courts of Yahweh's house, in your midst, Jerusalem. Praise Yahweh.

< Zaburi 116 >