< Hesabu 33 >

1 Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni.
These are the iourneyes of the children of Israel, which went out of the land of Egypt according to their bands vnder the hand of Moses and Aaron.
2 Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:
And Moses wrote their going out by their iourneies according to ye commandement of the Lord: so these are ye iourneies of their going out.
3 Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote,
Nowe they departed from Rameses the first moneth, euen the fifteenth day of the first moneth, on the morowe after the Passeouer: and the children of Israel went out with an hie hand in the sight of all the Egyptians.
4 waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.
(For the Egyptians buried all their first borne, which the Lord had smitten among them: vpon their gods also the Lord did execution.)
5 Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
And the children of Israel remoued from Rameses, and pitched in Succoth.
6 Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
And they departed from Succoth, and pitched in Etham, which is in the edge of the wildernesse.
7 Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.
And they remoued from Etham, and turned againe vnto Pi-hahiroth, which is before Baal-zephon, and pitched before Migdol.
8 Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.
And they departed from before Hahiroth, and went through the middes of the Sea into the wildernesse, and went three dayes iourney in the wildernesse of Etham, and pitched in Marah.
9 Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.
And they remoued from Marah, and came vnto Elim, and in Elim were twelue fountaines of water, and seuentie palme trees, and they pitched there.
10 Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.
And they remoued from Elim, and camped by the red Sea.
11 Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.
And they remoued from the red Sea, and lay in the wildernesse of Sin.
12 Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.
And they tooke their iourney out of the wildernesse of Sin, and set vp their tentes in Dophkah.
13 Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.
And they departed from Dophkah, and lay in Alush.
14 Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.
And they remoued from Alush, and lay in Rephidim, where was no water for the people to drinke.
15 Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.
And they departed from Rephidim, and pitched in the wildernesse of Sinai.
16 Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.
And they remoued from the desert of Sinai, and pitched in Kibroth Hattaauah.
17 Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.
And they departed from Kibroth Hattaauah, and lay at Hazeroth.
18 Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.
And they departed from Hazeroth, and pitched in Rithmah.
19 Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.
And they departed from Rithmah, and pitched at Rimmon Parez.
20 Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.
And they departed from Rimmon Parez, and pitched in Libnah.
21 Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.
And they remoued from Libnah, and pitched in Rissah.
22 Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.
And they iourneyed from Rissah, and pitched in Kehelathah.
23 Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.
And they went from Kehelathah, and pitched in mount Shapher.
24 Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.
And they remoued from mount Shapher, and lay in Haradah.
25 Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.
And they remoued from Haradah, and pitched in Makheloth.
26 Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.
And they remoued from Makheloth, and lay in Tahath.
27 Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.
And they departed from Tahath, and pitched in Tarah.
28 Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.
And they remoued from Tarah, and pitched in Mithkah.
29 Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.
And they went from Mithkah, and pitched in Hashmonah.
30 Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.
And they departed from Hashmonah, and lay in Moseroth.
31 Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.
And they departed from Moseroth, and pitched in Bene-iaakan.
32 Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.
And they remoued from Bene-iaakan, and lay in Hor-hagidgad.
33 Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.
And they went from Hor-hagidgad, and pitched in Iotbathah.
34 Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.
And they remoued from Iotbathah, and lay in Ebronah.
35 Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.
And they departed from Ebronah, and lay in Ezion-gaber.
36 Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.
And they remoued from Ezion-gaber, and pitched in the wildernesse of Zin, which is Kadesh.
37 Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu.
And they remooued from Kadesh, and pitched in mount Hor, in the edge of the land of Edom.
38 Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri.
(And Aaron the Priest went vp into mount Hor, at the commandement of the Lord, and died there, in the fourtieth yeere after the children of Israel were come out of the lande of Egypt, in the first day of the fifth moneth.
39 Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.
And Aaron was an hundreth, and three and twentie yeere olde, when hee dyed in mount Hor.
40 Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
And King Arad the Canaanite, which dwelt in the South of the land of Canaan, heard of the comming of the children of Israel)
41 Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.
And they departed from mount Hor, and pitched in Zalmonah.
42 Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.
And they departed from Zalmonah, and pitched in Punon.
43 Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.
And they departed from Punon, and pitched in Oboth.
44 Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.
And they departed from Oboth, and pitched in Iie-abarim, in the borders of Moab.
45 Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.
And they departed from Iim, and pitched in Dibon-gad.
46 Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.
And they remooued from Dibon-gad, and lay in Almon-diblathaim.
47 Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.
And they remooued from Almon-diblathaim, and pitched in the mountaines of Abarim before Nebo.
48 Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
And they departed from the mountaines of Abarim, and pitched in the plaine of Moab, by Iorden toward Iericho.
49 Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.
And they pitched by Iorden, from Bethieshimoth vnto Abel-shittim in the playne of Moab.
50 Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose,
And the Lord spake vnto Moses in the playne of Moab, by Iorden towarde Iericho, saying,
51 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani,
Speake vnto the children of Israel, and say vnto them, When ye are come ouer Iorden to enter into the land of Canaan,
52 wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada.
Ye shall then driue out all the inhabitants of the land before you, and destroy all their pictures, and breake asunder all their images of metall, and plucke downe all their hie places.
53 Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki.
And ye shall possesse the lande and dwell therein: for I haue giue you ye land to possesse it.
54 Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.
And ye shall inherite the land by lot according to your families: to the more yee shall giue more inheritance, and to the fewer the lesse inheritance. Where the lot shall fall to any man, that shall be his: according to the tribes of your fathers shall ye inherite.
55 “‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi.
But if ye will not driue out the inhabitants of the land before you, then those which yee let ramaine of them, shalbe prickes in your eyes, and thornes in your sides, and shall vexe you in the land wherein ye dwell.
56 Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’”
Moreouer, it shall come to passe, that I shall doe vnto you, as I thought to do vnto them.

< Hesabu 33 >