< Hesabu 26 >

1 Baada ya hiyo tauni, Bwana akamwambia Mose na Eleazari mwana wa kuhani Aroni,
Da sotten var forbi, sa Herren til Moses og til Eleasar, sønn av Aron, presten:
2 “Hesabu jumuiya yote ya Kiisraeli kwa jamaa zao, wale wote wenye umri wa miaka ishirini na zaidi, ambao wanaweza kutumika katika jeshi la Israeli.”
Ta op manntall over hele Israels barns menighet fra tyveårsalderen og opover, efter deres familier, over alle dem i Israel som kan dra ut i strid.
3 Hivyo Mose na kuhani Eleazari wakazungumza na watu kwenye nchi tambarare ya Moabu, ngʼambo ya Yordani kutokea Yeriko, wakasema,
Og Moses og Eleasar, presten, talte med dem på Moabs ødemarker ved Jordan, midt imot Jeriko, og sa:
4 “Hesabuni wanaume wenye umri wa miaka ishirini na zaidi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.” Hawa ndio Waisraeli waliotoka Misri:
Fra tyveårsalderen og opover skal de mønstres - således som Herren hadde befalt Moses og Israels barn, dem som hadde draget ut av Egyptens land.
5 Wazao wa Reubeni, mwana mzaliwa wa kwanza wa Israeli, walikuwa: kutoka kwa Hanoki, ukoo wa Wahanoki; kutoka kwa Palu, ukoo wa Wapalu;
Ruben var Israels førstefødte; Rubens barn var: Fra Hanok hanokittenes ætt, fra Pallu pallu'ittenes ætt,
6 kutoka kwa Hesroni, ukoo wa Wahesroni; kutoka kwa Karmi, ukoo wa Wakarmi.
fra Hesron hesronittenes ætt, fra Karmi karmittenes ætt.
7 Hizi zilikuwa ndizo koo za Reubeni; wale waliohesabiwa walikuwa 43,730.
Dette var rubenittenes ætter, og de av dem som blev mønstret, var tre og firti tusen, syv hundre og tretti.
8 Mwana wa Palu alikuwa Eliabu,
Pallus sønn var Eliab,
9 nao wana wa Eliabu walikuwa Nemueli, Dathani na Abiramu. Hawa wawili Dathani na Abiramu ndio walikuwa maafisa wa jumuiya ambao walimwasi Mose na Aroni, na walikuwa miongoni mwa wafuasi wa Kora wakati walimwasi Bwana.
og Eliabs barn var Nemuel og Datan og Abiram. Det var den Datan og den Abiram som var utkåret av menigheten, og som yppet strid mot Moses og Aron dengang Korahs flokk satte sig op imot Herren,
10 Ardhi ilifunua kinywa chake na kuwameza pamoja na Kora, ambaye wafuasi wake walikufa wakati moto ulipowateketeza wanaume 250. Nao walikuwa kama alama ya onyo.
og jorden oplot sin munn og slukte både dem og Korah, og hele flokken omkom idet ilden fortærte de to hundre og femti menn, og de blev til et tegn;
11 Pamoja na hayo, hao ukoo wa Kora hawakufa.
men Korahs barn omkom ikke.
12 Wazao wa Simeoni kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Nemueli, ukoo wa Wanemueli; kutoka kwa Yamini, ukoo wa Wayamini; kutoka wa Yakini, ukoo wa Wayakini;
Simeons barn var efter sine ætter: Fra Nemuel nemuelittenes ætt, fra Jamin jaminittenes ætt, fra Jakin jakinittenes ætt,
13 kutoka kwa Zera, ukoo wa Wazera; kutoka kwa Shauli, ukoo wa Washauli.
fra Serah serahittenes ætt, fra Sa'ul sa'ulittenes ætt.
14 Hizi ndizo koo za Simeoni; walikuwa 22,200.
Dette var simeonittenes ætter, to og tyve tusen og to hundre.
15 Wazao wa Gadi kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Sifoni, ukoo wa Wasifoni; kutoka kwa Hagi, ukoo wa Wahagi; kutoka kwa Shuni, ukoo wa Washuni;
Gads barn var efter sine ætter: Fra Sefon sefonittenes ætt, fra Haggi haggittenes ætt, fra Suni sunittenes ætt,
16 kutoka kwa Ozni, ukoo wa Waozni; kutoka kwa Eri, ukoo wa Waeri;
fra Osni osnittenes ætt, fra Eri erittenes ætt,
17 kutoka kwa Arodi, ukoo wa Waarodi; kutoka kwa Areli, ukoo wa Waareli.
fra Arod arodittenes ætt, fra Areli arelittenes ætt.
