< Mithali 30 >

1 Misemo ya Aguri mwana wa Yake, usia: Huyu mtu alimwambia Ithieli, naam, kwa Ithieli na kwa Ukali:
이 말씀은 야게의 아들 아굴의 잠언이니 그가 이디엘과 우갈에게 이른 것이니라
2 “Mimi ni mjinga kuliko wanadamu wote; sina ufahamu wa kibinadamu.
나는 다른 사람에게 비하면 짐승이라 내게는 사람의 총명이 있지아니하니라
3 Sijajifunza hekima, wala sina maarifa ya kumjua yeye Aliye Mtakatifu.
나는 지혜를 배우지 못하였고 또 거룩하신 자를 아는 지식이 없거니와
4 Ni nani ameshapanda mbinguni na kushuka? Ni nani ameshakusanya upepo kwenye vitanga vya mikono yake? Ni nani ameshafungia maji kwenye nguo yake? Ni nani ameimarisha miisho yote ya dunia? Jina lake ni nani, na mwanawe anaitwa nani? Niambie kama unajua!
하늘에 올라갔다가 내려온 자가 누구인지, 바람을 그 장중에 모은 자가 누구인지, 물을 옷에 싼자가 누구인지, 땅의 모든 끝을 정한 자가 누구인지, 그 이름이 무엇인지, 그 아들의 이름이 무엇인지 너는 아느냐?
5 “Kila neno la Mungu ni kamilifu; yeye ni ngao kwa wale wanaomkimbilia.
하나님의 말씀은 다 순전하며 하나님은 그를 의지하는 자의 방패시니라
6 Usiongeze kwenye maneno yake, ama atakukemea na kukuthibitisha kuwa mwongo.
너는 그 말씀에 더하지 말라 그가 너를 책망하시겠고 너는 거짓말 하는 자가 될까 두려우니라
7 “Ninakuomba vitu viwili, Ee Bwana; usininyime kabla sijafa:
내가 두 가지 일을 주께 구하였사오니 나의 죽기 전에 주시옵소서
8 Uutenge mbali nami udanganyifu na uongo; usinipe umaskini wala utajiri, bali unipe chakula cha kunitosha kila siku.
곧 허탄과 거짓말을 내게서 멀리 하옵시며 나로 가난하게도 마옵시고 부하게도 마옵시고 오직 필요한 양식으로 내게 먹이시옵소서
9 Nisije nikawa na vingi vya kuzidi nikakukana na kusema, ‘Bwana ni nani?’ Au nisije nikawa maskini nikaiba, nami nikaliaibisha jina la Mungu wangu.
혹 내가 배불러서 하나님을 모른다 여호와가 누구냐 할까 하오며 혹 내가 가난하여 도적질하고 내 하나님의 이름을 욕되게 할까 두려워함이니이다
10 “Usimchongee mtumishi kwa bwana wake, asije akakulaani, ukapatilizwa kwalo.
너는 종을 그 상전에게 훼방하지 말라 그가 너를 저주하겠고 너는 죄책을 당할까 두려우니라
11 “Wako watu wale ambao huwalaani baba zao na wala hawawabariki mama zao;
아비를 저주하며 어미를 축복하지 아니하는 무리가 있느니라
12 wale ambao ni safi machoni pao wenyewe kumbe hawakuoshwa uchafu wao;
스스로 깨끗한 자로 여기면서 오히려 그 더러운 것을 씻지 아니하는 무리가 있느니라
13 wale ambao daima macho yao ni ya kiburi, ambao kutazama kwao ni kwa dharau;
눈이 심히 높으며 그 눈꺼풀이 높이 들린 무리가 있느니라
14 wale ambao meno yao ni panga na ambao mataya yao yamewekwa visu kuwaangamiza maskini katika nchi, na wahitaji kutoka miongoni mwa wanadamu.
