< Zaburi 108 >

1 Wimbo. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
A Song. A Psalm by David. My heart is steadfast, God. I will sing and I will make music with my soul.
2 Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
Wake up, harp and lyre! I will wake up the dawn.
3 Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
I will give thanks to you, LORD, amongst the nations. I will sing praises to you amongst the peoples.
4 Kwa maana upendo wako ni mkuu, ni juu kuliko mbingu; uaminifu wako unazifikia anga.
For your loving kindness is great above the heavens. Your faithfulness reaches to the skies.
5 Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
Be exalted, God, above the heavens! Let your glory be over all the earth.
6 Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume, ili wale uwapendao wapate kuokolewa.
That your beloved may be delivered, save with your right hand, and answer us.
7 Mungu amenena kutoka patakatifu pake: “Nitaigawa Shekemu kwa ushindi na kulipima Bonde la Sukothi.
God has spoken from his sanctuary: “In triumph, I will divide Shechem, and measure out the valley of Succoth.
8 Gileadi ni yangu, Manase ni yangu, Efraimu ni kofia yangu ya chuma, nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.
Gilead is mine. Manasseh is mine. Ephraim also is my helmet. Judah is my sceptre.
9 Moabu ni sinia langu la kunawia, juu ya Edomu natupa kiatu changu; nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”
Moab is my wash pot. I will toss my sandal on Edom. I will shout over Philistia.”
10 Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome? Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?
Who will bring me into the fortified city? Who will lead me to Edom?
11 Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi, na hutoki tena na majeshi yetu?
Haven’t you rejected us, God? You don’t go out, God, with our armies.
12 Tuletee msaada dhidi ya adui, kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.
Give us help against the enemy, for the help of man is vain.
13 Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi, naye atawaponda adui zetu.
Through God, we will do valiantly, for it is he who will tread down our enemies.

< Zaburi 108 >