18 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Gadi; wale waliohesabiwa walikuwa 40,500.
Dette var Gads barns ætter, så mange av dem som blev mønstret, firti tusen og fem hundre.
19 Eri na Onani walikuwa wana wa Yuda, lakini walifia huko Kanaani.
Judas barn var Er og Onan; men Er og Onan døde i Kana'ans land.
20 Wazao wa Yuda kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Shela, ukoo wa Washela; kutoka kwa Peresi, ukoo wa Waperesi; kutoka kwa Zera, ukoo wa Wazera.
Og Judas barn var efter sine ætter: Fra Sela selanittenes ætt, fra Peres peresittenes ætt, fra Serah serahittenes ætt.
21 Wazao wa Peresi walikuwa: kutoka kwa Hesroni, ukoo wa Wahesroni; kutoka kwa Hamuli, ukoo wa Wahamuli.
Peres' barn var: Fra Hesron hesronittenes ætt, fra Hamul hamulittenes ætt.
22 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Yuda; wale waliohesabiwa walikuwa 76,500.
Dette var Judas ætter, så mange av dem som blev mønstret, seks og sytti tusen og fem hundre.
23 Wazao wa Isakari kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Tola, ukoo wa Watola; kutoka kwa Puva, ukoo wa Wapuva;
Issakars barn var efter sine ætter: Fra Tola tola'ittenes ætt, fra Puva punittenes ætt,
24 kutoka kwa Yashubu, ukoo wa Wayashubu; kutoka kwa Shimroni, ukoo wa Washimroni.
fra Jasub jasubittenes ætt, fra Simron simronittenes ætt.
25 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Isakari; wale waliohesabiwa walikuwa 64,300.
Dette var Issakars ætter, så mange av dem som blev mønstret, fire og seksti tusen og tre hundre.
26 Wazao wa Zabuloni kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Seredi, ukoo wa Waseredi; kutoka kwa Eloni, ukoo wa Waeloni; kutoka kwa Yaleeli, ukoo wa Wayaleeli.
Sebulons barn var efter sine ætter: Fra Sered sardittenes ætt, fra Elon elonittenes ætt, fra Jahle'el jahle'elittenes ætt.
27 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Zabuloni, wale waliohesabiwa walikuwa 60,500.
Dette var sebulonittenes ætter, så mange av dem som blev mønstret, seksti tusen og fem hundre.
28 Wazao wa Yosefu kwa koo zao kutoka kwa Manase na kwa Efraimu walikuwa:
Josefs barn var efter sine ætter: Manasse og Efra'im.
29 Wazao wa Manase: kutoka kwa Makiri, ukoo wa Wamakiri (Makiri alikuwa baba wa Gileadi); kutoka kwa Gileadi, ukoo wa Wagileadi.
Manasses barn var: Fra Makir makirittenes ætt, og Makir var far til Gilead, fra Gilead gileadittenes ætt.
30 Hawa ndio waliokuwa wazao wa Gileadi: kutoka kwa Iezeri, ukoo wa Waiezeri; kutoka kwa Heleki, ukoo wa Waheleki;
Gileads barn det var: Fra Jeser jesrittenes ætt, fra Helek helkittenes ætt
31 kutoka kwa Asirieli, ukoo wa Waasirieli; kutoka kwa Shekemu, ukoo wa Washekemu;
og fra Asriel asrielittenes ætt og fra Sekem sikmittenes ætt
32 kutoka kwa Shemida, ukoo wa Washemida; kutoka kwa Heferi, ukoo wa Waheferi.
og fra Semida semida'ittenes ætt og fra Hefer hefrittenes ætt.
33 (Selofehadi mwana wa Heferi hakuzaa wana, bali alikuwa na watoto wa kike tu, ambao majina yao yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa.)
Men Selofhad, Hefers sønn, hadde ingen sønner, bare døtre, og Selofhads døtre hette Mahla og Noa, Hogla, Milka og Tirsa.
34 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Manase; wale waliohesabiwa walikuwa 52,700.
Dette var Manasses ætter, og de av dem som blev mønstret, var to og femti tusen og syv hundre.
