< Hesabu 16 >

1 Kora mwana wa Ishari, mwana wa Kohathi, mwana wa Lawi, pamoja na baadhi ya Wareubeni, yaani Dathani na Abiramu, wana wa Eliabu, na Oni mwana wa Pelethi, wakachukua baadhi ya watu,
و قورح بن یصهار بن قهات بن لاوی وداتان و ابیرام پسران الیاب و اون بن فالت پسران روبین (کسان ) گرفته،۱
2 wakainuka dhidi ya Mose. Pamoja nao walikuwepo wanaume wa Kiisraeli 250, watu waliojulikana, viongozi wa jumuiya waliokuwa wameteuliwa kuwa wakuu wa kusanyiko.
با بعضی ازبنی‌اسرائیل، یعنی دویست و پنجاه نفر ازسروران جماعت که برگزیدگان شورا و مردان معروف بودند، به حضور موسی برخاستند.۲
3 Wakaja kama kikundi kuwapinga Mose na Aroni, wakawaambia, “Ninyi mmejitukuza sana! Kusanyiko hili lote ni takatifu, kila mmoja wao, naye Bwana yu pamoja nao. Kwa nini basi mmejitukuza wenyewe juu ya kusanyiko la Bwana?”
و به مقابل موسی و هارون جمع شده، به ایشان گفتند: «شما از حد خود تجاوز می‌نمایید، زیرا تمامی جماعت هریک از ایشان مقدس‌اند، و خداوند درمیان ایشان است. پس چرا خویشتن را بر جماعت خداوند برمی افرازید؟»۳
4 Mose aliposikia jambo hili, akaanguka kifudifudi.
و چون موسی این راشنید به روی خود درافتاد.۴
5 Kisha akamwambia Kora na wafuasi wake wote: “Asubuhi Bwana ataonyesha ni nani aliye wake na ni nani aliye mtakatifu, tena atamtaka mtu huyo aje kwake. Mtu yule ambaye atamchagua atamfanya kuja karibu naye.
و قورح و تمامی جمعیت او را خطاب کرده، گفت: «بامدادان خداوند نشان خواهد داد که چه کس از آن وی وچه کس مقدس است، و او را نزد خود خواهدآورد، و هرکه را برای خود برگزیده است، او رانزد خود خواهد آورد.۵
6 Wewe Kora na wafuasi wako wote mtafanya hivi: Chukueni vyetezo,
این را بکنید که مجمرهابرای خود بگیرید، ای قورح و تمامی جمعیت تو.۶
7 kesho wekeni moto na uvumba kwenye hivyo vyetezo mbele za Bwana. Mtu ambaye Bwana atamchagua atakuwa ndiye mtakatifu. Ninyi Walawi mmejitukuza sana!”
و آتش در آنها گذارده، فردا به حضورخداوند بخور در آنها بریزید، و آن کس که خداوند برگزیده است، مقدس خواهد شد. ای پسران لاوی شما از حد خود تجاوز می‌نمایید!»۷
8 Pia Mose akamwambia Kora, “Enyi Walawi! Sasa nisikilizeni.
و موسی به قورح گفت: «ای بنی لاوی بشنوید!۸
9 Haiwatoshi ninyi kwamba Mungu wa Israeli amewateua ninyi kutoka kusanyiko lote la Kiisraeli, na kuwaleta karibu naye mpate kufanya kazi kwenye Maskani ya Bwana, na kusimama mbele ya kusanyiko ili kuwahudumia?
آیا نزد شما کم است که خدای اسرائیل شما رااز جماعت اسرائیل ممتاز کرده است، تا شما رانزد خود بیاورد تا در مسکن خداوندخدمت نمایید، و به حضور جماعت برای خدمت ایشان بایستید؟۹
10 Amekuleta wewe na ndugu zako Walawi mwe karibu naye, lakini sasa unajaribu kupata na ukuhani pia.
و تو را و جمیع برادرانت بنی لاوی رابا تو نزدیک آورد، و آیا کهانت را نیز می‌طلبید؟۱۰
11 Wewe na wafuasi wako wote mmekusanyika pamoja kinyume cha Bwana. Aroni ni nani kwamba ninyi mnungʼunike dhidi yake?”
از این جهت تو و تمامی جمعیت تو به ضدخداوند جمع شده‌اید، و اما هارون چیست که براو همهمه می‌کنید؟»۱۱
12 Kisha Mose akawaita Dathani na Abiramu, wana wa Eliabu. Lakini wao wakasema, “Sisi hatuji!
و موسی فرستاد تا داتان و ابیرام پسران الیاب را بخواند، و ایشان گفتند: «نمی آییم!۱۲
13 Haitoshi tu kwamba wewe umetuleta kutoka nchi itiririkayo maziwa na asali ili kutuua sisi jangwani? Nawe sasa pia unataka kuwa mkuu juu yetu?
