< Mithali 21 >

1 Moyo wa mfalme uko katika mkono wa Bwana; huuongoza kama mkondo wa maji, popote apendapo.
Sicut divisiones aquarum, ita cor regis in manu Domini: quocumque voluerit, inclinabit illud.
2 Njia zote za mwanadamu huonekana sawa kwake, bali Bwana huupima moyo.
Omnis via viri recta sibi videtur: appendit autem corda Dominus.
3 Kufanya yaliyo sawa na haki inakubalika zaidi kwa Bwana kuliko dhabihu.
Facere misericordiam et iudicium, magis placet Domino quam victimæ.
4 Macho ya kudharau na moyo wa kiburi, ambavyo ni taa ya waovu, vyote ni dhambi!
Exaltatio oculorum est dilatatio cordis: lucerna impiorum peccatum.
5 Mipango ya mwenye bidii huelekeza kwenye faida, kama vile kwa hakika pupa huelekeza kwenye umaskini.
Cogitationes robusti semper in abundantia: omnis autem piger semper in egestate est.
6 Mali iliyopatikana kwa ulimi wa uongo ni mvuke upitao upesi na mtego wa kufisha.
Qui congregat thesauros lingua mendacii, vanus et excors est, et impingetur ad laqueos mortis.
7 Jeuri ya waovu itawaburuta mbali, kwa kuwa wanakataa kufanya yaliyo sawa.
Rapinæ impiorum detrahent eos, quia noluerunt facere iudicium.
8 Njia ya mwenye hatia ni ya upotovu, bali tabia ya mtu asiye na hatia ni nyofu.
Perversa via viri, aliena est: qui autem mundus est, rectum opus eius.
9 Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
Melius est sedere in angulo domatis, quam cum muliere litigiosa, et in domo communi.
10 Mtu mwovu hutamani sana ubaya, jirani yake hapati huruma kutoka kwake.
Anima impii desiderat malum, non miserebitur proximo suo.
11 Wakati mwenye mzaha ameadhibiwa, mjinga hupata hekima; wakati mtu mwenye hekima afundishwapo, hupata maarifa.
Mulctato pestilente sapientior erit parvulus: et si sectetur sapientem, sumet scientiam.
12 Mwenye Haki huyajua yanayotendeka katika nyumba za waovu, naye atawaangamiza waovu.
Excogitat iustus de domo impii, ut detrahat impios a malo.
13 Mtu akiziba masikio asisikie kilio cha maskini, yeye pia atalia, wala hatajibiwa.
Qui obturat aurem suam ad clamorem pauperis, et ipse clamabit, et non exaudietur.
14 Zawadi itolewayo kwa siri hutuliza hasira na rushwa iliyofichwa kwenye nguo hutuliza ghadhabu kali.
Munus absconditum extinguit iras: et donum in sinu indignationem maximam.
15 Wakati haki imetendeka, huleta furaha kwa wenye haki, bali kitisho kwa watenda mabaya.
Gaudium iusto est facere iudicium: et pavor operantibus iniquitatem.
16 Mtu anayepotea kutoka mapito ya ufahamu, hupumzika katika kundi la waliokufa.
Vir, qui erraverit a via doctrinæ, in cœtu gigantum commorabitur.
17 Mtu apendaye anasa atakuwa maskini, yeyote apendaye mvinyo na mafuta kamwe hatakuwa tajiri.
Qui diligit epulas, in egestate erit: qui amat vinum, et pinguia, non ditabitur.
18 Waovu huwa fidia kwa ajili ya wenye haki, nao wasio waaminifu kwa ajili ya wanyofu.
Pro iusto datur impius: et pro rectis iniquus.
19 Ni afadhali kuishi jangwani kuliko kuishi na mke mgomvi na mkorofi.
Melius est habitare in terra deserta, quam cum muliere rixosa et iracunda.
20 Katika nyumba ya mwenye hekima kuna akiba ya vyakula vizuri na mafuta, lakini mtu mpumbavu hutafuna vyote alivyo navyo.
Thesaurus desiderabilis, et oleum in habitaculo iusti: et imprudens homo dissipabit illud.
21 Yeye afuatiaye haki na upendo hupata uzima, mafanikio na heshima.
Qui sequitur iustitiam et misericordiam, inveniet vitam, iustitiam, et gloriam.
22 Mtu mwenye hekima huushambulia mji wa wenye nguvu, na kuangusha ngome wanazozitegemea.
Civitatem fortium ascendit sapiens, et destruxit robur fiduciæ eius.
23 Yeye alindaye kinywa chake na ulimi wake hujilinda na maafa.
Qui custodit os suum, et linguam suam, custodit ab angustiis animam suam.
24 Mtu mwenye kiburi na majivuno, “Mdhihaki” ndilo jina lake; hutenda mambo kwa kiburi kilichozidi.
Superbus et arrogans vocatur indoctus, qui in ira operatur superbiam.
25 Kutamani sana kwa mvivu kutakuwa kifo chake, kwa sababu mikono yake haitaki kufanya kazi.
Desideria occidunt pigrum: noluerunt enim quidquam manus eius operari:
26 Mchana kutwa hutamani zaidi, lakini mnyofu hutoa pasipo kuzuia.
tota die concupiscit et desiderat: qui autem iustus est, tribuet, et non cessabit.
27 Dhabihu ya mtu mwovu ni chukizo, si zaidi sana itolewapo kwa nia mbaya!
Hostiæ impiorum abominabiles, quia offeruntur ex scelere.
28 Shahidi wa uongo ataangamia, bali maneno ya mwenye kusikia yatadumu.
Testis mendax peribit: vir obediens loquetur victoriam.
29 Mtu mwovu ana uso wa ushupavu, bali mtu mnyofu huzifikiria njia zake.
Vir impius procaciter obfirmat vultum suum: qui autem rectus est, corrigit viam suam.
30 Hakuna hekima, wala akili, wala mpango unaoweza kufaulu dhidi ya Bwana.
Non est sapientia, non est prudentia, non est consilium contra Dominum.
31 Farasi huandaliwa kwa ajili ya siku ya vita, bali ushindi huwa kwa Bwana.
Equus paratur ad diem belli: Dominus autem salutem tribuit.

< Mithali 21 >