< Hesabu 31 >

1 Bwana akamwambia Mose,
Jehovah spoke to Moses, saying,
2 “Uwalipize kisasi Wamidiani kwa ajili ya Waisraeli. Halafu baada ya hayo, utakufa.”
"Avenge the children of Israel for the Midianites. Afterward you shall be gathered to your people."
3 Kwa hiyo Mose akawaambia watu, “Waandaeni baadhi ya wanaume wenu waende vitani kupigana na Wamidiani ili wawalipize kisasi cha Bwana.
Moses spoke to the people, saying, "Arm men from among you for the war, that they may go against Midian, to execute Jehovah's vengeance on Midian.
4 Peleka wanaume 1,000 vitani kutoka kila kabila la Israeli.”
Of every tribe one thousand, throughout all the tribes of Israel, you shall send to the war."
5 Kwa hiyo waliandaliwa wanaume 12,000 kwa vita, wanaume 1,000 kutoka kila kabila, walitolewa kutoka koo za Israeli.
So there were delivered, out of the thousands of Israel, a thousand of every tribe, twelve thousand armed for war.
6 Mose aliwatuma vitani, watu 1,000 kutoka kila kabila, pamoja na Finehasi mwana wa kuhani Eleazari, ambaye alichukua vyombo vya mahali patakatifu na tarumbeta za kuashiria.
Moses sent them, one thousand of every tribe, to the war, them and Phinehas the son of Eleazar the priest, to the war, with the vessels of the sanctuary and the trumpets for the alarm in his hand.
7 Walipigana dhidi ya Wamidiani, kama Bwana alivyomwagiza Mose, nao waliua kila mwanaume.
They warred against Midian, as Jehovah commanded Moses; and they killed every male.
8 Miongoni mwa watu waliouawa walikuwepo wafalme watano wa Midiani, nao ni Evi, Rekemu, Suri, Huri na Reba. Vilevile walimuua Balaamu mwana wa Beori kwa upanga.
They killed the kings of Midian with the rest of their slain: Evi, and Rekem, and Zur, and Hur, and Reba, the five kings of Midian: Balaam also the son of Beor they killed with the sword.
9 Waisraeli waliwateka wanawake wa Kimidiani pamoja na watoto wao na walichukua makundi ya ngʼombe, kondoo na mali zao kama nyara.
The children of Israel took captive the women of Midian and their little ones; and all their livestock, and all their flocks, and all their goods, they took for a prey.
10 Walichoma moto miji yote ambayo Wamidiani walikuwa wanaishi, pamoja na kambi zao zote.
All their cities in the places in which they lived, and all their encampments, they burnt with fire.
11 Walichukua nyara zote na mateka, pamoja na watu na wanyama,
They took all the spoil, and all the prey, both of man and of animal.
12 nao waliwaleta wafungwa mateka na nyara kwa Mose na kwa kuhani Eleazari, nao Waisraeli walikusanyika kwenye kambi zao katika tambarare za nchi ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
They brought the captives, and the prey, and the spoil, to Moses, and to Eleazar the priest, and to the congregation of the children of Israel, to the camp at the plains of Moab, which are by the Jordan at Jericho.
13 Mose, kuhani Eleazari na viongozi wote wa jumuiya wakatoka kuwalaki nje ya kambi.
Moses, and Eleazar the priest, and all the leaders of the congregation, went forth to meet them outside of the camp.
14 Mose aliwakasirikia maafisa wa jeshi, yaani hao wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia, ambao walirudi kutoka vitani.
Moses was angry with the officers of the army, the captains of thousands and the captains of hundreds, who came from the service of the war.
15 Mose akawauliza, “Je, mmewaacha wanawake wote hai?”
Moses said to them, "Have you saved all the women alive?
16 “Wanawake hao ndio waliofuata ushauri wa Balaamu, nao ndio waliowasababisha Waisraeli wamwasi Bwana kwa kile kilichotokea kule Peori, na kwa hiyo pigo liliwapata watu wa Bwana.
Look, these caused the children of Israel, through the counsel of Balaam, to commit trespass against Jehovah in the matter of Peor, and so the plague was among the congregation of Jehovah.
17 Sasa waue wavulana wote. Pia muue kila mwanamke ambaye alikwisha fanya tendo la ndoa,
Now therefore kill every male among the little ones, and kill every woman who has known man by lying with him.
