< Hesabu 28 >

1 Bwana akamwambia Mose,
Jehovah spoke to Moses, saying,
2 “Wape Waisraeli agizo hili na uwaambie: ‘Hakikisheni kwamba mnaniletea mimi kwa wakati uliowekwa chakula kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa moto, kama harufu nzuri ya kupendeza.’
"Command the children of Israel, and tell them, 'My offering, my food for my offerings made by fire, of a pleasant aroma to me, you shall observe to offer to me in their due season.'
3 Waambie: ‘Hii ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto mnayomtolea Bwana: wana-kondoo wawili wa mwaka mmoja wasio na dosari, kama sadaka ya kawaida ya kuteketezwa kila siku.
You shall tell them, 'This is the offering made by fire which you shall offer to Jehovah: male lambs a year old without blemish, two day by day, for a continual burnt offering.
4 Andaa mwana-kondoo mmoja asubuhi na mwingine jioni,
You shall offer the one lamb in the morning, and you shall offer the other lamb at evening;
5 kila mmoja atolewe pamoja na sadaka ya nafaka sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa pamoja na robo ya hini ya mafuta ya zeituni.
with the tenth part of an ephah of fine flour for a meal offering, mixed with the fourth part of a hin of beaten oil.
6 Hii ni sadaka ya kawaida ya kuteketezwa iliyoanzishwa katika Mlima Sinai kama harufu nzuri ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
It is a continual burnt offering, which was ordained in Mount Sinai for a pleasant aroma, an offering made by fire to Jehovah.
7 Sadaka ya kinywaji itakayotolewa pamoja na kila mwana-kondoo ni robo ya hini ya kinywaji kilichochachuka. Mimina sadaka ya kinywaji kwa Bwana mahali patakatifu.
Its drink offering shall be the fourth part of a hin for the one lamb. You shall pour out a drink offering of strong drink to Jehovah in the holy place.
8 Andaa yule mwana-kondoo wa pili jioni, pamoja na sadaka ya nafaka na sadaka ya kinywaji kama ulivyofanya kwa ile sadaka nyingine ya asubuhi. Hii ni sadaka iliyotolewa kwa kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
The other lamb you shall offer at evening: as the meal offering of the morning, and as the drink offering of it, you shall offer it, an offering made by fire, of a pleasant aroma to Jehovah.
9 “‘Siku ya Sabato, utatoa sadaka ya wana-kondoo wawili wa mwaka mmoja wasiokuwa na dosari pamoja na sadaka yake ya kinywaji na sadaka ya nafaka yenye uzito wa sehemu mbili za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta.
"'On the Sabbath day two male lambs a year old without blemish, and two tenth parts of an ephah of fine flour for a meal offering, mixed with oil, and the drink offering of it:
10 Hii ni sadaka ya kuteketezwa itakayotolewa kwa ajili ya kila Sabato, pamoja na sadaka ya kawaida ya kuteketezwa na sadaka yake ya kinywaji.
this is the burnt offering of every Sabbath, besides the continual burnt offering, and the drink offering of it.
11 “‘Siku ya kwanza ya kila mwezi, mtamletea Bwana sadaka ya kuteketezwa ya fahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasiokuwa na dosari.
"'In the beginnings of your months you shall offer a burnt offering to Jehovah: two young bulls, and one ram, seven male lambs a year old without blemish;
12 Pamoja na kila fahali, kutakuwa na sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa, uliochanganywa na mafuta, pamoja na kondoo dume mmoja, sadaka ya nafaka ya unga laini uliochanganywa na mafuta;
and three tenth parts of an ephah of fine flour for a meal offering, mixed with oil, for each bull; and two tenth parts of fine flour for a meal offering, mixed with oil, for the one ram;
13 pamoja na kila mwana-kondoo, sadaka ya nafaka yenye uzito wa sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na mafuta. Hii ni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, harufu nzuri, sadaka ya kuteketezwa iliyotolewa kwa moto kwa Bwana.
and a tenth part of fine flour mixed with oil for a meal offering to every lamb; for a burnt offering of a pleasant aroma, an offering made by fire to Jehovah.
14 Pamoja na kila fahali kutakuwa na sadaka ya kinywaji nusu ya hini ya divai; pamoja na kila kondoo dume, theluthi moja ya hini, na pamoja na kila mwana-kondoo robo hini. Hii ni sadaka ya kuteketezwa ya kila mwezi itakayotolewa kila mwandamo wa mwezi kwa mwaka.
