< Zaburi 102 >

1 Maombi ya mtu aliyechoka. Anapoteseka na kumimina malalamiko yake kwa Bwana. Ee Bwana, usikie maombi yangu, kilio changu cha kuomba msaada kikufikie.
Bēdu cilvēka lūgšana, kad tas ir noskumis un savas žēlabas izgāž Tā Kunga priekšā. Ak Kungs, klausi manu lūgšanu, un mana saukšana lai nāk pie Tevis.
2 Usinifiche uso wako ninapokuwa katika shida. Unitegee sikio lako, ninapoita, unijibu kwa upesi.
Neapslēp Savu vaigu priekš manis, atgriez Savu ausi pie manis bēdu laikā; tai dienā, kad es saucu, paklausi mani drīz.
3 Kwa kuwa siku zangu zinatoweka kama moshi, mifupa yangu inaungua kama kaa la moto.
Jo manas dienas ir iznīkušas kā dūmi, un mani kauli ir izdeguši kā pagale.
4 Moyo wangu umefifia na kunyauka kama jani, ninasahau kula chakula changu.
Mana sirds ir sasista un izkaltusi kā zāle, tā ka es aizmirstu pat savu maizi ēst.
5 Kwa sababu ya kusononeka kwangu kwa uchungu, nimebakia ngozi na mifupa.
Mani kauli līp pie manas miesas no kaukšanas un nopūšanās.
6 Nimekuwa kama bundi wa jangwani, kama bundi kwenye magofu.
Es esmu tā kā dumpis tuksnesī, es esmu kā apogs (pūce) izpostītās vietās.
7 Nilalapo sipati usingizi, nimekuwa kama ndege mpweke kwenye paa la nyumba.
Es esmu nomodā un tāpat kā vientulis putns uz jumta.
8 Mchana kutwa adui zangu hunidhihaki, wale wanaonizunguka hutumia jina langu kama laana.
Mani ienaidnieki mani nievā cauru dienu; kas pret mani trako, tie mani dara par lāsta vārdu.
9 Ninakula majivu kama chakula changu na nimechanganya kinywaji changu na machozi
Jo es ēdu pelnus kā maizi un sajaucu savu dzērienu ar asarām,
10 kwa sababu ya ghadhabu yako kuu, kwa maana umeniinua na kunitupa kando.
Tavas bardzības un dusmības pēc, jo Tu mani esi pacēlis un atkal nogāzis.
11 Siku zangu ni kama kivuli cha jioni, ninanyauka kama jani.
Manas dienas ir kā ēna pavakarē, un es kalstu kā zāle.
12 Lakini wewe, Ee Bwana, umeketi katika kiti chako cha enzi milele, sifa zako za ukuu zaendelea vizazi vyote.
Bet Tu, Kungs, paliec mūžīgi un Tava piemiņa līdz radu radiem.
13 Utainuka na kuihurumia Sayuni, kwa maana ni wakati wa kumwonyesha wema; wakati uliokubalika umewadia.
Kaut Tu celtos un apžēlotos par Ciānu, jo jau ir laiks par viņu apžēloties, jo tas nospriestais laiks ir atnācis.
14 Kwa maana mawe yake ni ya thamani kwa watumishi wako, vumbi lake lenyewe hulionea huruma.
Jo Tavi kalpi mīļo viņas akmeņus un žēlojās, ka tā guļ pīšļos.
15 Mataifa wataogopa jina la Bwana, wafalme wote wa dunia watauheshimu utukufu wako.
Tad pagāni bīsies Tā Kunga Vārdu, un visi ķēniņi virs zemes Tavu godību,
16 Kwa maana Bwana ataijenga tena Sayuni na kutokea katika utukufu wake.
Kad Tas Kungs Ciānu uztaisīs un parādīsies Savā godībā.
17 Ataitikia maombi ya mtu mkiwa, wala hatadharau hoja yao.
Viņš griežas pie bēdu ļaužu lūgšanas un nenicina pielūgšanu.
18 Hili na liandikwe kwa ajili ya kizazi kijacho, ili taifa litakaloumbwa baadaye waweze kumsifu Bwana:
Lai tas top uzrakstīts pēcnākamiem, un tie ļaudis, kas vēl taps radīti, slavēs To Kungu.
19 “Bwana alitazama chini kutoka patakatifu pake palipo juu, kutoka mbinguni alitazama dunia,
Jo Viņš skatās no Sava svēta augstuma, Tas Kungs lūko no debesīm uz zemi,
20 kusikiliza vilio vya uchungu vya wafungwa na kuwaweka huru wale waliohukumiwa kufa.”
Ka Viņš dzird cietumnieku nopūšanos un atsvabina nāves bērnus;
21 Kwa hiyo jina la Bwana latangazwa huko Sayuni na sifa zake katika Yerusalemu,
Ka Tā Kunga vārds top sludināts Ciānā un Viņa slava Jeruzālemē,
22 wakati mataifa na falme zitakapokusanyika ili kumwabudu Bwana.
Kad tautas sapulcējās kopā un valstis, Tam Kungam kalpot.
23 Katika kuishi kwangu alivunja nguvu zangu, akafupisha siku zangu.
Bet Viņš ir pazemojis ceļā manu spēku un paīsinājis manas dienas.
24 Ndipo niliposema: “Ee Mungu wangu, usinichukue katikati ya siku zangu; miaka yako inaendelea vizazi vyote.
Es saku: mans Dievs, neņem mani nost pusmūžā. Tavi gadi paliek līdz radu radiem.
25 Hapo mwanzo uliweka misingi ya dunia, nazo mbingu ni kazi ya mikono yako.
Senlaikus Tu esi nodibinājis zemi, un debesis ir Tavu roku darbs.
26 Hizi zitatoweka, lakini wewe utadumu, zote zitachakaa kama vazi. Utazibadilisha kama nguo nazo zitaondoshwa.
Tās zudīs, bet Tu pastāvēsi; tās sadils visas, kā drēbes; Tu tās pārvērtīsi kā drānas, un tās pārvērtīsies;
27 Lakini wewe, U yeye yule, nayo miaka yako haikomi kamwe.
Bet Tu palieci tas pats, un Tavi gadi nebeigsies.
28 Watoto wa watumishi wako wataishi mbele zako; wazao wao wataimarishwa mbele zako.”
Tavu kalpu bērni paliks, un viņu dzimums būs pastāvīgs Tavā priekšā.

< Zaburi 102 >