< Mithali 26 >

1 Kama theluji wakati wa kiangazi au mvua wakati wa mavuno, ndivyo asivyostahili heshima mpumbavu.
Come la neve non conviene all’estate, né la pioggia al tempo della mèsse, così non conviene la gloria allo stolto.
2 Kama shomoro apigapigavyo mabawa yake au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi, ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu.
Come il passero vaga qua e là e la rondine vola, così la maledizione senza motivo, non raggiunge l’effetto.
3 Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda, nayo fimbo kwa migongo ya wapumbavu!
La frusta per il cavallo, la briglia per l’asino, e il bastone per il dosso degli stolti.
4 Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama wewe mwenyewe utakuwa kama yeye.
Non rispondere allo stolto secondo la sua follia, che tu non gli abbia a somigliare.
5 Mjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama atakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe.
Rispondi allo stolto secondo la sua follia, perché non abbia a credersi savio.
6 Kama vile ilivyo kujikata miguu au kunywa hasara, ndivyo ilivyo kutuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu.
Chi affida messaggi a uno stolto si taglia i piedi e s’abbevera di pene.
7 Kama miguu ya kiwete inavyoningʼinia ndivyo ilivyo mithali katika kinywa cha mpumbavu.
Come le gambe dello zoppo son senza forza, così è una massima in bocca degli stolti.
8 Kama kufunga jiwe kwenye kombeo, ndivyo ilivyo kumpa mpumbavu heshima.
Chi onora uno stolto fa come chi getta una gemma in un mucchio di sassi.
9 Kama mwiba kwenye mkono wa mlevi ndivyo ilivyo mithali kinywani mwa mpumbavu.
Una massima in bocca agli stolti è come un ramo spinoso in mano a un ubriaco.
10 Kama mpiga upinde ambaye hujeruhi ovyo, ndivyo alivyo yeye aajiriye mpumbavu au yeyote apitaye njiani.
Chi impiega lo stolto e il primo che capita, è come un arciere che ferisce tutti.
11 Kama mbwa ayarudiavyo matapiko yake, ndivyo mpumbavu arudiavyo upumbavu wake.
Lo stolto che ricade nella sua follia, è come il cane che torna al suo vomito.
12 Je, unamwona mtu ajionaye mwenye hekima machoni pake mwenyewe? Liko tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
Hai tu visto un uomo che si crede savio? C’è più da sperare da uno stolto che da lui.
13 Mvivu husema, “Yuko simba barabarani, simba mkali anazunguka mitaa!”
Il pigro dice: “C’è un leone nella strada, c’è un leone per le vie!”
14 Kama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake, ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake.
Come la porta si volge sui cardini così il pigro sul suo letto.
15 Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, naye huchoka kuupeleka kwenye kinywa chake.
Il pigro tuffa la mano nel piatto; gli par fatica riportarla alla bocca.
16 Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe, kuliko watu saba wawezao kujibu kwa busara.
Il pigro si crede più savio di sette uomini che dànno risposte sensate.
17 Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio, ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu.
Il passante che si riscalda per una contesa che non lo concerne, è come chi afferra un cane per le orecchie.
18 Kama mtu mwendawazimu atupaye vijinga vya moto au mishale ya kufisha,
Come un pazzo che avventa tizzoni, frecce e morte,
19 ndivyo alivyo mtu amdanganyaye jirani yake na kusema, “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”
così è colui che inganna il prossimo, e dice: “Ho fatto per ridere!”
20 Bila kuni moto huzimika; pasipo uchongezi ugomvi humalizika.
Quando mancan le legna, il fuoco si spegne; e quando non c’è maldicente, cessan le contese.
21 Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.
Come il carbone da la brace, e le legna dànno la fiamma, così l’uomo rissoso accende le liti.
22 Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
Le parole del maldicente son come ghiottonerie, e penetrano fino nell’intimo delle viscere.
23 Kama rangi ingʼaayo iliyopakwa kwenye vyombo vya udongo ndivyo ilivyo midomo laini pamoja na moyo mbaya.
Labbra ardenti e un cuor malvagio son come schiuma d’argento spalmata sopra un vaso di terra.
24 Mtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake, lakini moyoni mwake huficha udanganyifu.
Chi odia, parla con dissimulazione; ma, dentro, cova la frode.
25 Ingawa maneno yake huvutia, usimwamini, kwa maana machukizo saba hujaza moyo wake.
Quando parla con voce graziosa, non te ne fidare, perché ha sette abominazioni in cuore.
26 Nia yake ya kudhuru wengine inaweza kufichwa na udanganyifu, lakini uovu wake utafichuliwa kwenye kusanyiko.
L’odio suo si nasconde sotto la finzione, ma la sua malvagità si rivelerà nell’assemblea.
27 Kama mtu akichimba shimo, atatumbukia ndani yake, kama mtu akivingirisha jiwe, litamrudia.
Chi scava una fossa vi cadrà, e la pietra torna addosso a chi la rotola.
28 Ulimi wa uongo, huwachukia wale unaowaumiza, nacho kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.
La lingua bugiarda odia quelli che ha ferito, e la bocca lusinghiera produce rovina.

< Mithali 26 >