Their drink offerings shall be half a hin of wine for a bull, and the third part of a hin for the ram, and the fourth part of a hin for a lamb: this is the burnt offering of every month throughout the months of the year.
15 Zaidi ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya kinywaji, mbuzi mmoja dume atatolewa kwa Bwana kama sadaka ya dhambi.
One male goat for a sin offering to Jehovah; it shall be offered besides the continual burnt offering, and the drink offering of it.
16 “‘Katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza, itafanyika Pasaka ya Bwana.
"'In the first month, on the fourteenth day of the month, is Jehovah's Passover.
17 Katika siku ya kumi na tano ya mwezi huo itakuwa sikukuu; kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu.
On the fifteenth day of this month shall be a feast: seven days shall unleavened bread be eaten.
18 Katika siku ya kwanza mtakuwa na kusanyiko takatifu, msifanye kazi za kawaida.
In the first day shall be a holy convocation: you shall do no servile work;
19 Leteni mbele za Bwana sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya kuteketezwa ya mafahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja na wana-kondoo dume saba wenye umri wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
but you shall offer an offering made by fire, a burnt offering to Jehovah: two young bulls, and one ram, and seven male lambs a year old; they shall be to you without blemish;
20 Pamoja na kila fahali, andaa sadaka ya nafaka sehemu tatu za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, andaa sehemu mbili za kumi za efa;
and their meal offering, fine flour mixed with oil: you shall offer three tenth parts for a bull, and two tenth parts for the ram.
21 pia pamoja na kila mmoja wa wale wana-kondoo saba, andaa sehemu ya kumi ya efa.
You shall offer a tenth part for every lamb of the seven lambs;
22 Pia mtoe beberu mmoja kama sadaka ya dhambi ambaye atafanya upatanisho kwa ajili yenu.
and one male goat for a sin offering, to make atonement for you.
23 Andaa hizi licha ya zile sadaka za kawaida za kuteketezwa za kila asubuhi.
You shall offer these besides the burnt offering of the morning, which is for a continual burnt offering.
24 Kwa njia hii andaa chakula cha sadaka ya kuteketezwa kila siku, kwa siku saba kama harufu nzuri impendezayo Bwana. Hii itaandaliwa licha ya ile sadaka ya kawaida ya kuteketezwa ya kila siku pamoja na sadaka yake ya kinywaji.
In this way you shall offer daily, for seven days, the food of the offering made by fire, of a pleasant aroma to Jehovah: it shall be offered besides the continual burnt offering, and the drink offering of it.
25 Siku ya saba mwe na kusanyiko takatifu na msifanye kazi zenu za kawaida.
On the seventh day you shall have a holy convocation: you shall do no servile work.
26 “‘Siku ya malimbuko, mnapomletea Bwana sadaka ya nafaka mpya wakati wa Sikukuu ya Majuma, mwe na kusanyiko takatifu na msifanye kazi zenu za kawaida.
"'Also in the day of the first fruits, when you offer a new meal offering to Jehovah in your feast of weeks, you shall have a holy convocation; you shall do no servile work;
27 Mlete sadaka ya kuteketezwa ya mafahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja, na pia wana-kondoo saba wenye umri wa mwaka mmoja, kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
but you shall offer a burnt offering for a pleasant aroma to Jehovah: two young bulls, one ram, seven male lambs a year old;
28 Pamoja na kila fahali itatolewa sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, andaa sehemu mbili za kumi za efa za unga laini;
and their meal offering, fine flour mixed with oil, three tenth parts for each bull, two tenth parts for the one ram,
29 na sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kwa kila mmoja wa wana-kondoo saba.
a tenth part for every lamb of the seven lambs;
30 Ongeza beberu mmoja kwa kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
one male goat, to make atonement for you.
31 Andaa hizi sadaka pamoja na sadaka zake za vinywaji, kuwa nyongeza ya sadaka za kawaida za kuteketezwa, pamoja na sadaka yake ya nafaka. Hakikisha kuwa wanyama hao hawana dosari.
Besides the continual burnt offering, and the meal offering of it, you shall offer them (they shall be to you without blemish), and their drink offerings.

< Hesabu 28 >