< Mithali 7 >

1 Mwanangu, shika maneno yangu na kuzihifadhi amri zangu ndani yako.
Fili mi, custodi sermones meos, et præcepta mea reconde tibi. Fili,
2 Shika amri zangu nawe utaishi; linda mafundisho yangu kama mboni ya jicho lako.
serva mandata mea, et vives; et legem meam quasi pupillam oculi tui:
3 Yafunge katika vidole vyako; yaandike katika kibao cha moyo wako.
liga eam in digitis tuis, scribe illam in tabulis cordis tui.
4 Mwambie hekima, “Wewe ni dada yangu,” uite ufahamu jamaa yako;
Dic sapientiæ: Soror mea es, et prudentiam voca amicam tuam:
5 watakuepusha na mwanamke mzinzi, kutokana na mwanamke mpotovu na maneno yake ya kubembeleza.
ut custodiant te a muliere extranea, et ab aliena quæ verba sua dulcia facit.
6 Kwenye dirisha la nyumba yangu nilitazama nje kupitia upenyo kwenye mwimo wa dirisha.
De fenestra enim domus meæ per cancellos prospexi,
7 Niliona miongoni mwa wajinga, nikagundua miongoni mwa wanaume vijana, kijana asiye na akili.
et video parvulos; considero vecordem juvenem,
8 Alikuwa akishuka njiani karibu na pembe ya kwake, akielekea kwenye nyumba ya huyo mwanamke
qui transit per plateam juxta angulum et prope viam domus illius graditur:
9 wakati wa machweo, jua likipungua nuru yake, giza la usiku lilipokuwa likiingia.
in obscuro, advesperascente die, in noctis tenebris et caligine.
10 Ndipo huyo mwanamke akatoka kumlaki, hali amevaa kama kahaba akiwa na nia ya udanganyifu.
Et ecce occurrit illi mulier ornatu meretricio, præparata ad capiendas animas: garrula et vaga,
11 (Ni mwanamke mwenye makelele na mkaidi, miguu yake haitulii nyumbani;
quietis impatiens, nec valens in domo consistere pedibus suis;
12 mara kwenye barabara za mji, mara kwenye viwanja vikubwa, kwenye kila pembe huvizia.)
nunc foris, nunc in plateis, nunc juxta angulos insidians.
13 Huyo mwanamke alimkumbatia kijana na kumbusu, na kwa uso usio na haya akamwambia:
Apprehensumque deosculatur juvenem, et procaci vultu blanditur, dicens:
14 “Nina sadaka za amani nyumbani; leo nimetimiza nadhiri zangu.
Victimas pro salute vovi; hodie reddidi vota mea:
15 Kwa hiyo nimetoka nje kukulaki; nimekutafuta na nimekupata!
idcirco egressa sum in occursum tuum, desiderans te videre, et reperi.
16 Nimetandika kitanda changu kwa kitani za rangi kutoka Misri.
Intexui funibus lectulum meum; stravi tapetibus pictis ex Ægypto:
17 Nimetia manukato kitanda changu kwa manemane, udi na mdalasini.
aspersi cubile meum myrrha, et aloë, et cinnamomo.
18 Njoo, tuzame katika mapenzi mpaka asubuhi; tujifurahishe wenyewe kwa mapenzi!
Veni, inebriemur uberibus, et fruamur cupitis amplexibus donec illucescat dies.
19 Mume wangu hayupo nyumbani; amekwenda safari ya mbali.
Non est enim vir in domo sua: abiit via longissima:
20 Amechukua mkoba uliojazwa fedha na hatakuwepo nyumbani karibuni.”
sacculum pecuniæ secum tulit; in die plenæ lunæ reversurus est in domum suam.
21 Kwa maneno laini yule mwanamke akampotosha; alimshawishi kwa maneno yake laini.
Irretivit eum multis sermonibus, et blanditiis labiorum protraxit illum.
22 Mara huyo kijana alimfuata yule mwanamke kama fahali aendaye machinjoni, kama kulungu aingiaye kwenye kitanzi,
Statim eam sequitur quasi bos ductus ad victimam, et quasi agnus lasciviens, et ignorans quod ad vincula stultus trahatur:
23 mpaka mshale umchome ini lake, kama ndege anayenaswa kwenye mtego, bila kujua itamgharimu maisha yake.
donec transfigat sagitta jecur ejus, velut si avis festinet ad laqueum, et nescit quod de periculo animæ illius agitur.
24 Sasa basi wanangu, nisikilizeni; sikilizeni kwa makini nisemalo.
Nunc ergo, fili mi, audi me, et attende verbis oris mei.
25 Usiruhusu moyo wako ugeukie njia za huyo mwanamke, wala usitangetange katika mapito yake.
Ne abstrahatur in viis illius mens tua, neque decipiaris semitis ejus;
26 Aliowaangusha ni wengi; aliowachinja ni kundi kubwa.
multos enim vulneratos dejecit, et fortissimi quique interfecti sunt ab ea.
27 Nyumba yake ni njia kuu iendayo kaburini, ielekeayo chini kwenye vyumba vya mauti. (Sheol h7585)
Viæ inferi domus ejus, penetrantes in interiora mortis. (Sheol h7585)

< Mithali 7 >