< Zaburi 106 >

1 Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
Praise ye Jehovah. Oh give thanks unto Jehovah; for he is good; For his lovingkindness [endureth] for ever.
2 Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
Who can utter the mighty acts of Jehovah, Or show forth all his praise?
3 Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
Blessed are they that keep justice, And he that doeth righteousness at all times.
4 Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
Remember me, O Jehovah, with the favor that thou bearest unto thy people; Oh visit me with thy salvation,
5 ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
That I may see the prosperity of thy chosen, That I may rejoice in the gladness of thy nation, That I may glory with thine inheritance.
6 Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
We have sinned with our fathers, We have committed iniquity, we have done wickedly.
7 Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
Our fathers understood not thy wonders in Egypt; They remembered not the multitude of thy lovingkindnesses, But were rebellious at the sea, even at the Red Sea.
8 Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
Nevertheless he saved them for his name’s sake, That he might make his mighty power to be known.
9 Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
He rebuked the Red Sea also, and it was dried up: So he led them through the depths, as through a wilderness.
10 Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
And he saved them from the hand of him that hated them, And redeemed them from the hand of the enemy.
11 Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
And the waters covered their adversaries; There was not one of them left.
12 Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
Then believed they his words; They sang his praise.
13 Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
They soon forgat his works; They waited not for his counsel,
14 Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
But lusted exceedingly in the wilderness, And tempted God in the desert.
15 Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
And he gave them their request, But sent leanness into their soul.
16 Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
They envied Moses also in the camp, [And] Aaron the saint of Jehovah.
17 Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
The earth opened and swallowed up Dathan, And covered the company of Abiram.
18 Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
And a fire was kindled in their company; The flame burned up the wicked.
19 Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
They made a calf in Horeb, And worshipped a molten image.
20 Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
Thus they changed their glory For the likeness of an ox that eateth grass.
21 Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
They forgat God their Saviour, Who had done great things in Egypt,
22 miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
Wondrous works in the land of Ham, [And] terrible things by the Red Sea.
23 Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
Therefore he said that he would destroy them, Had not Moses his chosen stood before him in the breach, To turn away his wrath, lest he should destroy [them].
24 Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
Yea, they despised the pleasant land, They believed not his word,
25 Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
But murmured in their tents, And hearkened not unto the voice of Jehovah.
26 Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
Therefore he sware unto them, That he would overthrow them in the wilderness,
27 kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
And that he would overthrow their seed among the nations, And scatter them in the lands.
28 Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
They joined themselves also unto Baal-peor, And ate the sacrifices of the dead.
29 Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
Thus they provoked him to anger with their doings; And the plague brake in upon them.
30 Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
Then stood up Phinehas, and executed judgment; And so the plague was stayed.
31 Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
And that was reckoned unto him for righteousness, Unto all generations for evermore.
32 Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
They angered him also at the waters of Meribah, So that it went ill with Moses for their sakes;
33 kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
Because they were rebellious against his spirit, And he spake unadvisedly with his lips.
34 Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
They did not destroy the peoples, As Jehovah commanded them,
35 bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
But mingled themselves with the nations, And learned their works,
36 Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
And served their idols, Which became a snare unto them.
37 Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
Yea, they sacrificed their sons and their daughters unto demons,
38 Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
And shed innocent blood, Even the blood of their sons and of their daughters, Whom they sacrificed unto the idols of Canaan; And the land was polluted with blood.
39 Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
Thus were they defiled with their works, And played the harlot in their doings.
40 Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
Therefore was the wrath of Jehovah kindled against his people, And he abhorred his inheritance.
41 Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
And he gave them into the hand of the nations; And they that hated them ruled over them.
42 Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
Their enemies also oppressed them, And they were brought into subjection under their hand.
43 Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
Many times did he deliver them; But they were rebellious in their counsel, And were brought low in their iniquity.
44 Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
Nevertheless he regarded their distress, When he heard their cry:
45 kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
And he remembered for them his covenant, And repented according to the multitude of his lovingkindnesses.
46 Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
He made them also to be pitied Of all those that carried them captive.
47 Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
Save us, O Jehovah our God, And gather us from among the nations, To give thanks unto thy holy name, And to triumph in thy praise.
48 Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.
Blessed be Jehovah, the God of Israel, From everlasting even to everlasting. And let all the people say, Amen. Praise ye Jehovah.

< Zaburi 106 >