< Zaburi 106 >

1 Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
Hallelujah! Bekennet Jehovah, denn Er ist gut, denn Seine Barmherzigkeit ist in Ewigkeit.
2 Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
Wer kann aussagen die Machttaten Jehovahs, kann hören lassen all Sein Lob?
3 Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
Selig, die das Recht halten und Gerechtigkeit tun alle Zeit!
4 Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
Gedenke mein, Jehovah, mit dem Wohlgefallen für Dein Volk, und suche mich heim mit Deinem Heil.
5 ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
Daß ich sehe das Gute Deiner Auserwählten, daß ich fröhlich sei in der Fröhlichkeit Deiner Völkerschaften, mich rühme mit Deinem Erbe.
6 Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
Wir sündigten mit unseren Vätern, wir haben Missetat, Ungerechtigkeit begangen.
7 Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
Unsere Väter in Ägypten begriffen Deine Wunder nicht, gedachten nicht Deiner vielen Barmherzigkeit, und sie widersetzten sich am Meer, am Meere des Schilfs.
8 Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
Er aber rettete sie um Seines Namens willen, um Seine Macht kund zu tun.
9 Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
Und Er bedrohte das Schilfmeer, und es trocknete aus, und Er ließ sie durch Abgründe gehen wie durch die Wüste.
10 Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
Und Er rettete sie aus des Hassers Hand, und aus des Feindes Hand erlöste Er sie.
11 Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
Und Wasser bedeckten ihre Dränger, nicht einer blieb von ihnen übrig.
12 Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
Und sie glaubten an Seine Worte, sie sangen Sein Lob.
13 Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
Eilig hatten Seine Werke sie vergessen, warteten nicht auf Seinen Ratschluß.
14 Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
Und es gelüstete sie in der Wüste ein Gelüste, und sie versuchten Gott im Wüstenland.
15 Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
Und Er gab ihnen ihr Erbetenes, sandte aber Magerkeit in ihre Seele.
16 Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
Und sie eiferten wider Mose in dem Lager, wider Aharon, den Heiligen Jehovahs.
17 Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
Die Erde tat sich auf und verschlang Dathan und überdeckte Abirams Gemeinde.
18 Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
Und es brannte Feuer in ihrer Gemeinde, und die Flamme entflammte die Ungerechten.
19 Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
Am Choreb machten sie ein Kalb und beteten das Gußbild an,
20 Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
Und sie vertauschten ihre Herrlichkeit mit dem Vorbilde eines Ochsen, der das Kraut frißt.
21 Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
Sie vergaßen des Gottes, Der sie gerettet, Der in Ägypten Großes tat.
22 miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
Wunder im Lande Cham, Furchtbares an dem Meere des Schilfs.
23 Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
Und Er sagte, Er wollte sie vernichten, wenn Mose, Sein Auserwählter, nicht vor Ihm vor den Riß gestanden wäre, um Seinen Grimm vom Verderben zurückzuwenden.
24 Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
Und sie verschmähten das begehrte Land, sie glaubten Seinem Worte nicht.
25 Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
Und sie beschwerten sich in ihren Zelten, und hörten nicht auf Jehovahs Stimme.
26 Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
Und Er hob Seine Hand auf wider sie, sie zu fällen in der Wüste.
27 kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
Und ihren Samen unter die Völkerschaften fallen zu lassen, und sie in die Länder zu zersprengen.
28 Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
Und sie klammerten sich an Baal-Peor und aßen die Opfer der Toten.
29 Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
Und reizten Ihn durch ihr Tun, daß eine Plage ausbrach unter ihnen.
30 Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
Und Phinechas stand da und schlichtete, und der Plage ward Einhalt getan.
31 Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
Und ihm ward es zur Gerechtigkeit gerechnet ins Geschlecht und Geschlecht in Ewigkeit.
32 Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
Und sie reizten zur Entrüstung am Wasser Meribah, und es war übel mit Mose um ihretwillen.
33 kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
Denn sie erbitterten den Geist ihm, und es entfuhr seinen Lippen.
34 Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
Sie vernichteten die Völker nicht, wie Jehovah zu ihnen gesprochen hatte,
35 bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
Und vermengten sich mit den Völkerschaften und lernten ihr Tun;
36 Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
Und sie dienten ihren Götzenbildern und sie wurden ihnen zum Fallstrick.
37 Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
Und sie opferten den Dämonen ihre Söhne und Töchter.
38 Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
Und sie vergossen unschuldig Blut, das Blut ihrer Söhne und ihrer Töchter, die sie den Götzenbildern Kanaans opferten, und das Land ward durch Blut entheiligt.
39 Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
Und sie verunreinigten sich durch ihre Werke, und buhlten durch ihr Tun.
40 Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
Und es entbrannte Jehovahs Zorn wider Sein Volk, und Sein Erbe ward Ihm zum Greuel.
41 Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
Und Er gab sie in der Völkerschaften Hand, und ihre Hasser herrschten über sie.
42 Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
Und ihre Feinde unterdrückten sie, und sie wurden unter ihre Hand gebeugt.
43 Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
Viel Male errettete Er sie, doch sie widersetzten sich in ihrem Ratschlusse, und schwanden dahin in ihrer Missetat.
44 Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
Und Er sah ihre Drangsal, wie Er ihren Angstschrei hörte.
45 kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
Und Er gedachte ihnen an Seinen Bund, und es gereute Ihn nach Seiner vielen Barmherzigkeit.
46 Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
Und Er ließ sie Erbarmen finden vor allen, die sie gefangen führten.
47 Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
Rette uns, Jehovah, unser Gott, und bringe uns zusammen aus den Völkerschaften, auf daß wir bekennen den Namen Deiner Heiligkeit und preisen Dein Lob.
48 Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.
Gesegnet sei Jehovah, der Gott Israels, von Ewigkeit und zu Ewigkeit! und alles Volk spreche: Amen. Hallelujah!

< Zaburi 106 >