< Mithali 11 >

1 Bwana huchukia sana mizani za udanganyifu, bali vipimo sahihi ni furaha yake.
La fausse balance est une abomination à l'Eternel; mais le poids juste lui plaît.
2 Kiburi kinapokuja, ndipo huja aibu, bali unyenyekevu huja na hekima.
L'orgueil est-il venu? aussi est venue l'ignominie; mais la sagesse est avec ceux qui sont modestes.
3 Uadilifu wa wenye haki huwaongoza, bali wasio waaminifu huharibiwa na hila yao.
L'intégrité des hommes droits les conduit; mais la perversité des perfides les détruit.
4 Utajiri haufaidi kitu katika siku ya ghadhabu, bali haki huokoa kutoka mautini.
Les richesses ne serviront de rien au jour de l'indignation; mais la justice garantira de la mort.
5 Haki ya wasio na lawama, huwatengenezea njia iliyonyooka, bali waovu huangushwa kwa uovu wao wenyewe.
La justice de l'homme intègre dresse sa voie; mais le méchant tombera par sa méchanceté.
6 Haki ya wanyofu huwaokoa, bali wasio waaminifu hunaswa na tamaa mbaya.
La justice des hommes droits les délivrera; mais les perfides seront pris dans [leur] méchanceté.
7 Wakati mtu mwovu anapokufa, matumaini yake hutoweka; yote aliyoyatazamia kutokana na nguvu zake huwa si kitu.
Quand l'homme méchant meurt, [son] attente périt; et l'espérance des hommes violents périra.
8 Mtu mwenye haki huokolewa kutoka taabu, naye mtu mwovu huingia humo badala yake.
Le juste est délivré de la détresse; mais le méchant entre en sa place.
9 Kwa kinywa chake mtu asiyemwamini Mungu humwangamiza jirani yake, bali kwa maarifa mwenye haki huokolewa.
Celui qui se contrefait de sa bouche corrompt son prochain; mais les justes [en] sont délivrés par la science.
10 Wakati mwenye haki anapofanikiwa, mji hufurahi; mwovu atowekapo, kuna kelele za furaha.
La ville s'égaye du bien des justes, et [il y a] chant de triomphe quand les méchants périssent.
11 Kutokana na baraka ya mtu mnyofu mji hukwezwa, bali kwa kinywa cha mwovu mji huharibiwa.
La ville est élevée par la bénédiction des hommes droits, mais elle est renversée par la bouche des méchants.
12 Mtu asiye na akili humdharau jirani yake, bali mtu mwenye ufahamu huuzuia ulimi wake.
Celui qui méprise son prochain, est dépourvu de sens; mais l'homme prudent se tait.
13 Masengenyo husaliti tumaini, bali mtu mwaminifu hutunza siri.
Celui qui va rapportant, révèle le secret; mais celui qui est de cœur fidèle, cèle la chose.
14 Pasipo ushauri wa hekima taifa huanguka, bali washauri wengi hufanya ushindi uwe wa hakika.
Le peuple tombe par faute de prudence, mais la délivrance est dans la multitude de gens de conseil.
15 Yeye amdhaminiye mgeni hakika atateseka, bali yeyote akataaye kuunga mkono dhamana ni salama.
Celui qui cautionne pour un étranger, ne peut manquer d'avoir du mal, mais celui qui hait ceux qui frappent [en la main], est assuré.
16 Mwanamke mwenye moyo wa huruma hupata heshima, bali wanaume wakorofi hupata mali tu.
La femme gracieuse obtient de l'honneur, et les hommes robustes obtiennent les richesses.
17 Mwenye huruma hujinufaisha mwenyewe, bali mkatili hujiletea taabu mwenyewe.
L'homme doux fait du bien à soi-même; mais le cruel trouble sa chair.
18 Mtu mwovu hupata ujira wa udanganyifu, bali yeye apandaye haki huvuna tuzo ya uhakika.
Le méchant fait une œuvre qui le trompe; mais la récompense est assurée à celui qui sème la justice.
19 Mtu mwenye haki kweli kweli hupata uzima, bali yeye afuatiliaye ubaya huendea kifo chake.
Ainsi la justice tend à la vie, et celui qui poursuit le mal tend à sa mort.
20 Bwana huwachukia sana watu wenye moyo wa upotovu, bali hupendezwa na wale ambao njia zao hazina lawama.
Ceux qui sont dépravés de cœur, sont en abomination à l'Eternel; mais ceux qui sont intègres dans leurs voies, lui sont agréables.
21 Uwe na hakika na hili: Waovu hawataepuka kuadhibiwa, bali wenye haki watakuwa huru.
De main en main le méchant ne demeurera point impuni; mais la race des justes sera délivrée.
22 Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe ndivyo alivyo mwanamke mzuri ambaye hana busara.
Une belle femme se détournant de la raison, est [comme] une bague d'or au museau d'une truie.
23 Shauku ya mwenye haki huishia tu kwenye mema, bali tumaini la mwovu huishia tu kwenye ghadhabu.
Le souhait des justes n'est que bien; [mais] l'attente des méchants n'est qu'indignation.
24 Kuna mtu atoaye kwa ukarimu, hata hivyo hupata zaidi, mwingine huzuia, lakini huwa maskini.
Tel répand, qui sera augmenté davantage; et tel resserre outre mesure, qui n'en aura que disette.
25 Mtu mkarimu atastawi; yeye awaburudishaye wengine ataburudishwa mwenyewe.
La personne qui bénit, sera engraissée; et celui qui arrose abondamment, regorgera lui-même.
26 Watu humlaani mtu awanyimae watu nafaka, bali baraka itamkalia kichwani kama taji yeye aliye radhi kuiuza.
Le peuple maudira celui qui retient le froment; mais la bénédiction [sera] sur la tête de celui qui le débite.
27 Yeye atafutaye mema hupata ukarimu, bali ubaya huja kwake yeye autafutaye.
Celui qui procure soigneusement le bien, acquiert de la faveur; mais le mal arrivera à celui qui le recherche.
28 Yeyote ategemeaye utajiri wake ataanguka, bali mwenye haki atastawi kama jani bichi.
Celui qui se fie en ses richesses, tombera; mais les justes reverdiront comme la feuille.
29 Yeye aletaye taabu kwa jamaa yake atarithi tu upepo, naye mpumbavu atakuwa mtumishi wa wenye hekima.
Celui qui ne gouverne pas sa maison par ordre, aura le vent pour héritage; et le fou sera serviteur du sage de cœur.
30 Tunda la mwenye haki ni mti wa uzima, naye mwenye hekima huvuta roho za watu.
Le fruit du juste est un arbre de vie; et celui qui gagne les âmes [est] sage.
31 Kama wenye haki watapokea ujira wao duniani, si zaidi sana yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi?
Voici, le juste reçoit en la terre sa rétribution, combien plus le méchant et le pécheur [la recevront-ils?]

< Mithali 11 >