< Hesabu 33 >

1 Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni.
To so potovanja Izraelovih otrok, ki so odšli naprej iz egiptovske dežele, s svojimi vojskami, pod Mojzesovo in Aronovo roko.
2 Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:
Mojzes je po Gospodovi zapovedi zapisal njihova odhajanja, glede na njihova potovanja, in to so njihova potovanja glede na njihova odhajanja.
3 Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote,
V prvem mesecu so se odpravili iz Ramesésa, na petnajsti dan prvega meseca. Naslednji dan po pashi so Izraelovi otroci odšli ven z dvignjeno roko pred očmi vseh Egipčanov.
4 waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.
Kajti Egipčani so pokopali vse svoje prvorojence, ki jih je Gospod udaril med njimi. Tudi nad njihovimi bogovi je Gospod izvršil sodbe.
5 Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
Izraelovi otroci so se odpravili iz Ramesésa in se utaborili v Sukótu.
6 Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
Odrinili so iz Sukóta in se utaborili v Etámu, ki je na robu divjine.
7 Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.
Odpravili so se iz Etáma in se ponovno obrnili k Pi Hahirótu, ki je pred Báal Cefónom in se utaborili pred Migdólom.
8 Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.
Odrinili so izpred Pi Hahiróta in prešli skozi sredo morja v divjino in odšli na tridnevno potovanje v Etámsko divjino in se utaborili v Mari.
9 Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.
Odpravili so se iz Mare in prišli v Elím in v Elímu je bilo dvanajst vodnih studencev in sedemdeset palmovih dreves in tam so se utaborili.
10 Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.
Odpravili so se iz Elíma in se utaborili pri Rdečem morju.
11 Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.
Odpravili so se od Rdečega morja in se utaborili v Sinski divjini.
12 Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.
Šli so na svoje potovanje iz Sinske divjine in se utaborili v Dofki.
13 Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.
Odrinili so iz Dofke in se utaborili v Alúšu.
14 Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.
Odpravili so se iz Alúša in se utaborili pri Refidímu, kjer ni bilo vode za ljudstvo, da pije.
15 Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.
Odrinili so iz Refidíma in se utaborili v Sinajski divjini.
16 Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.
Odpravili so se iz Sinajske puščave in se utaborili pri Kibrot-Hattaavi.
17 Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.
Odpravili so se iz Kibrot-Hattaave in se utaborili pri Hacerótu.
18 Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.
Odpravili so se iz Haceróta in se utaborili v Ritmi.
19 Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.
Odpravili so se iz Ritme in se utaborili pri Rimón Perecu.
20 Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.
Odpotovali so iz Rimón Pereca in se utaborili v Libni.
21 Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.
Odpravili so se iz Libne in se utaborili pri Risi.
22 Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.
Odpotovali so iz Rise in se utaborili v Keheláti.
23 Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.
Odšli so iz Keheláte in se utaborili na gori Šefer.
24 Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.
Odpravili so se z gore Šefer in se utaborili v Harádi.
25 Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.
Odpravili so se iz Haráde in se utaborili v Makhelótu.
26 Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.
Odpravili so se iz Makhelóta in se utaborili pri Tahatu.
27 Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.
Odpotovali so od Tahata in se utaborili pri Tarahu.
28 Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.
Odpravili so se od Taraha in se utaborili v Mitki.
29 Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.
Odšli so iz Mitke in se utaborili v Hašmóni.
30 Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.
Odpotovali so iz Hašmóne in se utaborili pri Moserótu.
31 Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.
Odrinili so iz Moseróta in se utaborili v Bené Jaakánu.
32 Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.
Odpravili so se iz Bené Jaakána in se utaborili pri Hor Hagidgadu.
33 Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.
Odšli so iz Hor Hagidgada in se utaborili v Jotbáti.
34 Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.
Odpravili so se iz Jotbáte in se utaborili pri Abróni.
35 Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.
Odrinili so iz Abróne in se utaborili pri Ecjón Geberju.
36 Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.
Odpravili so se iz Ecjón Geberja in se utaborili v Cinski divjini, ki je Kadeš.
37 Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu.
Odpravili so se iz Kadeša in se utaborili na gori Hor, na robu edómske dežele.
38 Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri.
Duhovnik Aron je odšel gor na goro Hor, po Gospodovi zapovedi in tam, v štiridesetem letu, potem ko so Izraelovi otroci prišli iz egiptovske dežele, umrl, na prvi dan petega meseca.
39 Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.
Aron je bil star sto triindvajset let, ko je umrl na gori Hor.
40 Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
Kralj Arád, Kánaanec, ki je prebival na jugu kánaanske dežele, je slišal o prihajanju Izraelovih otrok.
41 Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.
Odpravili so se z gore Hor in se utaborili v Calmóni.
42 Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.
Odšli so iz Calmóne in se utaborili v Punónu.
43 Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.
Odšli so iz Punóna in se utaborili v Obótu.
44 Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.
Odšli so iz Obóta in se utaborili v Ijé Abarímu, na moábski meji.
45 Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.
Odšli so iz Ijíma in se utaborili v Dibón Gadu.
46 Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.
Odpravili so se iz Dibón Gada in se utaborili v Almón Diblatájemi.
47 Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.
Odpravili so se iz Almón Diblatájeme in se utaborili na gorovju Abaríma, pred Nebójem.
48 Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
Odrinili so z gorovja Abarím in se utaborili na moábskih ravninah pri Jordanu, blizu Jerihe.
49 Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.
Utaborili so se pri Jordanu, od Bet Ješimóta celo do Abél Šitíma, na moábskih ravninah.
50 Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose,
In Gospod je spregovoril Mojzesu na moábskih ravninah poleg Jordana, blizu Jerihe, rekoč:
51 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani,
»Govori Izraelovim otrokom in jim reci: ›Ko prečkate Jordan, v kánaansko deželo,
52 wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada.
potem boste izpred sebe napodili vse prebivalce dežele, uničili vse njihove slike, uničili vse njihove ulite podobe, popolnoma uničili vse njihove visoke kraje
53 Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki.
in razlastili boste prebivalce dežele in prebivali v njej, kajti dal sem vam deželo, da jo zavzamete.
54 Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.
Deželo boste razdelili z žrebom za dediščino med svojimi družinami in številčnejšemu boste dali več dediščine in maloštevilnemu boste dali manj dediščine. Dediščina vsakogar bo na kraju, kjer pade njegov žreb. Dedovali boste glede na rodove svojih očetov.
55 “‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi.
Toda če izpred sebe ne boste napodili prebivalcev dežele, potem se bo zgodilo, da bodo tisti, ki jih boste izmed njih pustili, bodice v vaših očeh in trni v vaših bokih in vas bodo dražili v deželi, v kateri prebivate.
56 Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’”
Poleg tega se bo zgodilo, da vam bom storil, kakor sem mislil storiti njim.‹«

< Hesabu 33 >