18 lakini mwacheni hai kwa ajili yenu kila msichana ambaye kamwe hajawahi kuzini na mwanaume.
But all the girls, who have not known man by lying with him, keep alive for yourselves.
19 “Ninyi nyote ambao mmeua mtu yeyote au kumgusa mtu yeyote ambaye ameuawa, lazima mkae nje ya kambi kwa muda wa siku saba. Katika siku ya tatu na ya saba lazima mjitakase wenyewe pamoja na wafungwa wenu.
"Encamp outside of the camp seven days: whoever has killed any person, and whoever has touched any slain, purify yourselves on the third day and on the seventh day, you and your captives.
20 Takaseni kila vazi pamoja na kila kitu kilichotengenezwa kwa ngozi, kwa singa za mbuzi au kwa mti.”
As to every garment, and all that is made of skin, and all work of goats' hair, and all things made of wood, you shall purify yourselves."
21 Kisha kuhani Eleazari aliwaambia askari waliokuwa wamekwenda vitani, “Haya ndiyo matakwa ya sheria ambayo Bwana alimpa Mose:
Eleazar the priest said to the men of war who went to the battle, "This is the statute of the law which Jehovah has commanded Moses:
22 Dhahabu, fedha, shaba, chuma, bati, risasi,
however the gold, and the silver, the bronze, the iron, the tin, and the lead,
23 na kitu kingine chochote ambacho kinaweza kuhimili moto lazima mkipitishe kwenye moto, kisha kitakuwa safi. Lakini ni lazima pia kitakaswe kwa maji ya utakaso. Kitu chochote kisichoweza kuhimili moto lazima kipitishwe kwenye yale maji ya utakaso.
everything that may withstand the fire, you shall make to go through the fire, and it shall be clean; nevertheless it shall be purified with the water for impurity: and all that doesn't withstand the fire you shall make to go through the water.
24 Katika siku ya saba fueni nguo zenu, nanyi mtakuwa safi. Kisha mtaweza kuingia kambini.”
You shall wash your clothes on the seventh day, and you shall be clean; and afterward you shall come into the camp."
25 Bwana akamwambia Mose,
Jehovah spoke to Moses, saying,
26 “Wewe na kuhani Eleazari pamoja na viongozi wa jamaa ya jumuiya mtahesabu watu wote na wanyama ambao walitekwa.
"Take the sum of the prey that was taken, both of man and of animal, you, and Eleazar the priest, and the heads of the ancestral houses of the congregation;
27 Gawanyeni hizo nyara kati ya askari ambao walishiriki katika vita na kwa jumuiya.
and divide the prey into two parts: between the men skilled in war, who went out to battle, and all the congregation.
28 Kutoka fungu la wale waliokwenda kupigana vitani, tenga kama ushuru kwa ajili ya Bwana kitu kimoja kati ya kila mia tano, ikiwa ni wanadamu, ngʼombe, punda, kondoo au mbuzi.
Levy a tribute to Jehovah of the men of war who went out to battle: one soul of five hundred; of the persons, of the cattle, of the donkeys, and of the flocks.
29 Chukua ushuru huu kutoka fungu lao, umpe kuhani Eleazari kama sehemu ya Bwana.
Take it of their half, and give it to Eleazar the priest, for Jehovah's wave offering.
30 Kutoka fungu la Waisraeli, chukua kitu kimoja kati ya kila hamsini, ikiwa ni wanadamu, ngʼombe, punda, kondoo, mbuzi au wanyama wengine. Hivyo uwape Walawi, ambao wanawajibika kutunza Maskani ya Bwana.”
Of the children of Israel's half, you shall take one drawn out of every fifty, of the persons, of the cattle, of the donkeys, and of the flocks, of all the livestock, and give them to the Levites, who perform the duty of the tabernacle of Jehovah."
31 Kwa hiyo Mose na kuhani Eleazari wakafanya kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Moses and Eleazar the priest did as Jehovah commanded Moses.
32 Nyara zilizobaki kutoka mateka ambayo askari walichukua ni kondoo 675,000,
Now the prey, over and above the booty which the men of war took, was six hundred seventy-five thousand sheep,
33 ngʼombe 72,000,
and seventy-two thousand head of cattle,
34 punda 61,000,
and sixty-one thousand donkeys,
35 na wanawake 32,000 ambao hawakumjua mume kwa kufanya tendo la ndoa.
and thirty-two thousand persons in all, of the women who had not known man by lying with him.