آیاکم است که ما را از زمینی که به شیر و شهد جاری است، بیرون آوردی تا ما را در صحرا نیز هلاک سازی که می‌خواهی خود را بر ما حکمران سازی؟۱۳
14 Zaidi ya hayo, hujatuingiza katika nchi inayotiririka maziwa na asali, wala hujatupa urithi wa mashamba na mashamba ya mizabibu. Je, utayangʼoa macho ya watu hawa? Hapana, sisi hatuji!”
و ما را هم به زمینی که به شیر و شهدجاری است درنیاوردی و ملکیتی از مزرعه‌ها وتاکستانها به ما ندادی. آیا چشمان این مردمان رامی کنی؟ نخواهیم آمد!»۱۴
15 Ndipo Mose akakasirika sana na kumwambia Bwana, “Usiikubali sadaka yao. Mimi sikuchukua chochote, hata punda kutoka kwao, wala sijamkosea hata mmoja wao.”
و موسی بسیار خشمناک شده، به خداوندگفت: «هدیه ایشان را منظور منما، یک خر ازایشان نگرفتم، و به یکی از ایشان زیان نرساندم.»۱۵
16 Mose akamwambia Kora, “Wewe na wafuasi wako wote kesho mtatokea mbele za Bwana: yaani wewe na hao wenzako, pamoja na Aroni.
و موسی به قورح گفت: «تو با تمامی جمعیت خود فردا به حضور خداوند حاضر شوید، تو وایشان و هارون.۱۶
17 Kila mtu atachukua chetezo chake na kuweka uvumba ndani yake, vyetezo 250 kwa jumla, na kukileta mbele za Bwana. Wewe na Aroni mtaleta vyetezo vyenu pia.”
و هر کس مجمر خود راگرفته، بخور بر آنها بگذارد و شما هر کس مجمرخود، یعنی دویست و پنجاه مجمر به حضورخداوند بیاورید، تو نیز و هارون هر یک مجمرخود را بیاورید.»۱۷
18 Kwa hiyo kila mtu akachukua chetezo chake, akaweka moto na uvumba ndani yake, na kusimama pamoja na Mose na Aroni kwenye mlango wa Hema la Kukutania.
پس هر کس مجمر خود راگرفته، و آتش در آنها نهاده، و بخور بر آنهاگذارده، نزد دروازه خیمه اجتماع، با موسی وهارون ایستادند.۱۸
19 Kora alipokuwa amekusanya wafuasi wake wote kuwapinga Mose na Aroni kwenye mlango wa Hema la Kukutania, utukufu wa Bwana ukatokea kwa kusanyiko lote.
و قورح تمامی جماعت را به مقابل ایشان نزد در خیمه اجتماع جمع کرد، وجلال خداوند بر تمامی جماعت ظاهرشد.۱۹
20 Bwana akamwambia Mose na Aroni,
و خداوند موسی و هارون را خطاب کرده، گفت:۲۰
21 “Jitengeni kutoka kwenye kusanyiko hili ili nipate kuwaangamiza mara moja.”
«خود را از این جماعت دور کنید تاایشان را در لحظه‌ای هلاک کنم.»۲۱
22 Lakini Mose na Aroni wakaanguka kufudifudi na kulia kwa sauti, wakasema, “Ee Mungu, Mungu wa roho za wanadamu wote, utakuwa na hasira na kusanyiko lote wakati ni mtu mmoja tu ametenda dhambi?”
پس ایشان به روی در‌افتاده، گفتند: «ای خدا که خدای روحهای تمام بشر هستی، آیا یک نفر گناه ورزد وبر تمام جماعت غضبناک شوی؟»۲۲
23 Ndipo Bwana akamwambia Mose,
و خداوند موسی را خطاب کرده، گفت:۲۳
24 “Liambie kusanyiko, ‘Ondokeni hapo karibu na mahema ya Kora, Dathani na Abiramu.’”
«جماعت را خطاب کرده، بگو از اطراف مسکن قورح و داتان و ابیرام دور شوید.»۲۴
25 Mose akainuka na kuwaendea Dathani na Abiramu, nao wazee wa Israeli wakafuatana naye.
پس موسی برخاسته، نزد داتان و ابیرام رفت و مشایخ اسرائیل در عقب وی رفتند.۲۵
26 Mose akalionya kusanyiko, “Sogeeni nyuma mbali na mahema ya hawa watu waovu! Msiguse kitu chochote kilicho mali yao, la sivyo mtafagiliwa mbali kwa sababu ya dhambi zao zote.”
