< Obadia 1 >

1 Maono ya Obadia. Hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi kuhusu Edomu: Tumesikia ujumbe kutoka kwa Bwana: Mjumbe alitumwa kwa mataifa kusema, “Inukeni, twendeni tukapigane vita dhidi yake.”
La vision d'Abdias. Ainsi a dit le Seigneur l'Eternel touchant Edom: Nous avons ouï une publication de par l'Eternel, et un Envoyé a été dépêché parmi les nations, [et elles ont dit]: Courage levons-nous contre lui pour le combattre.
2 “Angalieni, nitawafanya wadogo miongoni mwa mataifa, mtadharauliwa kabisa.
Voici, je te rendrai petit entre les nations, tu seras fort méprisé.
3 Kiburi cha moyo wako kimekudanganya, wewe unayeishi katika majabali ya miamba na kufanya makao yako juu, wewe unayejiambia mwenyewe, ‘Ni nani awezaye kunishusha chini?’
L'orgueil de ton cœur t'a séduit, toi qui habites dans les fentes des rochers, qui sont ta haute demeure, et qui dis en ton cœur: Qui est-ce qui me renversera par terre?
4 Ingawa unapaa juu kama tai na kufanya kiota chako kati ya nyota, nitakushusha chini kutoka huko,” asema Bwana.
Quand tu aurais élevé ton nid comme l'aigle, et quand même tu l'aurais mis entre les étoiles, je te jetterai de là par terre, dit l'Eternel.
5 “Ikiwa wevi wangekuja kwako, ikiwa wanyangʼanyi wangekujia usiku: Lo! Tazama ni maafa kiasi gani yangekuwa yanakungojea: je, si wangeiba tu kiasi ambacho wangehitaji? Kama wachuma zabibu wangekuja kwako, je, wasingebakiza zabibu chache?
Sont-ce des larrons qui sont entrés chez toi, ou des voleurs de nuit? Comment [donc] as-tu été rasé? N'eussent-ils pas dérobé jusqu'à ce qu'ils en eussent eu assez? Si des vendangeurs fussent entrés chez toi, n'eussent-ils pas laissé quelque grappillage?
6 Lakini tazama jinsi Esau atakavyotekwa, jinsi hazina zake zilizofichwa zitatekwa nyara!
Comment a été fouillé Esaü? Comment ont été examinés ses lieux secrets?
7 Wote ulioungana nao watakufukuza hadi mpakani, rafiki zako watakudanganya na kukushinda, wale wanaokula mkate wako watakutegea mtego, lakini hutaweza kuugundua.
Tous tes alliés t'ont conduit jusqu'à la frontière; ceux qui étaient en paix avec toi t'ont trompé, et ont eu le dessus sur toi; ceux [qui mangeaient] ton pain t'ont donné le coup par-dessous, sans qu'on l'aperçût.
8 “Katika siku hiyo,” asema Bwana, “je, sitaangamiza watu wenye hekima wa Edomu, watu wenye ufahamu katika milima ya Esau?
Ne sera-ce pas en ce temps-là, dit l'Eternel, que je ferai périr les sages au milieu d'Edom, et la prudence dans la montagne d'Esaü?
9 Ee Temani, mashujaa wako watatiwa hofu, kila mmoja katika milima ya Esau ataangushwa chini kwa kuchinjwa.
Tes hommes forts seront aussi étonnés, ô Téman! afin que les hommes soient retranchés de la montagne d'Esaü, à force de les [y] tuer.
10 Kwa sababu ya jeuri uliyofanya dhidi ya ndugu yako Yakobo, aibu itakufunika; utaangamizwa milele.
La honte te couvrira, et tu seras retranché pour jamais, à cause de la violence [faite] à ton frère Jacob.
11 Siku ile ulisimama mbali ukiangalia wakati wageni walipojichukulia utajiri wake na watu wa nchi nyingine walipoingia malango yake wakipiga kura kwa ajili ya Yerusalemu, ulikuwa kama mmoja wao.
Lorsque tu te tenais vis-à-vis quand les étrangers menaient son armée en captivité, et que les forains entraient dans ses portes, et qu'ils jetaient le sort sur Jérusalem, tu étais aussi comme l'un d'eux.