앞니는 장검 같고 어금니는 군도 같아서 가난한 자를 땅에서 삼키며 궁핍한 자를 사람 중에서 삼키는 무리가 있느니라
15 “Mruba anao binti wawili waliao, ‘Nipe! Nipe!’ “Kuna vitu vitatu visivyotosheka kamwe, naam, viko vinne visivyosema, ‘Yatosha!’:
거머리에게는 두 딸이 있어 다고, 다고 하느니라 족한 줄을 알지 못하여 족하다 하지 아니하는 것 서넛이 있나니
16 Ni kaburi, tumbo lisilozaa, nchi isiyoshiba maji kamwe, na moto, usiosema kamwe, ‘Yatosha!’ (Sheol h7585)
곧 음부와 아이 배지 못하는 태와 물로 채울 수 없는 땅과 족하다 하지 아니하는 불이니라 (Sheol h7585)
17 “Jicho lile limdhihakilo baba, lile linalodharau kumtii mama, litangʼolewa na kunguru wa bondeni, litaliwa na tai.
아비를 조롱하며 어미 순종하기를 싫어하는 자의 눈은 골짜기의 까마귀에게 쪼이고 독수리 새끼에게 먹히리라
18 “Kuna vitu vitatu vinavyonishangaza sana, naam, vinne nisivyovielewa:
내가 심히 기이히 여기고도 깨닫지 못하는 것 서넛이 있나니
19 Ni mwendo wa tai katika anga, mwendo wa nyoka juu ya mwamba, mwendo wa meli katika maji makuu ya bahari, nao mwendo wa mtu pamoja na msichana.
곧 공중에 날아 다니는 독수리의 자취와 바다로 지나다니는 배의 자취와 남자가 여자와 함께 한 자취며
20 “Huu ndio mwendo wa mwanamke mzinzi, hula akapangusa kinywa chake na kusema, ‘Sikufanya chochote kibaya.’
음녀의 자취도 그러하니라 그가 먹고 그 입을 씻음 같이 말하기를 내가 악을 행치 아니하였다 하느니라
21 “Kwa mambo matatu nchi hutetemeka, naam, kwa mambo manne haiwezi kuvumilia:
세상을 진동시키며 세상으로 견딜 수 없게 하는 것 서넛이 있나니
22 Mtumwa awapo mfalme, mpumbavu ashibapo chakula,
곧 종이 임금된 것과 미련한 자가 배부른 것과
23 mwanamke asiyependwa aolewapo, naye mtumishi wa kike achukuapo nafasi ya bibi yake.
꺼림을 받는 계집이 시집간 것과 계집 종이 주모를 이은 것이니라
24 “Vitu vinne duniani vilivyo vidogo, lakini vina akili nyingi sana:
땅에 작고도 가장 지혜로운 것 넷이 있나니
25 Mchwa ni viumbe wenye nguvu ndogo, hata hivyo hujiwekea akiba ya chakula chao wakati wa kiangazi.
곧 힘이 없는 종류로되 먹을 것을 여름에 예비하는 개미와
26 Pelele ni viumbe vyenye uwezo mdogo hata hivyo hujitengenezea nyumba zao kwenye miamba.
약한 종류로되 집을 바위 사이에 짓는 사반과
27 Nzige hawana mfalme, hata hivyo huenda pamoja vikosi vikosi.
임군이 없으되 다 떼를 지어 나아가는 메뚜기와
28 Mjusi anaweza kushikwa kwa mkono, hata hivyo huonekana katika majumba ya kifalme.
손에 잡힐만하여도 왕궁에 있는 도마뱀이니라
29 “Viko vitu vitatu ambavyo vinapendeza katika mwendo wao, naam, vinne ambavyo hutembea kwa mwendo wa madaha:
잘 걸으며 위풍 있게 다니는 것 서넛이 있나니
30 simba, mwenye nguvu miongoni mwa wanyama, asiyerudi nyuma kwa chochote;
곧 짐승 중에 가장 강하여 아무 짐승 앞에서도 물러가지 아니하는 사자와
31 jogoo atembeaye kwa maringo, pia beberu, naye mfalme pamoja na jeshi lake lililomzunguka.
사냥개와 수염소와 및 당할 수 없는 왕이니라
32 “Ikiwa umefanya upumbavu na ukajitukuza mwenyewe, au kama umepanga mabaya, basi funika mdomo wako na mkono wako.
사냥개와 수염소와 및 당할 수 없는 왕이니라
33 Kwa maana kama vile kusukasuka maziwa hutoa siagi, na pia kule kufinya pua hutoa damu, kadhalika kuchochea hasira hutokeza ugomvi.”
대저 젖을 저으면 뻐터가 되고 코를 비틀면 피가 나는 것 같이 노를 격동하면 다툼이 남이니라

< Mithali 30 >