< Mithali 31 >

1 Misemo ya Mfalme Lemueli, usia wa mama yake aliyomfundisha:
کلام لموئیل پادشاه، پیغامی که مادرش به او تعلیم داد.۱
2 “Ee mwanangu, ee mwana wa tumbo langu, ee mwana wa nadhiri zangu,
چه گویم‌ای پسر من، چه گویم‌ای پسر رحم من! و چه گویم‌ای پسر نذرهای من!۲
3 Usitumie nguvu zako kwa wanawake, uhodari wako kwa wale wanaowaharibu wafalme.
قوت خود را به زنان مده، و نه طریقهای خویش را به آنچه باعث هلاکت پادشاهان است.۳
4 “Ee Lemueli, haifai wafalme, haifai wafalme kunywa mvinyo, haifai watawala kutamani sana kileo,
پادشاهان را نمی شاید‌ای لموئیل، پادشاهان را نمی شاید که شراب بنوشند، و نه امیران را که مسکرات را بخواهند.۴
5 wasije wakanywa na kusahau vile sheria inavyoamuru na kuwanyima haki zao wote walioonewa.
مبادا بنوشند و فرایض را فراموش کنند، وداوری جمیع ذلیلان را منحرف سازند.۵
6 Wape kileo wale wanaoangamia, mvinyo wale walio na uchungu,
مسکرات را به آنانی که مشرف به هلاکتندبده. و شراب را به تلخ جانان،۶
7 Wanywe na kusahau umaskini wao na wasikumbuke taabu yao tena.
تا بنوشند و فقر خود را فراموش کنند، ومشقت خویش را دیگر بیاد نیاورند.۷
8 “Sema kwa ajili ya wale wasioweza kujisemea, kwa ajili ya haki za wote walioachwa ukiwa.
دهان خود را برای گنگان باز کن، و برای دادرسی جمیع بیچارگان.۸
9 Sema na uamue kwa haki, tetea haki za maskini na wahitaji.”
دهان خود را باز کرده، به انصاف داوری نما، و فقیر و مسکین را دادرسی فرما.۹
10 Mke mwenye sifa nzuri, ni nani awezaye kumpata? Yeye ni wa thamani sana kuliko marijani.
زن صالحه را کیست که پیدا تواند کرد؟ قیمت او از لعلها گرانتر است.۱۰
11 Mume wake anamwamini kikamilifu wala hakosi kitu chochote cha thamani.
دل شوهرش بر او اعتماد دارد، و محتاج منفعت نخواهد بود.۱۱
12 Humtendea mumewe mema, wala si mabaya, siku zote za maisha yake.
برایش تمامی روزهای عمر خود، خوبی خواهد کرد و نه بدی.۱۲
13 Huchagua sufu na kitani naye hufanya kazi kwa mikono yenye bidii.
پشم و کتان را می‌جوید. و به‌دستهای خودبا رغبت کار می‌کند.۱۳
14 Yeye ni kama meli za biashara akileta chakula chake kutoka mbali.
او مثل کشتیهای تجار است، که خوراک خود را از دور می‌آورد.۱۴
15 Yeye huamka kungali bado giza huwapa jamaa yake chakula na mafungu kwa watumishi wake wa kike.
وقتی که هنوز شب است برمی خیزد، و به اهل خانه‌اش خوراک و به کنیزانش حصه ایشان را می دهد.۱۵
16 Huangalia shamba na kulinunua, kutokana na mapato yake hupanda shamba la mizabibu.
درباره مزرعه فکر کرده، آن را می‌خرد، و ازکسب دستهای خود تاکستان غرس می‌نماید.۱۶
17 Hufanya kazi zake kwa nguvu, mikono yake ina nguvu kwa ajili ya kazi zake.
کمر خود را با قوت می‌بندد، و بازوهای خویش را قوی می‌سازد.۱۷
18 Huona kwamba biashara yake ina faida, wala taa yake haizimiki usiku.
تجارت خود را می‌بیند که نیکو است، وچراغش در شب خاموش نمی شود.۱۸
19 Huweka mikono yake kwenye pia, navyo vidole vyake hushikilia kijiti chenye uzi.
دستهای خود را به دوک دراز می‌کند، وانگشتهایش چرخ را می‌گیرد.۱۹
20 Huwanyooshea maskini mikono yake na kuwakunjulia wahitaji vitanga vyake.
کفهای خود را برای فقیران مبسوطمی سازد، و دستهای خویش را برای مسکینان دراز می‌نماید.۲۰
21 Theluji ishukapo, hana hofu kwa ajili ya watu wa nyumbani mwake, kwa maana wote wamevikwa nguo za kutia joto.
به جهت اهل خانه‌اش از برف نمی ترسد، زیرا که جمیع اهل خانه او به اطلس ملبس هستند.۲۱
22 Hutengeneza mazulia ya urembo ya kufunika kitanda chake, yeye huvaa kitani safi na urujuani.
برای خود اسبابهای زینت می‌سازد. لباسش از کتان نازک و ارغوان می‌باشد.۲۲
23 Mume wake anaheshimiwa kwenye lango la mji, aketipo miongoni mwa wazee wa nchi.
شوهرش در دربارها معروف می‌باشد، و در میان مشایخ ولایت می‌نشیند.۲۳
24 Hutengeneza mavazi ya kitani na kuyauza, naye huwauzia wafanyabiashara mishipi.
جامه های کتان ساخته آنها را می‌فروشد، وکمربندها به تاجران می‌دهد.۲۴
25 Amevikwa nguvu na heshima, anaweza kucheka bila kuwa na hofu kwa siku zijazo.
قوت و عزت، لباس او است، و درباره وقت آینده می‌خندد.۲۵
26 Huzungumza kwa hekima na mafundisho ya kuaminika yapo ulimini mwake.
دهان خود را به حکمت می‌گشاید، و تعلیم محبت‌آمیز بر زبان وی است.۲۶
27 Huangalia mambo ya nyumbani mwake wala hali chakula cha uvivu.
به رفتار اهل خانه خود متوجه می‌شود، وخوراک کاهلی نمی خورد.۲۷
28 Watoto wake huamka na kumwita aliyebarikiwa, mumewe pia humsifu, akisema:
پسرانش برخاسته، او را خوشحال می‌گویند، و شوهرش نیز او را می‌ستاید.۲۸
29 “Wanawake wengi hufanya vitu vyenye sifa nzuri, lakini wewe umewapita wote.”
دختران بسیار اعمال صالحه نمودند، اما توبر جمیع ایشان برتری داری.۲۹
30 Kujipamba ili kuvutia ni udanganyifu na uzuri unapita upesi, bali mwanamke anayemcha Bwana atasifiwa.
جمال، فریبنده و زیبایی، باطل است، اما زنی که از خداوند می‌ترسد ممدوح خواهدشد.۳۰
31 Mpe thawabu anayostahili, nazo kazi zake na zimletee sifa kwenye lango la mji.
وی را از ثمره دستهایش بدهید و اعمالش او را نزد دروازه‌ها بستاید.۳۱

< Mithali 31 >