< Zaburi 111 >

1 Msifuni Bwana. Nitamtukuza Bwana kwa moyo wangu wote, katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko.
Praise Yahweh. I will give thanks to Yahweh with my whole heart in the assembly of the upright, in their gathering.
2 Kazi za Bwana ni kuu, wote wanaopendezwa nazo huzitafakari.
The works of Yahweh are great, eagerly awaited by all those who desire them.
3 Kazi zake zimejaa fahari na utukufu, haki yake hudumu daima.
His work is majestic and glorious, and his righteousness endures forever.
4 Amefanya maajabu yake yakumbukwe, Bwana ni mwenye neema na huruma.
He does wonderful things that will be remembered; Yahweh is gracious and merciful.
5 Huwapa chakula wale wanaomcha, hulikumbuka agano lake milele.
He gives food to his faithful followers. He will always call to mind his covenant.
6 Amewaonyesha watu wake uwezo wa kazi zake, akiwapa nchi za mataifa mengine.
He showed his powerful works to his people in giving them the inheritance of the nations.
7 Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki, mausia yake yote ni ya kuaminika.
The works of his hands are trustworthy and just; all his instructions are reliable.
8 Zinadumu milele na milele, zikifanyika kwa uaminifu na unyofu.
They are established forever, to be observed faithfully and properly.
9 Aliwapa watu wake ukombozi, aliamuru agano lake milele: jina lake ni takatifu na la kuogopwa.
He gave victory to his people; he ordained his covenant forever; holy and awesome is his name.
10 Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, wote wanaozifuata amri zake wana busara. Sifa zake zadumu milele.
To honor Yahweh is the beginning of wisdom; those who carry out his instructions have good understanding. His praise endures forever.

< Zaburi 111 >