و جماعت راخطاب کرده، گفت: «از نزد خیمه های این مردمان شریر دور شوید، و چیزی را که از آن ایشان است لمس منمایید، مبادا در همه گناهان ایشان هلاک شوید.»۲۶
27 Hivyo wakaondoka karibu na mahema ya Kora, Dathani na Abiramu. Dathani na Abiramu walikuwa wametoka nje, nao walikuwa wamesimama pamoja na wake zao, watoto wao na wale wanyonyao kwenye mlango wa mahema yao.
پس از اطراف مسکن قورح و داتان وابیرام دور شدند، و داتان و ابیرام بیرون آمده، بازنان و پسران و اطفال خود به در خیمه های خودایستادند.۲۷
28 Ndipo Mose akasema, “Hivi ndivyo mtakavyojua kuwa Bwana amenituma kufanya mambo haya, na kwamba halikuwa wazo langu.
و موسی گفت: «از این خواهیددانست که خداوند مرا فرستاده است تا همه این کارها را بکنم و به اراده من نبوده است.۲۸
29 Ikiwa watu hawa watakufa kifo cha kawaida na kupatwa na yale ya kawaida yanayowapata wanadamu, basi Bwana hakunituma mimi.
اگر این کسان مثل موت سایر بنی آدم بمیرند و اگر مثل وقایع جمیع بنی آدم بر ایشان واقع شود، خداوندمرا نفرستاده است.۲۹
30 Lakini ikiwa Bwana ataleta jambo jipya kabisa, ardhi ikifunua kinywa chake na kuwameza wao, pamoja na kila kitu kilicho mali yao, nao washuke chini kaburini wakiwa hai, ndipo mtafahamu kuwa watu hawa wamemdharau Bwana.” (Sheol h7585)
و اما اگر خداوند چیزتازه‌ای بنماید و زمین دهان خود را گشاده، ایشان را با جمیع مایملک ایشان ببلعد که به گور زنده فرود روند، آنگاه بدانید که این مردمان خداوند رااهانت نموده‌اند.» (Sheol h7585)۳۰
31 Mara Mose alipomaliza kusema haya yote, ardhi iliyokuwa chini yao ikapasuka,
و چون از گفتن همه این سخنان فارغ شد، زمینی که زیر ایشان بود، شکافته شد.۳۱
32 nchi ikafunua kinywa chake na kuwameza wao, pamoja na jamaa zao, na watu wote wa Kora na mali zao zote.
و زمین دهان خود را گشوده، ایشان را و خانه های ایشان و همه کسان را که تعلق به قورح داشتند، با تمامی اموال ایشان بلعید.۳۲
33 Wakashuka chini kaburini wakiwa hai, pamoja na kila kitu walichokuwa nacho; nchi ikajifunika juu yao, nao wakaangamia wakatoweka kutoka kusanyiko. (Sheol h7585)
و ایشان با هرچه به ایشان تعلق داشت، زنده به گور فرورفتند، و زمین برایشان به هم آمد که از میان جماعت هلاک شدند. (Sheol h7585)۳۳
34 Kutoka kilio chao, Waisraeli wote waliowazunguka walikimbia, wakipaza sauti, “Nchi inatumeza na sisi pia!”
و جمیع اسرائیلیان که به اطراف ایشان بودند، از نعره ایشان گریختند، زیرا گفتند مبادا زمین ما رانیز ببلعد.۳۴
35 Moto ukaja kutoka kwa Bwana, ukawateketeza wale watu 250 waliokuwa wakifukiza uvumba.
و آتش از حضور خداوند بدر‌آمده، دویست و پنجاه نفر را که بخور می‌گذرانیدند، سوزانید.۳۵
36 Bwana akamwambia Mose,
و خداوند موسی را خطاب کرده، گفت:۳۶
37 “Mwambie Eleazari mwana wa kuhani Aroni, atoe vyetezo kwenye mabaki ya moto na kutawanya makaa mbali kiasi, kwa maana vyetezo ni vitakatifu:
«به العازار بن هارون کاهن بگو که مجمرها را ازمیان آتش بردار، و آتش را به آن طرف بپاش زیراکه آنها مقدس است.۳۷
38 vyetezo vya watu waliofanya dhambi iliyowagharimu maisha yao. Fua vyetezo hivyo kuwa bamba ili kufunika madhabahu, kwa maana vimeletwa mbele za Bwana na vimekuwa vitakatifu. Navyo viwe ishara kwa Waisraeli.”
