< Hesabu 15 >

1 Bwana akamwambia Mose,
And the LORD spoke to Moses, saying,
2 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Baada ya ninyi kuingia katika nchi ninayowapa kama nyumbani,
Speak to the children of Israel, and say to them, When ye shall have come into the land of your habitations, which I give to you,
3 nanyi mkitoa sadaka za kuteketezwa kwa moto, kutoka makundi ya ngʼombe au kondoo, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana, ikiwa ni sadaka za kuteketezwa au dhabihu, kwa ajili ya nadhiri maalum ama sadaka ya hiari au sadaka ya sikukuu zenu,
And will make an offering by fire to the LORD, a burnt-offering, or a sacrifice in performing a vow, or in a free-will-offering, or in your solemn feasts, to make a sweet savor to the LORD, of the herd, or of the flock:
4 ndipo yeye aletaye sadaka yake ataiweka mbele za Bwana sadaka ya nafaka, sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta.
Then shall he that offereth his offering to the LORD bring a meat-offering of a tenth part of flour mingled with the fourth [part] of a hin of oil.
5 Pamoja na kila mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa au dhabihu, andaa robo ya hini ya divai kwa sadaka ya kinywaji.
And the fourth [part] of a hin of wine for a drink-offering shalt thou prepare with the burnt-offering or sacrifice, for one lamb.
6 “‘Pamoja na kondoo dume andaa sadaka ya nafaka ya sehemu mbili za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na theluthi moja ya hini ya mafuta,
Or for a ram, thou shalt prepare [for] a meat-offering two tenth parts of flour mingled with the third [part] of a hin of oil.
7 na theluthi moja ya hini ya divai kama sadaka ya kinywaji. Vitoe kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
And for a drink-offering thou shalt offer the third [part] of a hin of wine, [for] a sweet savor to the LORD.
8 “‘Unapoandaa fahali mchanga kama sadaka ya kuteketezwa au dhabihu, kwa ajili ya nadhiri maalum au sadaka ya amani kwa Bwana,
And when thou preparest a bullock [for] a burnt-offering, or [for] a sacrifice in performing a vow, or peace-offerings to the LORD:
9 leta pamoja na huyo fahali sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa uliochanganywa na nusu ya hini ya mafuta.
Then shall he bring with a bullock a meat-offering of three tenth parts of flour mingled with half a hin of oil.
10 Pia utaleta nusu ya hini ya divai kama sadaka ya kinywaji. Itakuwa sadaka iliyoteketezwa kwa moto, harufu nzuri inayompendeza Bwana.
And thou shalt bring for a drink-offering half a hin of wine, [for] an offering made by fire, of a sweet savor to the LORD:
11 Kila fahali au kondoo dume, kila mwana-kondoo au mbuzi mchanga, atatayarishwa kwa njia hii.
Thus shall it be done for one bullock, or for one ram, or for a lamb, or a kid.
12 Fanyeni hivi kwa ajili ya kila mmoja, kwa kadiri ya wingi wa mtakavyoandaa.
According to the number that ye shall prepare, so shall ye do to every one according to their number.
13 “‘Kila mmoja ambaye ni mzawa ni lazima afanye vitu hivi kwa njia hii hapo aletapo sadaka ya kuteketezwa kwa moto kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
All that are born in the country shall do these things after this manner, in offering an offering made by fire, of a sweet savor to the LORD.
14 Kwa vizazi vijavyo, wakati wowote mgeni au mtu mwingine yeyote anayeishi miongoni mwenu aletapo sadaka ya kuteketezwa kuwa harufu nzuri ya kumpendeza Bwana, ni lazima afanye sawasawa kabisa na jinsi mnavyofanya ninyi.
And if a stranger shall sojourn with you, or whoever shall [be] among you in your generations, and will offer an offering made by fire, of a sweet savor to the LORD; as ye do, so he shall do.
15 Jumuiya itakuwa na sheria hizo hizo kwenu na kwa mgeni aishiye miongoni mwenu; hii ni amri ya kudumu kwa vizazi vijavyo. Ninyi na mgeni mtakuwa sawa mbele za Bwana:
One ordinance [shall be both] for you of the congregation, and also for the stranger that sojourneth [with you], an ordinance for ever in your generations: as ye [are], so shall the stranger be before the LORD.
16 Sheria hizo hizo na masharti hayo hayo hayo, yatawahusu ninyi na mgeni aishiye miongoni mwenu.’”
One law and one manner shall be for you, and for the stranger that sojourneth with you.
17 Bwana akamwambia Mose,
And the LORD spoke to Moses, saying,
18 “Sema na Waisraeli na uwaambie: ‘Mtakapoingia katika nchi ninayowapeleka
Speak to the children of Israel, and say to them, When ye come into the land whither I bring you,
19 nanyi mkala chakula cha nchi hiyo, toeni sehemu ya chakula hicho kama sadaka kwa Bwana.
Then it shall be, that when ye eat of the bread of the land, ye shall offer up a heave-offering to the LORD.
20 Toeni andazi kutoka kwa malimbuko ya chakula chenu kitokacho katika ardhi, na mkitoe kama sadaka kutoka sakafu ya kupuria nafaka.
Ye shall offer a cake of the first of your dough [for] a heave-offering: as [ye do] the heave-offering of the threshing-floor, so shall ye heave it.
21 Kwa vizazi vyote vijavyo hamna budi kutoa sadaka hii kwa Bwana kutoka kwa malimbuko ya unga wenu.
Of the first of your dough ye shall give to the LORD a heave-offering in your generations.
