< Zaburi 107 >

1 Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
Give thanks to the LORD, for he is good, for his loving kindness endures forever.
2 Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
Let the redeemed by the LORD say so, whom he has redeemed from the hand of the adversary,
3 wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
And gathered out of the lands, from the east and from the west, from the north and from the south.
4 Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
They wandered in the wilderness in a desert way. They found no city to live in.
5 Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
Hungry and thirsty, their soul fainted in them.
6 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Then they cried to the LORD in their trouble, and he delivered them out of their distresses,
7 Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
he led them also by a straight way, that they might go to a city to live in.
8 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Let them praise the LORD for his loving kindness, for his wonderful works for the descendants of Adam.
9 kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
For he satisfies the longing soul. He fills the hungry soul with good.
10 Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
Some sat in darkness and in the shadow of death, being bound in affliction and iron,
11 kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
because they rebelled against the words of God, and condemned the counsel of the Most High.
12 Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
Therefore he brought down their heart with labor. They fell down, and there was none to help.
13 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Then they cried to the LORD in their trouble, and he saved them out of their distresses.
14 Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
He brought them out of darkness and the shadow of death, and broke their bonds in sunder.
15 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
Let them praise the LORD for his loving kindness, for his wonderful works for the descendants of Adam.
16 kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
For he has broken the gates of bronze, and cut through bars of iron.
17 Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
Fools are afflicted because of their disobedience, and because of their iniquities.
18 Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
Their soul abhors all kinds of food. They draw near to the gates of death.
19 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Then they cried to the LORD in their trouble; he saved them out of their distresses.
20 Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
He sent his word and healed them; he delivered them from their traps.
21 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Let them praise the LORD for his loving kindness, for his wonderful works for the descendants of Adam.
22 Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
Let them offer the sacrifices of thanksgiving, and declare his works with singing.
23 Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
Those who go down to the sea in ships, who do business in great waters;
24 Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
These see the LORD's works, and his wonders in the deep.
25 Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
For he commands, and raises the stormy wind, which lifts up its waves.
26 Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
They mount up to the sky; they go down again to the depths. Their soul melts away because of trouble.
27 Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
They reel back and forth, and stagger like a drunken man, and are at their wits' end.
28 Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
Then they cry to the LORD in their trouble, and he brings them out of their distress.
29 Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
He makes the storm a calm, so that its waves are still.
30 Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
Then they are glad because it is calm, so he brings them to their desired haven.
31 Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Let them praise the LORD for his loving kindness, for his wonderful works for the descendants of Adam.
32 Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
Let them exalt him also in the assembly of the people, and praise him in the seat of the elders.
33 Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
He turns rivers into a desert, water springs into a thirsty ground,
34 nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
and a fruitful land into a salt waste, for the wickedness of those who dwell in it.
35 Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
He turns a desert into a pool of water, and a dry land into water springs.
36 aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
There he makes the hungry live, that they may prepare a city to live in,
37 Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
sow fields, plant vineyards, and reap the fruits of increase.
38 Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
He blesses them also, so that they are multiplied greatly. He doesn't allow their livestock to decrease.
39 Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
Again, they are diminished and bowed down through oppression, trouble, and sorrow.
40 Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
He pours contempt on princes, and causes them to wander in a trackless waste.
41 Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
Yet he lifts the needy out of their affliction, and increases their families like a flock.
42 Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
The upright will see it, and be glad. All the wicked will shut their mouths.
43 Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.
Whoever is wise will pay attention to these things. They will consider the loving kindnesses of the LORD.

< Zaburi 107 >