< Hesabu 9 >

1 Bwana akasema na Mose katika Jangwa la Sinai katika mwezi wa kwanza wa mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka Misri. Akasema,
And Jehovah spoke to Moses in the wilderness of Sinai, in the first month of the second year after their departure from the land of Egypt, saying,
2 “Waamuru Waisraeli waadhimishe Pasaka katika wakati ulioamriwa.
Let the children of Israel also hold the passover at its set time;
3 Adhimisheni wakati ulioamriwa, yaani wakati wa kuzama jua siku ya kumi na nne ya mwezi huu, kufuatana na desturi zake zote na masharti yake.”
on the fourteenth day in this month between the two evenings, ye shall hold it at its set time; according to all the rites of it, and according to all the ordinances thereof shall ye hold it.
4 Hivyo Mose akawaambia Waisraeli waiadhimishe Pasaka,
And Moses spoke to the children of Israel, that they should hold the passover.
5 nao wakafanya hivyo kwenye Jangwa la Sinai wakati wa kuzama jua siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza. Waisraeli wakafanya kila kitu kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.
And they held the passover in the first [month] on the fourteenth day of the month, between the two evenings, in the wilderness of Sinai: according to all that Jehovah had commanded Moses, so did the children of Israel.
6 Lakini baadhi yao hawakuweza kuadhimisha Pasaka siku ile kwa sababu walikuwa najisi kwa taratibu za kiibada kwa ajili ya kugusa maiti. Kwa hiyo wakamwendea Mose na Aroni siku ile ile,
And there were men, who were unclean through the dead body of a man, and could not hold the passover on that day; and they came before Moses and before Aaron on that day.
7 wakamwambia Mose, “Tumekuwa najisi kwa sababu tumegusa maiti, lakini kwa nini tuzuiliwe kumtolea Bwana sadaka yake pamoja na Waisraeli wengine katika wakati ulioamriwa?”
And those men said to him, We are unclean by reason of the dead body of a man: why are we kept back, that we may not present the offering of Jehovah at its set time among the children of Israel?
8 Mose akawajibu, “Ngojeni mpaka nitafute kile Bwana anachoagiza kuwahusu ninyi.”
And Moses said to them, Stay, and I will hear what Jehovah commands concerning you.
9 Ndipo Bwana akamwambia Mose,
And Jehovah spoke to Moses, saying,
10 “Waambie Waisraeli: ‘Wakati mmoja wenu au wazao wenu wanapokuwa najisi kwa sababu ya maiti au wakiwa safarini, hata hivyo wanaweza kuadhimisha Pasaka ya Bwana.
Speak unto the children of Israel, saying, If any one of you or of your generations be unclean by reason of a dead body or be on a journey afar off, yet he shall hold the passover to Jehovah.
11 Wataiadhimisha wakati wa kuzama jua siku ya kumi na nne ya mwezi wa pili. Watamla mwana-kondoo, pamoja na mkate usiotiwa chachu, na mboga chungu.
In the second month, on the fourteenth day, between the two evenings, shall they hold it; with unleavened bread and bitter herbs shall they eat it.
12 Wasibakize chochote hadi asubuhi wala wasivunje mifupa ya mwana-kondoo. Wakati wanapoadhimisha Pasaka, hawana budi kufuata masharti yote.
They shall leave none of it until the morning, nor break a bone thereof: according to every ordinance of the passover shall they hold it.
13 Lakini kama mtu ni safi kwa taratibu za kiibada naye hayuko safarini, asipoadhimisha Pasaka, mtu huyo hana budi kukatiliwa mbali na watu wake kwa sababu hakutoa sadaka ya Bwana kwa wakati ulioamriwa. Mtu huyo atawajibika kubeba matokeo ya dhambi yake.
But a man that is clean, and is not on a journey, and forbeareth to hold the passover, that soul shall be cut off from among his peoples; because he presented not the offering of Jehovah at its set time: that man shall bear his sin.
14 “‘Mgeni anayeishi miongoni mwenu ambaye anataka kuadhimisha Pasaka ya Bwana, lazima afanye hivyo kwa kufuata desturi na masharti. Lazima masharti yawe sawasawa kwa mgeni na mzawa.’”
And if a stranger shall sojourn among you, and would hold the passover to Jehovah, according to the rite of the passover, and according to the ordinance thereof, so shall he do. Ye shall have one rite, both for the stranger and for him that is born in the land.
15 Katika siku hiyo ambayo Maskani, Hema la Ushuhuda, iliposimamishwa, wingu liliifunika. Kuanzia jioni mpaka asubuhi wingu lililokuwa juu ya Maskani lilionekana kama moto.
And on the day that the tabernacle was set up, the cloud covered the tabernacle of the tent of testimony; and at even it was upon the tabernacle as the appearance of fire, until the morning.
16 Hivyo ndivyo lilivyoendelea kuwa; wingu liliifunika wakati wa mchana, na usiku lilionekana kama moto.
So it was continually: the cloud covered it, and at night it was as the appearance of fire.
17 Wakati wowote wingu lilipoinuka kutoka juu ya Hema, nao Waisraeli waliondoka; mahali popote wingu liliposimama, Waisraeli walipiga kambi.
And when the cloud rose from the tent, then the children of Israel journeyed; and at the place where the cloud stood still, there the children of Israel encamped.
18 Kwa amri ya Bwana Waisraeli waliondoka, na kwa amri yake walipiga kambi. Kwa muda wote wingu liliposimama juu ya Maskani, Waisraeli walibaki wamepiga kambi.
According to the commandment of Jehovah the children of Israel journeyed, and according to the commandment of Jehovah they [remained] encamped; all the days that the cloud dwelt upon the tabernacle they encamped.
19 Wakati wingu lilipobaki juu ya Maskani kwa muda mrefu, Waisraeli walitii amri ya Bwana nao hawakuondoka.
And when the cloud was long upon the tabernacle many days, then the children of Israel kept the charge of Jehovah, and journeyed not.
20 Wakati mwingine wingu lilikuwa juu ya Maskani kwa siku chache tu; kwa amri ya Bwana wangelipiga kambi na kisha kwa amri yake wangeliondoka.
And if it were so that the cloud was a few days upon the tabernacle, according to the commandment of Jehovah they encamped, and according to the commandment of Jehovah they journeyed.
21 Wakati mwingine wingu lilikuwepo kuanzia jioni mpaka asubuhi tu, na lilipoinuka asubuhi, nao waliondoka. Ikiwa ni mchana au usiku, wakati wowote wingu lilipoinuka, waliondoka.
And if it were so that the cloud was there from the evening until the morning, and that the cloud was taken up in the morning, then they journeyed; or a day and a night, and the cloud was taken up, they journeyed;
22 Ikiwa wingu lilikaa juu ya Maskani kwa siku mbili au mwezi au mwaka, Waisraeli wangebaki wamepiga kambi na hawakuondoka; lakini lilipoinuka, wangeondoka.
or two days, or a month, or many days, when the cloud was long upon the tabernacle, dwelling upon it, the children of Israel [remained] encamped, and journeyed not; but when it was taken up, they journeyed.
23 Kwa amri ya Bwana walipiga kambi, na kwa amri ya Bwana waliondoka. Walitii amri ya Bwana, kufuatana na agizo lake kupitia Mose.
At the commandment of Jehovah they encamped, and at the commandment of Jehovah they journeyed: they kept the charge of Jehovah according to the commandment of Jehovah through Moses.

< Hesabu 9 >