35 Hawa walikuwa wazao wa Efraimu kwa koo zao: kutoka kwa Shuthela, ukoo wa Washuthela; kutoka kwa Bekeri, ukoo wa Wabekeri; kutoka kwa Tahani, ukoo wa Watahani;
Efra'ims barn det var efter deres ætter: Fra Sutelah sutelahittenes ætt, fra Beker bakrittenes ætt, fra Tahan tahanittenes ætt.
36 Hawa ndio walikuwa wazao wa Shuthela: kutoka kwa Erani, ukoo wa Waerani.
Sutelahs barn det var: Fra Eran eranittenes ætt.
37 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Efraimu; wale waliohesabiwa walikuwa 32,500. Hawa ndio waliokuwa wazao wa Yosefu kwa koo zao.
Dette var Efra'ims barns ætter, så mange av dem som blev mønstret, to og tretti tusen og fem hundre. Dette var Josefs barn efter deres ætter.
38 Wazao wa Benyamini kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Bela, ukoo wa Wabela; kutoka kwa Ashbeli, ukoo wa Waashbeli; kutoka kwa Ahiramu, ukoo wa Waahiramu;
Benjamins barn var efter sine ætter: Fra Bela balittenes ætt, fra Asbel asbelittenes ætt, fra Akiram akiramittenes ætt,
39 kutoka kwa Shufamu, ukoo wa Washufamu; kutoka kwa Hufamu, ukoo wa Wahufamu.
fra Sefufam sufamittenes ætt, fra Hufam hufamittenes ætt.
40 Wazao wa Bela kutoka kwa Ardi na Naamani walikuwa: kutoka kwa Ardi, ukoo wa Waardi; kutoka kwa Naamani, ukoo wa Wanaamani.
Belas barn var: Ard og Na'aman, fra Ard ardittenes ætt, fra Na'aman na'amittenes ætt.
41 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Benyamini; wale waliohesabiwa walikuwa 45,600.
Dette var Benjamins barn efter deres ætter, og de av dem som blev mønstret, var fem og firti tusen og seks hundre.
42 Hawa ndio waliokuwa wazao wa Dani kwa koo zao: kutoka kwa Shuhamu, ukoo wa Washuhamu. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Dani:
Dans barn var efter sine ætter: Fra Suham suhamittenes ætt. Dette var Dans ætter efter deres ættetavle.
43 Wote walikuwa koo za Washuhamu; wale waliohesabiwa walikuwa 64,400.
Alle suhamittenes ætter, så mange av dem som blev mønstret, var fire og seksti tusen og fire hundre.
44 Wazao wa Asheri kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Imna, ukoo wa Waimna; kutoka kwa Ishvi, ukoo wa Waishvi; kutoka kwa Beria, ukoo wa Waberia;
Asers barn var efter sine ætter: Fra Jimna jimna'ittenes ætt, fra Jisvi jisvittenes ætt, fra Beria beriittenes ætt;
45 kutoka kwa wazao wa Beria: kutoka kwa Heberi, ukoo wa Waheberi; kutoka kwa Malkieli, ukoo wa Wamalkieli.
av Berias barn: Fra Heber hebrittenes ætt, fra Malkiel malkielittenes ætt.
46 (Asheri alikuwa na binti aliyeitwa Sera.)
Asers datter hette Serah.
47 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Asheri; wale waliohesabiwa walikuwa 53,400.
Dette var Asers barns ætter, så mange av dem som blev mønstret, tre og femti tusen og fire hundre.
48 Wazao wa Naftali kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Yaseeli, ukoo wa Wayaseeli; kutoka kwa Guni, ukoo wa Waguni;
Naftalis barn var efter sine ætter: Fra Jahse'el jahse'elittenes ætt, fra Guni gunittenes ætt,
49 kutoka kwa Yeseri, ukoo wa Wayeseri; kutoka kwa Shilemu, ukoo wa Washilemu.
fra Jeser jisrittenes ætt, fra Sillem sillemittenes ætt.
50 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Naftali; wale waliohesabiwa walikuwa 45,400.
Dette var Naftalis ætter efter deres ættetavle, og de av dem som blev mønstret, var fem og firti tusen og fire hundre.
51 Jumla ya hesabu ya wanaume wa Israeli ilikuwa 601,730.
Dette var de av Israels barn som blev mønstret, seks hundre og ett tusen, syv hundre og tretti.
