< Zaburi 100 >

1 Zaburi ya shukrani. Mpigieni Bwana kelele za shangwe, dunia yote.
Psaume de louange. Vous, toute la terre, jetez des cris de réjouissance à l'Éternel!
2 Mwabuduni Bwana kwa furaha; njooni mbele zake kwa nyimbo za shangwe.
Servez l'Éternel avec joie; venez devant sa face avec des cris d'allégresse.
3 Jueni kwamba Bwana ndiye Mungu. Yeye ndiye alituumba, sisi tu mali yake; sisi tu watu wake, kondoo wa malisho yake.
Sachez que l'Éternel est Dieu. C'est lui qui nous a faits, et non pas nous; nous sommes son peuple et le troupeau qu'il fait paître.
4 Ingieni malangoni mwake kwa shukrani na katika nyua zake kwa kusifu, mshukuruni yeye na kulisifu jina lake.
Entrez dans ses portes avec des actions de grâces, dans ses parvis avec la louange; célébrez-le, bénissez son nom
5 Kwa maana Bwana ni mwema na upendo wake wadumu milele; uaminifu wake unadumu kwa vizazi vyote.
Car l'Éternel est bon; sa bonté demeure à toujours, et sa fidélité d'âge en âge.

< Zaburi 100 >