< Zaburi 114 >

1 Wakati Israeli walipotoka Misri, nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
When Israel went forth out of Egypt, the house of Jacob from a people of foreign language;
2 Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu, Israeli akawa milki yake.
Judah became his sanctuary, Israel his dominion.
3 Bahari ilitazama ikakimbia, Yordani ulirudi nyuma,
The sea saw it, and fled. The Jordan was driven back.
4 milima ilirukaruka kama kondoo dume, vilima kama wana-kondoo.
The mountains skipped like rams, the little hills like lambs.
5 Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia, nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
What was it, you sea, that you fled? You Jordan, that you turned back?
6 enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume, enyi vilima, kama wana-kondoo?
You mountains, that you skipped like rams; you little hills, like lambs?
7 Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana, mbele za Mungu wa Yakobo,
Tremble, you earth, at the presence of the Lord, at the presence of the God of Jacob,
8 aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji, mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.
who turned the rock into a pool of water, the flint into a spring of waters.

< Zaburi 114 >