یعنی مجمرهای این گناهکاران را به ضد جان ایشان و از آنها تختهای پهن برای پوشش مذبح بسازند، زیرا چونکه آنهارا به حضور خداوند گذرانیده‌اند مقدس شده است، تا برای بنی‌اسرائیل آیتی باشد.»۳۸
39 Hivyo kuhani Eleazari akavikusanya vile vyetezo vya shaba vilivyoletwa na wale waliokuwa wameteketezwa kwa moto, naye akavifua kufunika madhabahu,
پس العازار کاهن مجمرهای برنجین را که سوخته شدگان گذرانیده بودند گرفته، از آنها پوشش مذبح ساختند.۳۹
40 kama vile Bwana alivyomwelekeza kupitia Mose. Hili lilikuwa kuwakumbusha Waisraeli kwamba hakuna mtu hata mmoja, isipokuwa mzao wa Aroni, awezaye kuja kufukiza uvumba mbele za Bwana, la sivyo, angekuwa kama Kora na wafuasi wake.
تا برای بنی‌اسرائیل یادگارباشد تا هیچ غریبی که از اولاد هارون نباشدبجهت سوزانیدن بخور به حضور خداوند نزدیک نیاید، مبادا مثل قورح و جمعیتش بشود، چنانکه خداوند به واسطه موسی او را امر فرموده بود.۴۰
41 Siku iliyofuata jumuiya yote ya Kiisraeli wakanungʼunika dhidi ya Mose na Aroni, wakisema, “Mmewaua watu wa Bwana.”
و در فردای آن روز تمامی جماعت بنی‌اسرائیل بر موسی و هارون همهمه کرده، گفتند که شما قوم خداوند را کشتید.۴۱
42 Lakini wakati kusanyiko lilipokusanyika kupingana na Mose na Aroni, nalo likageuka kuelekea Hema la Kukutania, ghafula wingu likafunika Hema, nao utukufu wa Bwana ukatokea.
و چون جماعت بر موسی و هارون جمع شدند، به سوی خیمه اجتماع نگریستند، و اینک ابر آن راپوشانید و جلال خداوند ظاهر شد.۴۲
43 Ndipo Mose na Aroni wakaenda mbele ya Hema la Kukutania,
و موسی وهارون پیش خیمه اجتماع آمدند.۴۳
44 naye Bwana akamwambia Mose,
و خداوندموسی را خطاب کرده، گفت:۴۴
45 “Jitenge mbali na kusanyiko hili ili niweze kuwaangamiza mara moja.” Wakaanguka chini kifudifudi.
«از میان این جماعت دور شوید تا ایشان را ناگهان هلاک سازم.» و ایشان به روی خود درافتادند.۴۵
46 Kisha Mose akamwambia Aroni, “Chukua chetezo chako na uweke uvumba ndani yake, pamoja na moto kutoka madhabahuni, nawe uende haraka kwenye kusanyiko ili kufanya upatanisho kwa ajili yao. Ghadhabu imekuja kutoka kwa Bwana, na tauni imeanza.”
و موسی به هارون گفت: «مجمر خود راگرفته، آتش از روی مذبح در آن بگذار، و بخور برآن بریز، و به زودی به سوی جماعت رفته، برای ایشان کفاره کن، زیرا غضب از حضور خداوندبرآمده، و وبا شروع شده است.»۴۶
47 Hivyo Aroni akafanya kama Mose alivyosema, akakimbilia katikati ya kusanyiko. Tauni ilikuwa tayari imeanza miongoni mwa watu, lakini Aroni akafukiza uvumba na kufanya upatanisho kwa ajili yao.
پس هارون به نحوی که موسی گفته بود آن را گرفته، در میان جماعت دوید و اینک وبا در میان قوم شروع شده بود، پس بخور را بریخت و بجهت قوم کفاره نمود.۴۷
48 Aroni akasimama kati ya waliokuwa hai na waliokufa, nayo tauni ikakoma.
و او در میان مردگان و زندگان ایستاد ووبا بازداشته شد.۴۸
49 Lakini walikufa watu 14,700 kutokana na tauni hiyo, licha ya wale waliokuwa wamekufa kwa sababu ya Kora.
و عدد کسانی که از وبا مردندچهارده هزار و هفتصد بود، سوای آنانی که درحادثه قورح هلاک شدند.۴۹
50 Ndipo Aroni akamrudia Mose kwenye mlango wa Hema la Kukutania, kwa maana tauni ilikuwa imekoma.
پس هارون نزدموسی به در خیمه اجتماع برگشت و وبا رفع شد.۵۰

< Hesabu 16 >