< Zaburi 104 >

1 Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
Mon âme, bénis l'Éternel! Éternel, mon Dieu, tu es merveilleusement grand; tu es revêtu de splendeur et de majesté.
2 Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
Il s'enveloppe de lumière comme d'un vêtement; il étend les cieux comme une tenture.
3 na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
Il construit sa haute demeure avec les eaux; il fait des nuées son char; il se promène sur les ailes du vent.
4 Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
Il fait des vents ses messagers, des flammes de feu ses serviteurs.
5 Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
Il a posé la terre sur ses bases; elle est inébranlable à jamais.
6 Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
Tu l'avais couverte de l'abîme comme d'un vêtement; les eaux se tenaient sur les montagnes.
7 Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
A ta menace, elles se retirèrent; au bruit de ton tonnerre, elles s'enfuirent.
8 yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
Les montagnes s'élevèrent, les vallées s'abaissèrent au lieu que tu leur avais assigné.
9 Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
Tu as fixé pour les eaux une borne qu'elles ne passeront pas; elles ne reviendront pas couvrir la terre.
10 Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
Il envoie des sources dans les vallées, et elles courent entre les montagnes.
11 Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
Elles abreuvent toutes les bêtes des champs; les ânes sauvages y étanchent leur soif.
12 Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
Les oiseaux habitent sur leurs bords, faisant résonner leur voix dans le feuillage.
13 Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
De sa haute demeure, il abreuve les montagnes; la terre est rassasiée du fruit de tes œuvres.
14 Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
Il fait germer le foin pour le bétail et l'herbe pour le service de l'homme, faisant sortir la nourriture de la terre;
15 divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
Et le vin qui réjouit le cœur de l'homme et fait resplendir son visage plus que l'huile; et le pain qui soutient le cœur de l'homme.
16 Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
Les arbres de l'Éternel sont rassasiés, les cèdres du Liban qu'il a plantés.
17 Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
C'est là que les oiseaux font leurs nids; les cyprès sont la demeure de la cigogne;
18 Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
Les hautes montagnes sont pour les bouquetins; les rochers sont la retraite des lapins.
19 Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
Il a fait la lune pour marquer les temps; le soleil connaît son coucher.
20 Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
Tu amènes les ténèbres, et la nuit vient, où toutes les bêtes des forêts se promènent.
21 Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
Les lionceaux rugissent après la proie, et pour demander à Dieu leur pâture.
22 Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
Le soleil se lève; ils se retirent, et se couchent dans leurs tanières.
23 Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
Alors l'homme sort à son ouvrage, et à son travail jusqu'au soir.
24 Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
O Éternel, que tes œuvres sont en grand nombre! Tu les as toutes faites avec sagesse; la terre est pleine de tes richesses.
25 Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
Et cette grande et vaste mer! Là sont des animaux sans nombre, gros et petits.
26 Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
Là se promènent les navires, et ce Léviathan que tu as formé pour s'y jouer.
27 Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
Tous, ils s'attendent à toi, pour que tu leur donnes leur nourriture en son temps.
28 Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
Tu la leur donnes, et ils la recueillent; tu ouvres ta main, et ils sont rassasiés de biens.
29 Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
Caches-tu ta face? ils sont éperdus; retires-tu leur souffle? ils expirent, et retournent en leur poussière.
30 Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
Envoies-tu ton esprit? ils sont créés, et tu renouvelles la face de la terre.
31 Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
Que la gloire de l'Éternel dure à toujours! Que l'Éternel se réjouisse dans ses œuvres!
32 yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
Il regarde la terre et elle tremble; il touche les montagnes et elles fument.
33 Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
Je chanterai à l'Éternel tant que je vivrai; je psalmodierai à mon Dieu tant que j'existerai.
34 Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
Que ma méditation lui soit agréable! Je me réjouirai en l'Éternel.
35 Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.
Que les pécheurs disparaissent de la terre, et que les méchants ne soient plus! Mon âme, bénis l'Éternel! Louez l'Éternel!

< Zaburi 104 >