< Hesabu 25 >

1 Israeli alipokuwa akikaa Shitimu, wanaume wa Israeli walianza kuzini na wanawake wa Kimoabu,
And Israel abode in Shittim, and the people began to commit lewdness with the daughters of Moab.
2 ambao waliwaalika kushiriki katika kutoa kafara kwa miungu yao. Watu wakala na kusujudu mbele ya miungu hii.
And they called the people to the sacrifices of their gods: and the people ate, and bowed down to their gods.
3 Kwa hiyo Israeli akaungana katika kumwabudu Baali wa Peori. Hasira ya Bwana ikawaka dhidi yao.
And Israel joined himself to Baal-peor: and the anger of the LORD was kindled against Israel.
4 Bwana akamwambia Mose, “Uwachukue viongozi wote wa watu hawa, uwaue na uwaweke hadharani mchana peupe mbele za Bwana, ili hasira kali ya Bwana iweze kuondoka kwa Israeli.”
And the LORD said to Moses, Take all the heads of the people, and hang them up before the LORD against the sun, that the fierce anger of the LORD may be turned away from Israel.
5 Kwa hiyo Mose akawaambia waamuzi wa Israeli, “Kila mmoja wenu lazima awaue wale wanaume wenu, walioshiriki katika kumwabudu Baali wa Peori.”
And Moses said to the judges of Israel, Slay ye every one his men that were joined to Baal-peor.
6 Ndipo mwanaume wa Kiisraeli akamleta mwanamke wa Kimidiani katika jamaa yake palepale mbele ya Mose na mkutano wote wa Israeli walipokuwa wakilia kwenye lango la Hema la Kukutania.
And, behold, one of the children of Israel came and brought to his brethren a Midianitish woman in the sight of Moses, and in the sight of all the congregation of the children of Israel, who [were] weeping [before] the door of the tabernacle of the congregation.
7 Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani Aroni, alipoona jambo hili, akaondoka kwenye kusanyiko, akachukua mkuki mkononi mwake,
And when Phinehas, the son of Eleazar, the son of Aaron the priest, saw [it], he rose from among the congregation, and took a javelin in his hand;
8 akamfuata yule Mwisraeli ndani ya hema. Akawachoma mkuki wote wawili kwa pamoja, ukapenya kwenye mwili wa yule Mwisraeli na mwili wa yule mwanamke. Ndipo tauni iliyokuwepo dhidi ya Waisraeli ikakoma.
And he went after the man of Israel into the tent, and thrust both of them through, the man of Israel, and the woman through her belly: So the plague was stayed from the children of Israel.
9 Lakini wale waliokufa kwa hiyo tauni walikuwa watu 24,000.
And those that died in the plague were twenty and four thousand.
10 Bwana akamwambia Mose,
And the LORD spoke to Moses, saying,
11 “Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani Aroni, amegeuza hasira yangu mbali na Waisraeli, kwa sababu alikuwa na wivu kama nilio nao kwa heshima yangu miongoni mwao, hata kwamba kwa wivu wangu sikuwaangamiza.
Phinehas, the son of Eleazar, the son of Aaron the priest, hath turned my wrath away from the children of Israel, (while he was zealous for my sake among them, ) that I consumed not the children of Israel in my jealousy.
12 Kwa hiyo mwambie Finehasi ninafanya Agano langu la amani naye.
Wherefore say, Behold, I give to him my covenant of peace.
13 Yeye pamoja na wazao wake watakuwa na Agano la ukuhani milele, kwa sababu alikuwa na wivu kwa ajili ya heshima ya Mungu wake, na akafanya upatanisho kwa Waisraeli.”
And he shall have it, and his seed after him, [even] the covenant of an everlasting priesthood; because he was zealous for his God, and made an atonement for the children of Israel.
14 Jina la Mwisraeli ambaye aliuawa pamoja na mwanamke wa Kimidiani ni Zimri mwana wa Salu, kiongozi wa jamaa ya Simeoni.
Now the name of the Israelite that was slain, [even] that was slain with the Midianitish woman, [was] Zimri, the son of Salu, a prince of a chief house among the Simeonites.
15 Jina la mwanamke wa Kimidiani aliyeuawa ni Kozbi binti wa Suri, aliyekuwa mkuu wa kabila la jamaa ya Wamidiani.
And the name of the Midianitish woman that was slain [was] Cozbi the daughter of Zur; he [was] head over a people, [and] of a chief house in Midian.
16 Bwana akamwambia Mose,
And the LORD spoke to Moses, saying,
17 “Watendeeni Wamidiani kama adui na mwaue,
Distress the Midianites, and smite them:
18 kwa sababu wao waliwatendea kama adui wakati waliwadanganya katika tukio la Peori na dada yao Kozbi, binti wa kiongozi wa Kimidiani, mwanamke ambaye aliuawa wakati tauni ilikuja kama matokeo ya tukio la Peori.”
For they distress you with their wiles, with which they have beguiled you in the matter of Peor, and in the matter of Cozbi, the daughter of a prince of Midian their sister, who was slain in the day of the plague for Peor's sake.

< Hesabu 25 >