< Zaburi 1 >

1 Heri mtu yule ambaye haendi katika shauri la watu waovu, wala hasimami katika njia ya wenye dhambi, au kuketi katika baraza la wenye mizaha.
Blessed is the man who does not walk in the advice of the wicked, or stand in the pathway with sinners, or sit in the assembly of mockers.
2 Bali huifurahia sheria ya Bwana, naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.
But his delight is in the law of Yahweh, and on his law he meditates day and night.
3 Mtu huyo ni kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji, ambao huzaa matunda kwa majira yake na majani yake hayanyauki. Lolote afanyalo hufanikiwa.
He will be like a tree planted by the streams of water that produces its fruit in its season, whose leaves do not wither; whatever he does will prosper.
4 Sivyo walivyo waovu! Wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
The wicked are not so, but are instead like the chaff that the wind drives away.
5 Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
So the wicked will not stand in the judgment, nor sinners in the assembly of the righteous.
6 Kwa maana Bwana huziangalia njia za mwenye haki, bali njia ya waovu itaangamia.
For Yahweh approves of the way of the righteous, but the way of the wicked will perish.

< Zaburi 1 >