22 “‘Basi kama pasipo kukusudia umeshindwa kushika mojawapo katika amri hizi ambazo Bwana alimpa Mose,
And if ye have erred, and not observed all these commandments which the LORD hath spoken to Moses,
23 amri yoyote ya Bwana kwenu kupitia Mose, tangu siku ile Bwana alipowapa na inaendelea hadi vizazi vyote vijavyo;
[Even] all that the LORD hath commanded you by the hand of Moses, from the day that the LORD commanded [Moses], and henceforward among your generations;
24 ikiwa hili limefanyika pasipo kukusudia bila jumuiya kuwa na habari nalo, basi jumuiya yote itatoa fahali mchanga kuwa sadaka ya kuteketezwa ikiwa harufu nzuri inayompendeza Bwana, pamoja na sadaka ya nafaka na ya kinywaji zilizoamriwa kwayo, na mbuzi dume kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
Then it shall be, if [aught] shall be committed by ignorance without the knowledge of the congregation, that all the congregation shall offer one young bullock for a burnt-offering, for a sweet savor to the LORD, with his meat-offering, and his drink-offering, according to the manner, and one kid of the goats for a sin-offering.
25 Kuhani atafanya upatanisho kwa ajili ya jumuiya yote ya Kiisraeli, nao watasamehewa, kwa kuwa haikuwa makusudi nao wamemletea Bwana sadaka iliyoteketezwa kwa moto na sadaka ya dhambi kwa ajili ya kosa lao.
And the priest shall make an atonement for all the congregation of the children of Israel, and it shall be forgiven them; for it [is] ignorance: and they shall bring their offering, a sacrifice made by fire to the LORD, and their sin-offering before the LORD, for their ignorance:
26 Jumuiya yote ya Kiisraeli pamoja na wageni waishio miongoni mwao watasamehewa, kwa sababu watu wote walihusika katika kosa lile lisilokusudiwa.
And it shall be forgiven all the congregation of the children of Israel, and the stranger that sojourneth among them; seeing all the people [were] in ignorance.
27 “‘Lakini kama mtu mmoja peke yake akitenda dhambi pasipo kukusudia, ni lazima alete mbuzi mke wa mwaka mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
And if any soul shall sin through ignorance, then he shall bring a she-goat of the first year for a sin-offering.
28 Kuhani atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya yule aliyekosa kwa kufanya dhambi pasipo kukusudia, upatanisho utakapofanywa kwa ajili yake, atasamehewa.
And the priest shall make an atonement for the soul that sinneth ignorantly, when he sinneth by ignorance before the LORD, to make an atonement for him; and it shall be forgiven him.
29 Sheria hiyo moja itamhusu kila mmoja ambaye ametenda dhambi pasipo kukusudia, awe Mwisraeli mzawa ama mgeni.
Ye shall have one law for him that sinneth through ignorance, [both for] him that is born among the children of Israel, and for the stranger that sojourneth among them.
30 “‘Lakini yeyote ambaye amefanya dhambi kwa dharau awe mzawa au mgeni, anamkufuru Bwana, naye mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.
But the soul that doeth [aught] presumptuously, [whether he be] born in the land, or a stranger, the same reproacheth the LORD; and that soul shall be cut off from among his people.
31 Kwa sababu amelidharau neno la Bwana na kuvunja amri zake, mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali; hatia yake inabaki juu yake.’”
Because he hath despised the word of the LORD, and hath broken his commandment, that soul shall utterly be cut off; his iniquity [shall be] upon him.
32 Waisraeli walipokuwa jangwani, mtu mmoja alikutwa akikusanya kuni siku ya Sabato.
And while the children of Israel were in the wilderness, they found a man that gathered sticks upon the sabbath-day.
33 Wale waliomkuta akikusanya kuni wakamleta kwa Mose, Aroni na kusanyiko lote,
And they that found him gathering sticks brought him to Moses and Aaron, and to all the congregation.
34 nao wakamweka kifungoni, kwa sababu haikufahamika kwa wazi kwamba afanyiwe nini.
And they put him in custody, because it was not declared what should be done to him.
35 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Huyo mtu ni lazima afe. Kusanyiko lote lazima limpige mawe nje ya kambi.”
And the LORD said to Moses, The man shall surely be put to death: all the congregation shall stone him with stones without the camp.
36 Hivyo kusanyiko likamtoa nje ya kambi na kumpiga mawe hadi akafa, kama Bwana alivyomwamuru Mose.
And all the congregation brought him without the camp, and stoned him with stones, and he died; as the LORD commanded Moses.
37 Bwana akamwambia Mose,
And the LORD spoke to Moses, saying,
38 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Kwa vizazi vyote vijavyo jifanyieni vifundo katika pindo za mavazi yenu vikiwa na uzi wa buluu kwenye kila kifundo.
Speak to the children of Israel, and bid them that they make them fringes on the borders of their garments throughout their generations, and that they put upon the fringe of the borders a ribin of blue:
39 Mtakuwa mkivitazama vifundo hivyo ili mpate kukumbuka amri zote za Bwana, ili mpate kuzitii msije mkajitia uzinzi wenyewe kwa kuzifuata tamaa za mioyo yenu na za macho yenu.
And it shall be to you for a fringe, that ye may look upon it, and remember all the commandments of the LORD, and do them; and that ye seek not after your own heart and your own eyes, after which ye use to go astray:
40 Ndipo mtakumbuka kuzitii amri zangu zote nanyi mtawekwa wakfu kwa Mungu wenu.
That ye may remember, and do all my commandments, and be holy to your God.
41 Mimi Ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewatoa Misri niwe Mungu wenu. Mimi Ndimi Bwana Mungu wenu.’”
I [am] the LORD your God, who brought you out of the land of Egypt, to be your God: I [am] the LORD your God.

< Hesabu 15 >