12 Usingemdharau ndugu yako katika siku ya msiba wake, wala kufurahia juu ya watu wa Yuda katika siku ya maangamizi yao, wala kujigamba sana katika siku ya taabu yao.
Mais tu ne devais pas prendre plaisir à voir la journée de ton frère quand il a été livré aux étrangers, et tu ne devais pas te réjouir sur les enfants de Juda au jour qu'ils ont été détruits, et tu ne [les] devais pas braver au jour de la détresse.
13 Usingeingia katika malango ya watu wangu katika siku ya maafa yao, wala kuwadharau katika janga lao katika siku ya maafa yao, wala kunyangʼanya mali zao katika siku ya maafa yao.
Et tu ne devais pas entrer dans la porte de mon peuple au jour de sa calamité, et tu ne devais pas prendre plaisir, toi, dis-je, à voir son mal au jour de sa calamité, et [tes mains] ne se devaient pas avancer sur son bien, au jour de sa calamité.
14 Usingengoja kwenye njia panda na kuwaua wakimbizi wao, wala kuwatoa watu wake waliosalia katika siku ya shida yao.
Et tu ne te devais pas tenir sur les passages, pour exterminer ses réchappés; ni livrer ceux qui étaient restés, au jour de la détresse.
15 “Siku ya Bwana iko karibu kwa mataifa yote. Kama ulivyofanya, nawe utafanyiwa vivyo hivyo, matendo yako yatakurudia juu ya kichwa chako.
Car la journée de l'Eternel est proche sur toutes les nations; comme tu as fait, il te sera ainsi fait; ta récompense retournera sur ta tête.
16 Kama vile ulivyokunywa juu ya mlima wangu mtakatifu, vivyo hivyo mataifa yote watakunywa mfululizo, watakunywa na kunywa, nao watatoweka kana kwamba hawajawahi kuwepo.
Car comme vous avez bu sur la montagne de ma sainteté [la coupe de ma fureur], ainsi toutes les nations [la] boiront sans interruption; oui, elles [la] boiront, et [l']avaleront, et elles seront comme si elles n'avaient point été.
17 Lakini katika Mlima Sayuni kutakuwepo na wale watakaookoka; nao utakuwa mtakatifu, nayo nyumba ya Yakobo itamiliki urithi wake.
Mais il y aura des réchappés sur la montagne de Sion, et elle sera sainte, et la maison de Jacob possédera ses possessions.
18 Nyumba ya Yakobo itakuwa moto, na nyumba ya Yosefu itakuwa mwali wa moto; nayo nyumba ya Esau itakuwa bua kavu, nao wataiwasha moto na kuiteketeza. Hakutakuwa na watakaosalimika kutoka nyumba ya Esau.” Bwana amesema.
Et la maison de Jacob sera un feu, et la maison de Joseph une flamme, et la maison d'Esaü du chaume; ils s'allumeront parmi eux, et les consumeront; et il n'y aura rien de reste dans la maison d'Esaü; car l'Eternel a parlé.
19 Watu kutoka nchi ya Negebu wataikalia milima ya Esau, na watu kutoka miteremko ya vilima watamiliki nchi ya Wafilisti. Watayakalia mashamba ya Efraimu na Samaria, naye Benyamini atamiliki Gileadi.
Ils posséderont le Midi, [savoir] la montagne d'Esaü; et la campagne, [savoir] les Philistins, et ils posséderont le territoire d'Ephraïm, et le territoire de Samarie; et Benjamin [possédera] Galaad.
20 Kundi la Waisraeli walioko uhamishoni Kanaani watarudi na kumiliki nchi mpaka Sarepta. Walioko uhamishoni Sefaradi kutoka Yerusalemu watamiliki miji ya Negebu.
Et ces bandes des enfants d'Israël qui auront été transportés, [posséderont] ce qui était des Cananéens, jusqu'à Sarepta; et ceux de Jérusalem qui auront été transportés, [posséderont] ce qui [est] jusqu'à Sépharad, ils le posséderont avec les villes du Midi.
21 Waokoaji watakwea juu ya Mlima Sayuni kutawala milima ya Esau. Nao ufalme utakuwa wa Bwana.
Car les libérateurs monteront en la montagne de Sion, pour juger la montagne d'Esaü; et le Royaume sera à l'Eternel.

< Obadia 1 >