< Hesabu 33 >

1 Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni.
These are the journeys of the children of Israel, when they went forth out of the land of Egypt by their armies under the hand of Moses and Aaron.
2 Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:
Moses wrote their goings out according to their journeys by the commandment of the LORD: and these are their journeys according to their goings out.
3 Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote,
They traveled from Rameses in the first month, on the fifteenth day of the first month; on the next day after the Passover the children of Israel went out triumphantly in the sight of all the Egyptians,
4 waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.
while the Egyptians were burying all their firstborn, whom the LORD had struck among them: on their gods also the LORD executed judgments.
5 Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
The children of Israel traveled from Rameses, and camped in Succoth.
6 Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
They traveled from Succoth, and camped in Etham, which is in the edge of the wilderness.
7 Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.
They traveled from Etham, and turned back to Pihahiroth, which is before Baal Zephon: and they camped before Migdol.
8 Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.
They traveled from before Hahiroth, and passed through the midst of the sea into the wilderness: and they went three days' journey in the wilderness of Etham, and camped in Marah.
9 Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.
They traveled from Marah, and came to Elim: and in Elim were twelve springs of water, and seventy palm trees; and they camped there.
10 Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.
They traveled from Elim, and camped by the Red Sea.
11 Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.
They traveled from the Red Sea, and camped in the wilderness of Sin.
12 Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.
They traveled from the wilderness of Sin, and camped in Dophkah.
13 Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.
They traveled from Dophkah, and camped in Alush.
14 Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.
They traveled from Alush, and camped in Rephidim, where there was no water for the people to drink.
15 Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.
They traveled from Rephidim, and camped in the wilderness of Sinai.
16 Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.
They traveled from the wilderness of Sinai, and camped in Kibroth Hattaavah.
17 Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.
They traveled from Kibroth Hattaavah, and camped in Hazeroth.
18 Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.
They traveled from Hazeroth, and camped in Rithmah.
19 Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.
They traveled from Rithmah, and camped in Rimmon Perez.
20 Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.
They traveled from Rimmon Perez, and camped in Libnah.
21 Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.
They traveled from Libnah, and camped in Rissah.
22 Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.
They traveled from Rissah, and camped in Kehelathah.
23 Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.
They traveled from Kehelathah, and camped in Mount Shepher.
24 Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.
They traveled from Mount Shepher, and camped in Haradah.
25 Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.
They traveled from Haradah, and camped in Makheloth.
26 Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.
They traveled from Makheloth, and camped in Tahath.
27 Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.
They traveled from Tahath, and camped in Terah.
28 Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.
They traveled from Terah, and camped in Mithkah.
29 Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.
They traveled from Mithkah, and camped in Hashmonah.
30 Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.
They traveled from Hashmonah, and camped in Moseroth.
31 Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.
They traveled from Moseroth, and camped in Bene Jaakan.
32 Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.
They traveled from Bene Jaakan, and camped in Hor Haggidgad.
33 Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.
They traveled from Hor Haggidgad, and camped in Jotbathah.
34 Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.
They traveled from Jotbathah, and camped in Abronah.
35 Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.
They traveled from Abronah, and camped in Ezion Geber.
36 Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.
They traveled from Ezion Geber, and camped in the wilderness of Zin (that is, Kadesh).
37 Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu.
They traveled from Kadesh, and camped in Mount Hor, in the edge of the land of Edom.
38 Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri.
Aaron the priest went up into Mount Hor at the commandment of the LORD, and died there, in the fortieth year after the children of Israel had come out of the land of Egypt, in the fifth month, on the first day of the month.
39 Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.
Aaron was one hundred twenty-three years old when he died in Mount Hor.
40 Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
The Canaanite, the king of Arad, who lived in the Negev in the land of Canaan, heard of the coming of the children of Israel.
41 Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.
They traveled from Mount Hor, and camped in Zalmonah.
42 Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.
They traveled from Zalmonah, and camped in Punon.
43 Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.
They traveled from Punon, and camped in Oboth.
44 Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.
They traveled from Oboth, and camped in Iye Abarim, in the border of Moab.
45 Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.
They traveled from Iyim, and camped in Dibon Gad.
46 Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.
They traveled from Dibon Gad, and camped in Almon Diblathaim.
47 Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.
They traveled from Almon Diblathaim, and camped in the mountains of Abarim, before Nebo.
48 Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
They traveled from the mountains of Abarim, and camped in the plains of Moab by the Jordan at Jericho.
49 Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.
They camped by the Jordan, from Beth Jeshimoth even to Abel Shittim in the plains of Moab.
50 Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose,
The LORD spoke to Moses in the plains of Moab by the Jordan at Jericho, saying,
51 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani,
Speak to the children of Israel, and tell them, "When you pass over the Jordan into the land of Canaan,
52 wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada.
then you shall drive out all the inhabitants of the land from before you, destroy all their stone idols, destroy all their molten images, and demolish all their high places.
53 Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki.
You shall take possession of the land, and dwell in it; for I have given the land to you to possess it.
54 Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.
You shall inherit the land by lot according to your families; to the more you shall give the more inheritance, and to the fewer you shall give the less inheritance: wherever the lot falls to any man, that shall be his. You shall inherit according to the tribes of your fathers.
55 “‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi.
"But if you do not drive out the inhabitants of the land from before you, then those you let remain of them will be as pricks in your eyes and as thorns in your sides, and they will harass you in the land in which you dwell.
56 Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’”
It shall happen that as I thought to do to them, so will I do to you."

< Hesabu 33 >