52 Bwana akamwambia Mose,
Og Herren talte til Moses og sa:
53 “Watagawiwa nchi kama urithi kwa kulingana na hesabu ya majina.
Mellem disse skal landet skiftes ut til arv efter folketallet.
54 Kundi kubwa zaidi lipe urithi mkubwa zaidi, na kundi dogo zaidi lipewe urithi mdogo zaidi; kila kundi litapokea urithi wake kulingana na hesabu ya wale walioorodheshwa.
Den stamme som er stor, skal du gi en stor arv, og den som er liten, skal du gi en liten arv; hver stamme skal få sin arv efter tallet på dem som blev mønstret der.
55 Hakikisha kuwa nchi inagawanywa kwa kura. Kile kitakachorithiwa na kila kikundi kitakuwa kwa kulingana na majina ya kabila la babu yao.
Men ved loddkasting skal landet skiftes ut; efter navnene på sine fedrenestammer skal de ta arv.
56 Kila urithi utagawanywa kwa kura miongoni mwa makundi makubwa na madogo.”
Efter som loddet faller, skal hver stamme, stor eller liten, få sin arv.
57 Hawa walikuwa Walawi ambao walihesabiwa kwa koo zao: kutoka kwa Gershoni, ukoo wa Wagershoni; kutoka kwa Kohathi, ukoo wa Wakohathi; kutoka kwa Merari, ukoo wa Wamerari.
Dette var de av levittene som blev mønstret, efter sine ætter: Fra Gerson gersonittenes ætt, fra Kahat kahatittenes ætt, fra Merari merarittenes ætt.
58 Hizi pia zilikuwa koo za Walawi: ukoo wa Walibni; ukoo wa Wahebroni; ukoo wa Wamahli; ukoo wa Wamushi; ukoo wa wana wa Kora. (Kohathi alikuwa baba aliyemzaa Amramu;
Dette var levittenes ætter: libnittenes ætt, hebronittenes ætt, mahlittenes ætt, musittenes ætt, korahittenes ætt. Kahat var far til Amram,
59 jina la mke wa Amramu ni Yokebedi, naye pia alikuwa mzao wa Lawi, ambaye alizaliwa kwa Walawi nchini Misri. Alimzalia Amramu: Aroni, Mose na dada yao Miriamu.
og Amrams hustru hette Jokebed; hun var datter av Levi og født i Egypten; og Amram fikk med henne Aron og Moses og deres søster Mirjam.
60 Aroni alikuwa baba yake Nadabu na Abihu, Eleazari na Ithamari.
Og Aron fikk sønnene Nadab og Abihu, Eleasar og Itamar;
61 Lakini Nadabu na Abihu walikufa wakati walitoa sadaka mbele za Bwana kwa moto usioruhusiwa.)
men Nadab og Abihu døde dengang de bar fremmed ild inn for Herrens åsyn.
62 Wanaume wote wa Walawi wa umri wa mwezi mmoja na zaidi walikuwa 23,000. Wao hawakuhesabiwa pamoja na Waisraeli wengine kwa sababu hawakupokea urithi miongoni mwao.
Og de av levittene som blev mønstret, var tre og tyve tusen, alt mannkjønn blandt dem fra den som var en måned gammel og opover; de blev ikke mønstret sammen med de andre Israels barn, fordi det ikke var gitt dem arv blandt Israels barn.
63 Hawa ndio walioorodheshwa na Mose na kuhani Eleazari wakati waliwahesabu Waisraeli kwenye nchi tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
Disse var det som blev mønstret av Moses og Eleasar, presten, da de mønstret Israels barn på Moabs ødemarker ved Jordan midt imot Jeriko,
64 Hakuna hata mmoja wao aliyekuwa miongoni mwa wale waliohesabiwa na Mose na kuhani Aroni wakati waliwahesabu Waisraeli katika Jangwa la Sinai.
og blandt disse var det ikke nogen av dem som blev mønstret av Moses og Aron, presten, dengang de mønstret Israels barn i Sinai ørken.
65 Kwa maana Bwana alikuwa amewaambia hao Waisraeli hakika wangekufa huko jangwani, wala hakuna mmoja wao aliyeachwa, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune na Yoshua mwana wa Nuni.
For Herren hadde sagt at de skulde dø i ørkenen. Og det var ingen tilbake av dem uten Kaleb, Jefunnes sønn, og Josva, Nuns sønn.

< Hesabu 26 >