< Zaburi 111 >

1 Msifuni Bwana. Nitamtukuza Bwana kwa moyo wangu wote, katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko.
Praise JAH. I will give thanks to Jehovah with my whole heart, in the council of the upright, and in the congregation.
2 Kazi za Bwana ni kuu, wote wanaopendezwa nazo huzitafakari.
Jehovah's works are great, pondered by all those who delight in them.
3 Kazi zake zimejaa fahari na utukufu, haki yake hudumu daima.
His work is honor and majesty. His righteousness endures forever.
4 Amefanya maajabu yake yakumbukwe, Bwana ni mwenye neema na huruma.
He has caused his wonderful works to be remembered. Jehovah is gracious and merciful.
5 Huwapa chakula wale wanaomcha, hulikumbuka agano lake milele.
He has given food to those who fear him. He always remembers his covenant.
6 Amewaonyesha watu wake uwezo wa kazi zake, akiwapa nchi za mataifa mengine.
He has shown his people the power of his works, in giving them the heritage of the nations.
7 Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki, mausia yake yote ni ya kuaminika.
The works of his hands are truth and justice. All his precepts are sure.
8 Zinadumu milele na milele, zikifanyika kwa uaminifu na unyofu.
They are established forever and ever. They are done in truth and uprightness.
9 Aliwapa watu wake ukombozi, aliamuru agano lake milele: jina lake ni takatifu na la kuogopwa.
He has sent redemption to his people. He has ordained his covenant forever. His name is holy and awesome.
10 Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, wote wanaozifuata amri zake wana busara. Sifa zake zadumu milele.
The fear of Jehovah is the beginning of wisdom. All those who do his work have a good understanding. His praise endures forever.

< Zaburi 111 >