< Zaburi 11 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Kwa Bwana ninakimbilia, unawezaje basi kuniambia: “Ruka kama ndege kwenye mlima wako.
For the chief musician. A psalm of David. I take refuge in Yahweh; how will you say to me, “Flee like a bird to the mountain”?
2 Hebu tazama, waovu wanapinda pinde zao, huweka mishale kwenye uzi wake, wakiwa gizani ili kuwapiga wale wanyofu wa moyo.
For see! The wicked prepare their bows. They make ready their arrows on the strings to shoot in the darkness at the upright in heart.
3 Wakati misingi imeharibiwa, mwenye haki anaweza kufanya nini?”
For if the foundations are ruined, what can the righteous do?
4 Bwana yuko ndani ya Hekalu lake takatifu; Bwana yuko kwenye kiti chake cha enzi mbinguni. Huwaangalia wana wa watu, macho yake yanawajaribu.
Yahweh is in his holy temple; his eyes watch, his eyes examine the children of mankind.
5 Bwana huwajaribu wenye haki, lakini waovu na wanaopenda jeuri, nafsi yake huwachukia.
Yahweh examines both the righteous and the wicked, but he hates those who love to do violence.
6 Atawanyeshea waovu makaa ya moto mkali na kiberiti kinachowaka, upepo wenye joto kali ndio fungu lao.
He rains burning coals and brimstone upon the wicked; a scorching wind will be their portion from his cup!
7 Kwa kuwa Bwana ni mwenye haki, yeye hupenda haki. Wanyofu watauona uso wake.
For Yahweh is righteous, and he loves righteousness; the upright will see his face.

< Zaburi 11 >