< Mithali 21 >

1 Moyo wa mfalme uko katika mkono wa Bwana; huuongoza kama mkondo wa maji, popote apendapo.
Tel est le cours de l'eau, tel est le cœur du roi dans la main de Dieu; de quelque côté qu'il veuille l'incliner, c'est là qu'Il le dirige.
2 Njia zote za mwanadamu huonekana sawa kwake, bali Bwana huupima moyo.
Tout homme semble juste à ses yeux; mais Dieu dirige les cœurs.
3 Kufanya yaliyo sawa na haki inakubalika zaidi kwa Bwana kuliko dhabihu.
Faire des choses justes et dire la vérité est plus agréable au Seigneur que le sang des victimes.
4 Macho ya kudharau na moyo wa kiburi, ambavyo ni taa ya waovu, vyote ni dhambi!
Le cœur de l'audacieux est superbe dans son insolence; la lampe des impies est le péché.
5 Mipango ya mwenye bidii huelekeza kwenye faida, kama vile kwa hakika pupa huelekeza kwenye umaskini.
6 Mali iliyopatikana kwa ulimi wa uongo ni mvuke upitao upesi na mtego wa kufisha.
Amasser des trésors avec une langue trompeuse, c'est poursuivre des vanités sur les filets de la mort.
7 Jeuri ya waovu itawaburuta mbali, kwa kuwa wanakataa kufanya yaliyo sawa.
La destruction habitera avec les impies, parce qu'ils ne veulent pas pratiquer la justice.
8 Njia ya mwenye hatia ni ya upotovu, bali tabia ya mtu asiye na hatia ni nyofu.
Devant les hommes tortueux Dieu place des voies tortueuses; car Ses œuvres sont droites et pures.
9 Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
Mieux vaut demeurer dans un carrefour en plein air, que dans une grande maison bien crépie avec l'iniquité.
10 Mtu mwovu hutamani sana ubaya, jirani yake hapati huruma kutoka kwake.
Nul homme ne sera miséricordieux pour l'âme des impies.
11 Wakati mwenye mzaha ameadhibiwa, mjinga hupata hekima; wakati mtu mwenye hekima afundishwapo, hupata maarifa.
La punition de l'intempérant rend l'innocent plus réfléchi; l'homme sage et intelligent en reçoit une leçon.
12 Mwenye Haki huyajua yanayotendeka katika nyumba za waovu, naye atawaangamiza waovu.
Le juste pénètre le cœur des impies, et les méprise à cause de leur malice.
13 Mtu akiziba masikio asisikie kilio cha maskini, yeye pia atalia, wala hatajibiwa.
Celui qui ferme l'oreille au cri du faible criera lui-même, et nul ne l'écoutera.
14 Zawadi itolewayo kwa siri hutuliza hasira na rushwa iliyofichwa kwenye nguo hutuliza ghadhabu kali.
Un don secret détourne les colères; celui qui épargne les présents excite de violents courroux.
15 Wakati haki imetendeka, huleta furaha kwa wenye haki, bali kitisho kwa watenda mabaya.
La joie du juste est de faire justice; le saint n'est pas pur aux yeux des méchants.
16 Mtu anayepotea kutoka mapito ya ufahamu, hupumzika katika kundi la waliokufa.
L'homme qui s'égare loin des voies de la justice se reposera dans l'assemblée des géants.
17 Mtu apendaye anasa atakuwa maskini, yeyote apendaye mvinyo na mafuta kamwe hatakuwa tajiri.
L'indigent aime la joie; il désire le vin et l'huile en abondance.
18 Waovu huwa fidia kwa ajili ya wenye haki, nao wasio waaminifu kwa ajili ya wanyofu.
Les déréglés sont en abomination aux justes.
19 Ni afadhali kuishi jangwani kuliko kuishi na mke mgomvi na mkorofi.
Mieux vaut habiter le désert qu'avec une femme bavarde, colère et querelleuse.
20 Katika nyumba ya mwenye hekima kuna akiba ya vyakula vizuri na mafuta, lakini mtu mpumbavu hutafuna vyote alivyo navyo.
Un trésor désirable reposera sur la bouche du sage; mais les insensés le dévorent.
21 Yeye afuatiaye haki na upendo hupata uzima, mafanikio na heshima.
Les voies de la justice et de la miséricorde conduisent à la vie et à la gloire.
22 Mtu mwenye hekima huushambulia mji wa wenye nguvu, na kuangusha ngome wanazozitegemea.
Le sage a pris d'assaut les villes fortes; il a démoli les forteresses sur lesquelles comptaient les impies.
23 Yeye alindaye kinywa chake na ulimi wake hujilinda na maafa.
Celui qui est maître de sa bouche et de sa langue garde son âme de la tribulation.
24 Mtu mwenye kiburi na majivuno, “Mdhihaki” ndilo jina lake; hutenda mambo kwa kiburi kilichozidi.
L'homme audacieux, arrogant et présomptueux peut être appelé un fléau; le vindicatif n'est pas dans la loi.
25 Kutamani sana kwa mvivu kutakuwa kifo chake, kwa sababu mikono yake haitaki kufanya kazi.
Les désirs tuent le paresseux; car ses mains ne se lèvent pas pour faire quoi que ce soit.
26 Mchana kutwa hutamani zaidi, lakini mnyofu hutoa pasipo kuzuia.
L'impie, durant tout le jour, a des désirs mauvais; le juste n'est avare ni de compassion ni de miséricorde.
27 Dhabihu ya mtu mwovu ni chukizo, si zaidi sana itolewapo kwa nia mbaya!
Les sacrifices des impies sont en abomination au Seigneur; car ils les offrent le cœur plein d'iniquité.
28 Shahidi wa uongo ataangamia, bali maneno ya mwenye kusikia yatadumu.
Le faux témoin périra; un homme docile parlera avec réserve.
29 Mtu mwovu ana uso wa ushupavu, bali mtu mnyofu huzifikiria njia zake.
L'impie compose effrontément son visage; mais l'homme droit saura bien discerner ses voies.
30 Hakuna hekima, wala akili, wala mpango unaoweza kufaulu dhidi ya Bwana.
Il n'est point de sagesse, point de courage, point de raison chez l'impie.
31 Farasi huandaliwa kwa ajili ya siku ya vita, bali ushindi huwa kwa Bwana.
Le cheval est tout prêt pour le jour du combat; mais le secours vient de Dieu.

< Mithali 21 >