< Zaburi 111 >

1 Msifuni Bwana. Nitamtukuza Bwana kwa moyo wangu wote, katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko.
Hallelujah. I will thank the Lord with all my heart, in the assembled congregation of his people.
2 Kazi za Bwana ni kuu, wote wanaopendezwa nazo huzitafakari.
Great are the things that the Lord has done, worthy of study by those who love them.
3 Kazi zake zimejaa fahari na utukufu, haki yake hudumu daima.
Majestic and glorious is his work, and his righteousness abides forever.
4 Amefanya maajabu yake yakumbukwe, Bwana ni mwenye neema na huruma.
For his marvellous deeds he has won renown; the Lord is gracious and full of compassion.
5 Huwapa chakula wale wanaomcha, hulikumbuka agano lake milele.
Food he gives to those who fear him, always he remembers his covenant.
6 Amewaonyesha watu wake uwezo wa kazi zake, akiwapa nchi za mataifa mengine.
His mighty works he has shown to his people, in giving to them the nations for heritage.
7 Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki, mausia yake yote ni ya kuaminika.
All that he does is faithful and right, all his behests are firm and sure.
8 Zinadumu milele na milele, zikifanyika kwa uaminifu na unyofu.
They are established for ever and ever, executed with truth and uprightness.
9 Aliwapa watu wake ukombozi, aliamuru agano lake milele: jina lake ni takatifu na la kuogopwa.
To his people he sent redemption, he has appointed his covenant forever. His name is holy and awe-inspiring.
10 Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, wote wanaozifuata amri zake wana busara. Sifa zake zadumu milele.
The fear of the Lord is the beginning of wisdom those who keep it are wise indeed. His praise abides for ever and ever.

< Zaburi 111 >