< Hesabu 17 >

1 Bwana akamwambia Mose,
Jehovah spoke to Moses, saying,
2 “Sema na Waisraeli, na ujipatie fimbo kumi na mbili kutoka kwao, moja kutoka kwa kila mmoja wa viongozi wa kabila za baba zao. Andika jina la kila mtu kwenye fimbo yake.
"Speak to the children of Israel, and take of them rods, one for each fathers' house, of all their princes according to their fathers' houses, twelve rods: write every man's name on his rod.
3 Kwenye fimbo ya Lawi andika jina la Aroni, kwa maana ni lazima iwepo fimbo moja kwa kila kiongozi kwa ajili ya kila kabila la baba zao.
You shall write Aaron's name on the rod of Levi; for there shall be one rod for each head of their fathers' houses.
4 Ziweke hizo fimbo ndani ya Hema la Kukutania mbele ya Sanduku la Ushuhuda, mahali nikutanapo nawe.
You shall lay them up in the Tent of Meeting before the testimony, where I meet with you.
5 Fimbo ya mtu nitakayemchagua itachipuka, nami mwenyewe nitayakomesha haya manungʼuniko ya mara kwa mara ya Waisraeli dhidi yako.”
It shall happen, that the rod of the man whom I shall choose shall bud: and I will make to cease from me the murmurings of the children of Israel, which they murmur against you."
6 Hivyo Mose akasema na Waisraeli, nao viongozi wao wakampa fimbo kumi na mbili, fimbo moja kwa ajili ya kila kabila la baba zao, nayo fimbo ya Aroni ikiwa miongoni mwa hizo.
Moses spoke to the children of Israel; and all their leaders gave him rods, one for each leader, according to their ancestral houses, even twelve rods: and the rod of Aaron was among their rods.
7 Mose akaziweka hizo fimbo mbele za Bwana ndani ya Hema la Ushuhuda.
Moses laid up the rods before Jehovah in the tent of the testimony.
8 Siku iliyofuata Mose aliingia kwenye Hema la Ushuhuda akaona ile fimbo ya Aroni ambayo iliwakilisha jamaa ya Lawi haikuwa tu imechipuka, bali pia ilikuwa imetoa machipukizi, kuchanua maua na kuzaa malozi.
It happened on the next day, that Moses went into the tent of the testimony; and look, the rod of Aaron for the house of Levi was budded, and put forth buds, and produced blossoms, and bore ripe almonds.
9 Ndipo Mose akaleta zile fimbo zote kwa Waisraeli wote kutoka mbele za Bwana. Wakaziangalia, na kila mtu akaichukua fimbo yake mwenyewe.
Moses brought out all the rods from before Jehovah to all the children of Israel: and they looked, and took every man his rod.
10 Bwana akamwambia Mose, “Rudisha fimbo ya Aroni mbele ya Sanduku la Ushuhuda, ili ihifadhiwe kama alama kwa waasi. Hili litakomesha manungʼuniko yao dhidi yangu, ili kwamba wasife.”
Jehovah said to Moses, "Put back the rod of Aaron before the testimony, to be kept for a token against the rebels; that you may make an end of their murmurings against me, that they not die."
11 Mose akafanya kama Bwana alivyomwamuru.
Moses did so. As Jehovah commanded him, so he did.
12 Waisraeli wakamwambia Mose, “Tutakufa! Tumepotea, sote tumepotea!
The children of Israel spoke to Moses, saying, "Look, we perish. We are undone. We are all undone.
13 Yeyote akaribiaye Maskani ya Bwana atakufa. Je, sisi sote tutakufa?”
Everyone who comes near, who comes near to the tabernacle of Jehovah, dies. Will we all perish?"

< Hesabu 17 >