< Mithali 29 >

1 Mtu anayeendelea kuwa na shingo ngumu baada ya maonyo mengi, ataangamia ghafula, wala hapati dawa.
L'homme qui étant repris roidit son cou, sera subitement brisé, sans qu'il y ait de guérison.
2 Wenye haki wanapostawi, watu hufurahi; waovu watawalapo, watu hulia kwa huzuni.
Quand les justes sont avancés, le peuple se réjouit; mais quand le méchant domine, le peuple gémit.
3 Mtu apendaye hekima huleta furaha kwa baba yake, bali aambatanaye na makahaba hutapanya mali yake.
L'homme qui aime la sagesse, réjouit son père; mais celui qui entretient les femmes débauchées, dissipe ses richesses.
4 Kwa haki mfalme huipa nchi uthabiti, bali mfalme aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza.
Le Roi maintient le pays par le jugement; mais l'homme qui est adonné aux présents, le ruinera.
5 Yeyote amsifuye jirani yake isivyostahili, anautandaza wavu kuitega miguu yake.
L'homme qui flatte son prochain, étend le filet devant ses pas.
6 Mtu mbaya hutegwa na dhambi yake mwenyewe bali mwenye haki huweza kuimba na kufurahi.
Le mal qui est au forfait de l'homme, lui est comme un piège; mais le juste chantera, et se réjouira.
7 Mwenye haki hujali haki kwa ajili ya maskini, bali mwovu hajishughulishi na hilo.
Le juste prend connaissance de la cause des pauvres; [mais] le méchant n'en prend point connaissance.
8 Wenye mzaha huuchochea mji, bali watu wenye hekima hugeuzia mbali hasira.
Les hommes moqueurs troublent la ville; mais les sages apaisent la colère.
9 Kama mwenye hekima akienda mahakamani na mpumbavu, mpumbavu hukasirika na kudhihaki, wala hakuna amani.
L'homme sage contestant avec l'homme fou, soit qu'il s'émeuve, soit qu'il rie, n'aura point de repos.
10 Watu wamwagao damu humchukia mtu mwadilifu na hutafuta kumuua mtu mnyofu.
Les hommes sanguinaires ont en haine l'homme intègre, mais les hommes droits tiennent chère sa vie.
11 Mpumbavu huonyesha hasira yake yote, bali mwenye hekima hujizuia.
Le fou pousse au-dehors toute sa passion, mais le sage la réprime, et [la renvoie] en arrière.
12 Kama mtawala akisikiliza uongo, maafisa wake wote huwa waovu.
Tous les serviteurs d'un Prince qui prête l'oreille à la parole de mensonge, sont méchants.
13 Mtu maskini na mtu anayeonea wanafanana kwa jambo hili: Bwana hutia nuru macho yao wote wawili.
Le pauvre et l'homme usurier s'entre-rencontrent, et l'Eternel illumine les yeux de tous deux.
14 Kama mfalme akiwaamua maskini kwa haki, kiti chake cha enzi kitakuwa thabiti siku zote.
Le trône du Roi qui fait justice selon la vérité aux pauvres, sera établi à perpétuité.
15 Fimbo ya maonyo hutia hekima, bali mtoto aliyeachiwa bila maonyo humwaibisha mama yake.
La verge et la répréhension donnent la sagesse; mais l'enfant abandonné à lui-même fait honte à sa mère.
16 Wakati waovu wanapostawi, pia dhambi vivyo hivyo, lakini wenye haki wataliona anguko lao.
Quand les méchants sont avancés, les forfaits se multiplient; mais les justes verront leur ruine.
17 Mrudi mwanao, naye atakupa amani, atakufurahisha nafsi yako.
Corrige ton enfant, et il te mettra en repos, et il donnera du plaisir à ton âme.
18 Mahali pasipo na ufunuo, watu kujizuia, bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
Lorsqu'il n'y a point de vision, le peuple est abandonné; mais bienheureux est celui qui garde la Loi.
19 Mtumishi hawezi kuonywa kwa maneno matupu, ajapoelewa, hataitikia.
Le serviteur ne se corrige point par des paroles; car il entendra, et ne répondra point.
20 Je, unamwona mtu azungumzaye kwa haraka? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko yeye.
As-tu vu un homme précipité en ses paroles? il y a plus d'espérance d'un fou que de lui.
21 Kama mtu akimdekeza mtumishi wake tangu ujanani, atamletea sikitiko mwishoni.
Le serviteur sera enfin fils de celui qui l'élève délicatement dès sa jeunesse.
22 Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi, naye mtu mwenye hasira ya haraka hutenda dhambi nyingi.
L'homme colère excite les querelles, et l'homme furieux [commet] plusieurs forfaits.
23 Kiburi cha mtu humshusha, bali mtu mwenye roho ya unyenyekevu hupata heshima.
L'orgueil de l'homme l'abaisse, mais celui qui est humble d'esprit obtient la gloire.
24 Anayekubaliana na mwizi ni adui wa nafsi yake mwenyewe; huapishwa lakini hathubutu kushuhudia.
Celui qui partage avec le larron, hait son âme; il entend le serment d'exécration, et il ne le décèle point.
25 Kuwaogopa watu huwa ni mtego, bali yeyote amtumainiaye Bwana atakuwa salama.
L'effroi que conçoit un homme, lui tend un piège; mais celui qui s'assure en l'Eternel aura une haute retraite.
26 Wengi hutafuta kusikilizwa na mtawala, bali mtu hupata haki kutoka kwa Bwana.
Plusieurs recherchent la face de celui qui domine; mais c'est de l'Eternel que vient le jugement qu'on donne touchant quelqu'un.
27 Mwenye haki huwachukia sana wasio waaminifu; waovu huwachukia sana wenye haki.
L'homme inique est en abomination aux justes; et celui qui va droit, est en abomination au méchant.

< Mithali 29 >