36 Nusu ya fungu la wale waliokwenda kupigana vitani lilikuwa: Kondoo 337,500
The half, which was the portion of those who went out to war, was in number three hundred thirty-seven thousand five hundred sheep:
37 ambayo ushuru kwa ajili ya Bwana ilikuwa kondoo 675;
and Jehovah's tribute of the sheep was six hundred seventy-five.
38 ngʼombe 36,000 ambao ushuru kwa ajili ya Bwana ulikuwa ngʼombe 72;
The cattle were thirty-six thousand; of which Jehovah's tribute was seventy-two.
39 punda 30,500 ambao ushuru kwa ajili ya Bwana ulikuwa punda 61;
The donkeys were thirty thousand five hundred; of which Jehovah's tribute was sixty-one.
40 Watu 16,000 ambao ushuru kwa ajili ya Bwana ulikuwa watu 32.
The persons were sixteen thousand; of whom Jehovah's tribute was thirty-two persons.
41 Mose alimpa kuhani Eleazari ushuru kama sehemu ya Bwana, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Moses gave the tribute, which was Jehovah's wave offering, to Eleazar the priest, as Jehovah commanded Moses.
42 Ile nusu iliyokuwa ya Waisraeli, ambayo Mose aliitenga kutoka kwa ile ya watu waliokwenda vitani,
Of the children of Israel's half, which Moses divided off from the men who warred
43 nusu iliyokuwa ya jumuiya, ilikuwa kondoo 337,500,
(now the congregation's half was three hundred thirty-seven thousand five hundred sheep,
44 ngʼombe 36,000,
and thirty-six thousand head of cattle,
45 punda 30,500,
and thirty thousand five hundred donkeys,
46 na wanadamu 16,000.
and sixteen thousand persons),
47 Kutoka hiyo nusu iliyokuwa ya Waisraeli, Mose alichagua moja kati ya kila hamsini ya wanadamu na wanyama, kama Bwana alivyomwagiza, naye aliwapa Walawi, ambao waliwajibika kutunza Maskani ya Bwana.
even of the children of Israel's half, Moses took one drawn out of every fifty, both of man and of animal, and gave them to the Levites, who performed the duty of the tabernacle of Jehovah; as Jehovah commanded Moses.
48 Kisha maafisa waliokuwa juu ya vikosi vya jeshi, wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia, walimwendea Mose
The officers who were over the thousands of the army, the captains of thousands, and the captains of hundreds, came near to Moses;
49 na kumwambia, “Watumishi wako wamehesabu askari walio chini ya amri yetu na hakuna hata mmoja aliyekosekana.
and they said to Moses, "Your servants have taken the sum of the men of war who are under our command, and there lacks not one man of us.
50 Kwa hiyo tumeleta kama sadaka kwa Bwana vyombo vya dhahabu kila mmoja wetu alivyopata, yaani vikuku, bangili, pete za muhuri, vipuli na mikufu, ili kufanya upatanisho kwa ajili yetu mbele za Bwana.”
We have brought Jehovah's offering, what every man has gotten, of jewels of gold, armlets, and bracelets, signet rings, earrings, and necklaces, to make atonement for our souls before Jehovah."
51 Mose na kuhani Eleazari wakapokea kutoka kwao dhahabu, yaani vyombo vyote vilivyonakshiwa.
Moses and Eleazar the priest took their gold, even all worked jewels.
52 Dhahabu yote kutoka kwa wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia ambavyo Mose na kuhani Eleazari walimletea Bwana kama zawadi ilikuwa shekeli 16,750
All the gold of the wave offering that they offered up to Jehovah, of the captains of thousands, and of the captains of hundreds, was sixteen thousand seven hundred fifty shekels.
53 Kila askari alikuwa amejichukulia nyara zake binafsi.
(The men of war had taken booty, every man for himself.)
54 Mose na kuhani Eleazari walipokea dhahabu kutoka kwa wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia, wakazileta katika Hema la Kukutania kama ukumbusho kwa Waisraeli mbele za Bwana.
Moses and Eleazar the priest took the gold of the captains of thousands and of hundreds, and brought it into the Tent of Meeting, for a memorial for the children of Israel before Jehovah.

< Hesabu 31 >