< Zaburi 106 >

1 Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
Alléluia! Rendez hommage à l’Eternel, car sa grâce dure à jamais.
2 Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
Qui saura dire la toute-puissance de l’Eternel, exprimer toute sa gloire?
3 Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
Heureux ceux qui respectent le droit, pratiquent la justice en tout temps!
4 Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
Souviens-toi de moi, ô Eternel, dans ta bienveillance pour ton peuple, veille sur moi, par ta protection,
5 ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
pour que je puisse voir le bonheur de tes élus, me réjouir de la joie de ton peuple, me glorifier de concert avec ton héritage.
6 Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
Nous avons péché tout comme nos pères, nous avons mal agi, nous sommes coupables!
7 Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
Nos pères, en Egypte, n’ont pas compris tes miracles, ni gardé le souvenir de tes nombreux bienfaits! Ils se révoltèrent aux bords de la mer, de la mer des Joncs.
8 Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
Lui cependant les secourut à cause de son nom, pour faire connaître sa puissance.
9 Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
Il apostropha la mer des Joncs, et elle se dessécha, il leur fit traverser les flots comme une terre nue.
10 Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
Il leur porta secours contre l’oppresseur, les délivra de la main de l’ennemi.
11 Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
Les eaux recouvrirent leurs persécuteurs, pas un d’entre eux n’en réchappa.
12 Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
Alors ils eurent foi en ses paroles, et chantèrent ses louanges.
13 Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
Bien vite ils oublièrent ses œuvres; ils ne mirent pas leur attente dans ses desseins.
14 Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
Ils furent pris d’ardentes convoitises dans le désert, et mirent Dieu à l’épreuve dans la solitude.
15 Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
Il leur accorda ce qu’ils réclamaient, mais envoya la consomption dans leurs organes.
16 Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
Ils furent jaloux de Moïse dans le camp, d’Aaron, le saint de l’Eternel.
17 Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
La terre, s’entrouvrant, engloutit Dathan, elle se referma sur la bande d’Abirâm.
18 Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
Un feu consuma leur troupe, une flamme embrasa les impies.
19 Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
Ils fabriquèrent un veau près du Horeb, et se prosternèrent devant une idole en fonte.
20 Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
Ils troquèrent ainsi leur gloire contre l’effigie d’un bœuf qui broute l’herbe.
21 Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
Ils avaient oublié Dieu, leur sauveur, qui avait accompli de si grandes choses en Egypte,
22 miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
des merveilles dans le pays de Cham, de formidables prodiges près de la mer des Joncs.
23 Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
Il parlait de les anéantir, si Moïse, son élu, ne se fût placé sur la brèche devant lui, pour détourner sa colère prête à tout détruire.
24 Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
Puis ils montrèrent du dédain pour un pays délicieux, n’ayant pas foi en sa parole.
25 Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
Ils murmurèrent dans leurs tentes, n’écoutèrent point la voix de l’Eternel;
26 Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
et il leva la main contre eux pour jurer qu’il les ferait succomber dans le désert,
27 kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
qu’il rejetterait leurs descendants parmi les nations, et les disperserait dans leurs contrées.
28 Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
Ils se prostituèrent à Baal-Peor, et mangèrent des sacrifices offerts à des dieux inanimés.
29 Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
Ils déchaînèrent la colère par leurs actes, et un fléau fit irruption parmi eux.
30 Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
Mais Phinéas se leva pour faire justice, et le fléau cessa de sévir.
31 Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
Cette action lui fut comptée comme un mérite, d’âge en âge, jusque dans l’éternité.
32 Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
Ils suscitèrent le courroux divin aux eaux de Meriba, et il advint du mal à Moïse à cause d’eux.
33 kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
Car ils furent rebelles à l’esprit de Dieu, et ses lèvres prononcèrent l’arrêt.
34 Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
Ils n’exterminèrent point les nations que l’Eternel leur avait désignées.
35 bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
Ils se mêlèrent aux peuples et s’inspirèrent de leurs coutumes,
36 Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
adorant leurs idoles, qui devinrent pour eux un piège.
37 Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
Ils sacrifièrent leurs fils et leurs filles aux démons,
38 Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
répandirent du sang innocent, le sang de leurs fils et de leurs filles, qu’ils immolaient aux idoles de Canaan, et le pays fut déshonoré par des flots de sang.
39 Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
Ils se souillèrent par leurs œuvres, et leurs actes furent une longue prostitution.
40 Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
La colère de l’Eternel s’alluma contre son peuple, et il prit en horreur son héritage.
41 Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
Il les livra au pouvoir des nations, ceux qui les haïssaient devinrent leurs maîtres.
42 Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
Leurs ennemis les opprimèrent, et les firent plier sous leur joug.
43 Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
Maintes fois Dieu les délivra, mais ils redevenaient rebelles de propos délibéré, et tombaient en décadence par leurs fautes.
44 Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
Il devenait attentif à leur détresse, quand il entendait leurs supplications,
45 kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
se souvenant, pour leur bien, de son alliance, et se laissant fléchir dans son infinie miséricorde.
46 Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
Il émouvait la pitié en leur faveur chez tous ceux qui les retenaient captifs.
47 Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
Viens à notre secours, Eternel, notre Dieu, rassemble-nous d’entre les nations, pour que nous rendions hommage à ton saint nom, et cherchions notre gloire dans tes louanges.
48 Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.
Béni soit l’Eternel, le Dieu d’Israël, d’éternité en éternité, et que le peuple tout entier dise: "Amen! Alléluia!"

< Zaburi 106 >