< Mithali 12 >

1 Yeyote apendaye kuadibishwa hupenda maarifa, bali yeye achukiaye kuonywa ni mpumbavu.
Kto miłuje ćwiczenie, miłuje umiejętność; a kto ma w nienawiści karność, głupim jest.
2 Mtu mwema hupata kibali kutoka kwa Bwana, bali Bwana humhukumu mwenye hila.
Dobry odniesie łaskę od Pana; ale męża który złe myśli, Bóg potępi.
3 Mtu hathibitiki kutokana na uovu, bali mwenye haki hataondolewa.
Nie zmocni się człowiek z niezbożności; ale korzeń sprawiedliwych nie będzie poruszony.
4 Mke mwenye tabia nzuri ni taji ya mumewe, bali aaibishaye ni kama uozo katika mifupa ya mumewe.
Żona stateczna koroną jest męża swego; ale która go do hańby przywodzi, jest jako zgniłość w kościach jego.
5 Mipango ya mtu mwadilifu ni ya haki, bali ushauri wa mwovu ni udanganyifu.
Myśli sprawiedliwych są prawe: ale rady niepobożnych zdradliwe.
6 Maneno ya waovu huotea kumwaga damu, bali maneno ya waadilifu huwaokoa.
Słowa niepobożnych czyhają na krew; ale usta sprawiedliwych wybawiają ich.
7 Watu waovu huondolewa na kutoweka, bali nyumba ya mwenye haki husimama imara.
Niepobożni podwróceni bywają, tak, że ich niestaje; ale dom sprawiedliwych zostaje.
8 Mtu husifiwa kulingana na hekima yake, bali watu wenye akili zilizopotoka hudharauliwa.
Z rozumu swego mąż chwalony bywa; ale kto jest przewrotnego serca, wzgardzony będzie.
9 Heri mtu wa hali ya chini mwenye mtumishi, kuliko kujifanya mtu wa hali ya juu nawe huna chakula.
Lepszy jest człowiek podły, który ma sługę, niżeli chlubny, któremu nie staje chleba.
10 Mtu mwenye haki hujali mahitaji ya mnyama wake, bali matendo ya huruma ya mwovu ni ukatili.
Sprawiedliwy ma na pieczy żywot bydlątka swego; ale serce niepobożnych okrutne jest.
11 Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yeye afuataye mambo ya upuzi hana akili.
Kto sprawuje ziemię swoję, chlebem nasycony bywa; ale kto naśladuje próżnujących, głupi jest.
12 Waovu hutamani mateka ya watu wabaya, bali shina la mwenye haki hustawi.
Niepobożny pragnie obrony przeciw nieszczęściu; ale korzeń sprawiedliwych daje ją.
13 Mtu mwovu hunaswa kwa mazungumzo yake ya dhambi, bali mwenye haki huepuka taabu.
W przestępstwie warg upląta się złośnik; ale sprawiedliwy z ucisku wychodzi.
14 Kutokana na tunda la midomo yake mtu hujazwa na mambo mema, hakika kama ilivyo kazi ya mikono yake humtunza.
Z owocu ust każdy będzie nasycony dobrem, a nagrodę spraw rąk jego Bóg mu odda.
15 Njia ya mpumbavu huonekana sawa machoni pake mwenyewe, bali mtu mwenye hekima husikiliza ushauri.
Droga głupiego zda się prosta przed oczyma jego; ale kto słucha rady, mądrym jest.
16 Mpumbavu huonyesha kuudhika kwake mara moja, bali mtu wa busara hupuuza matukano.
Gniew głupiego zaraz poznany bywa; ale ostrożny pokrywa hańbę swoję.
17 Shahidi wa kweli hutoa ushuhuda wa kuaminika, bali shahidi wa uongo husema uongo.
Kto mówi prawdę, opowiada sprawiedliwość; ale świadek kłamliwy mówi zdradę.
18 Maneno ya kipumbavu huchoma kama upanga, bali ulimi wa mwenye hekima huleta uponyaji.
Znajdzie takowego, co mówi słowa jako miecz przerażające; ale język mądrych jest lekarstwem.
19 Midomo isemayo kweli hudumu milele, bali ulimi wa uongo hudumu kwa muda mfupi tu.
Wargi prawdomówne utwierdzone będą na wieki; ale króciuchno trwa język kłamliwy.
20 Upo udanganyifu katika mioyo ya wale ambao hupanga mabaya, bali kuna furaha kwa wale wanaoleta amani.
Zdrada jest w sercu tych, którzy złe myślą; ale którzy radzą do pokoju, mają wesele.
21 Hakuna dhara linalompata mwenye haki, bali waovu wana taabu nyingi.
Nie spotka sprawiedliwego żadne nieszczęście; ale niezbożnicy pełni będą złego.
22 Bwana anachukia sana midomo idanganyayo, bali hufurahia watu ambao ni wa kweli.
Obrzydliwością są Panu wargi kłamliwe; ale czyniący prawdę podobają mu się.
23 Mtu mwenye busara hujihifadhia maarifa yeye mwenyewe, bali moyo wa wapumbavu hububujika upumbavu.
Człowiek ostrożny tai umiejętność; ale serce głupich wywołuje głupstwo.
24 Mikono yenye bidii itatawala, bali uvivu huishia katika kazi za utumwa.
Ręka pracowitych będzie panowała; ale zdradliwa będzie dań dawała.
25 Moyo wa wasiwasi humlemea mtu, bali neno la huruma humfurahisha.
Frasunek w sercu człowieczem poniża je; ale powieść dobra uwesela je.
26 Mtu mwenye haki ni mwangalifu katika urafiki, bali njia ya waovu huwapotosha.
Zacniejszy jest nad bliźniego swego sprawiedliwy; ale droga niezbożnych zawodzi ich.
27 Mtu mvivu haoki mawindo yake, bali mtu mwenye bidii ana mali za thamani.
Nie upiecze chytry obłowu swojego; ale człowiek pilny majętności kosztownych nabędzie.
28 Katika njia ya haki kuna uzima; katika mapito hayo kuna maisha ya milele.
Na ścieszce sprawiedliwości żywot, a na drodze ścieszki jej niemasz śmierci.

< Mithali 12 >