< Hesabu 15 >

1 Bwana akamwambia Mose,
The LORD spoke to Moses, saying,
2 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Baada ya ninyi kuingia katika nchi ninayowapa kama nyumbani,
"Speak to the children of Israel, and tell them, 'When you have come into the land of your habitations, which I give to you,
3 nanyi mkitoa sadaka za kuteketezwa kwa moto, kutoka makundi ya ngʼombe au kondoo, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana, ikiwa ni sadaka za kuteketezwa au dhabihu, kwa ajili ya nadhiri maalum ama sadaka ya hiari au sadaka ya sikukuu zenu,
and will make an offering by fire to the LORD, a burnt offering, or a sacrifice, to accomplish a vow, or as a freewill offering, or in your set feasts, to make a pleasant aroma to the LORD, of the herd, or of the flock;
4 ndipo yeye aletaye sadaka yake ataiweka mbele za Bwana sadaka ya nafaka, sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta.
then he who offers his offering shall offer to the LORD a meal offering of a tenth part of an ephah of fine flour mixed with the fourth part of a hin of oil:
5 Pamoja na kila mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa au dhabihu, andaa robo ya hini ya divai kwa sadaka ya kinywaji.
and wine for the drink offering, the fourth part of a hin, you shall prepare with the burnt offering, or for the sacrifice, for each lamb.
6 “‘Pamoja na kondoo dume andaa sadaka ya nafaka ya sehemu mbili za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na theluthi moja ya hini ya mafuta,
"'Or for a ram, you shall prepare for a meal offering two tenth parts of an ephah of fine flour mixed with the third part of a hin of oil:
7 na theluthi moja ya hini ya divai kama sadaka ya kinywaji. Vitoe kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
and for the drink offering you shall offer the third part of a hin of wine, of a pleasant aroma to the LORD.
8 “‘Unapoandaa fahali mchanga kama sadaka ya kuteketezwa au dhabihu, kwa ajili ya nadhiri maalum au sadaka ya amani kwa Bwana,
When you prepare a bull for a burnt offering, or for a sacrifice, to accomplish a vow, or for peace offerings to the LORD;
9 leta pamoja na huyo fahali sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa uliochanganywa na nusu ya hini ya mafuta.
then shall he offer with the bull a meal offering of three tenth parts of an ephah of fine flour mixed with half a hin of oil:
10 Pia utaleta nusu ya hini ya divai kama sadaka ya kinywaji. Itakuwa sadaka iliyoteketezwa kwa moto, harufu nzuri inayompendeza Bwana.
and you shall offer for the drink offering half a hin of wine, for an offering made by fire, of a pleasant aroma to the LORD.
11 Kila fahali au kondoo dume, kila mwana-kondoo au mbuzi mchanga, atatayarishwa kwa njia hii.
Thus shall it be done for each bull, or for each ram, or for each of the male lambs, or of the young goats.
12 Fanyeni hivi kwa ajili ya kila mmoja, kwa kadiri ya wingi wa mtakavyoandaa.
According to the number that you shall prepare, so you shall do to everyone according to their number.
13 “‘Kila mmoja ambaye ni mzawa ni lazima afanye vitu hivi kwa njia hii hapo aletapo sadaka ya kuteketezwa kwa moto kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
"'All who are native-born shall do these things in this way, in offering an offering made by fire, of a pleasant aroma to the LORD.
14 Kwa vizazi vijavyo, wakati wowote mgeni au mtu mwingine yeyote anayeishi miongoni mwenu aletapo sadaka ya kuteketezwa kuwa harufu nzuri ya kumpendeza Bwana, ni lazima afanye sawasawa kabisa na jinsi mnavyofanya ninyi.
If a stranger lives as a foreigner with you, or whoever may be among you throughout your generations, and will offer an offering made by fire, of a pleasant aroma to the LORD; as you do, so he shall do.
15 Jumuiya itakuwa na sheria hizo hizo kwenu na kwa mgeni aishiye miongoni mwenu; hii ni amri ya kudumu kwa vizazi vijavyo. Ninyi na mgeni mtakuwa sawa mbele za Bwana:
For the assembly, there shall be one statute for you, and for the stranger who lives among you, a statute forever throughout your generations: as you are, so shall the foreigner be before the LORD.
16 Sheria hizo hizo na masharti hayo hayo hayo, yatawahusu ninyi na mgeni aishiye miongoni mwenu.’”
One law and one ordinance shall be for you, and for the stranger who lives as a foreigner with you.'"
17 Bwana akamwambia Mose,
The LORD spoke to Moses, saying,
18 “Sema na Waisraeli na uwaambie: ‘Mtakapoingia katika nchi ninayowapeleka
"Speak to the children of Israel, and tell them, 'When you come into the land where I bring you,
19 nanyi mkala chakula cha nchi hiyo, toeni sehemu ya chakula hicho kama sadaka kwa Bwana.
then it shall be that when you eat of the bread of the land, you shall offer up a wave offering to the LORD.
20 Toeni andazi kutoka kwa malimbuko ya chakula chenu kitokacho katika ardhi, na mkitoe kama sadaka kutoka sakafu ya kupuria nafaka.
Of the first of your dough you shall offer up a cake for a wave offering: as the wave offering of the threshing floor, so you shall heave it.
21 Kwa vizazi vyote vijavyo hamna budi kutoa sadaka hii kwa Bwana kutoka kwa malimbuko ya unga wenu.
Of the first of your dough you shall give to the LORD a wave offering throughout your generations.
22 “‘Basi kama pasipo kukusudia umeshindwa kushika mojawapo katika amri hizi ambazo Bwana alimpa Mose,
"'When you shall err, and not observe all these commandments, which the LORD has spoken to Moses,
23 amri yoyote ya Bwana kwenu kupitia Mose, tangu siku ile Bwana alipowapa na inaendelea hadi vizazi vyote vijavyo;
even all that the LORD has commanded you by Moses, from the day that the LORD gave commandment, and onward throughout your generations;
24 ikiwa hili limefanyika pasipo kukusudia bila jumuiya kuwa na habari nalo, basi jumuiya yote itatoa fahali mchanga kuwa sadaka ya kuteketezwa ikiwa harufu nzuri inayompendeza Bwana, pamoja na sadaka ya nafaka na ya kinywaji zilizoamriwa kwayo, na mbuzi dume kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
then it shall be, if it be done unwittingly, without the knowledge of the congregation, that all the congregation shall offer one young bull for a burnt offering, for a pleasant aroma to the LORD, with the meal offering of it, and the drink offering of it, according to the ordinance, and one male goat for a sin offering.
25 Kuhani atafanya upatanisho kwa ajili ya jumuiya yote ya Kiisraeli, nao watasamehewa, kwa kuwa haikuwa makusudi nao wamemletea Bwana sadaka iliyoteketezwa kwa moto na sadaka ya dhambi kwa ajili ya kosa lao.
The cohen shall make atonement for all the congregation of the children of Israel, and they shall be forgiven; for it was an error, and they have brought their offering, an offering made by fire to the LORD, and their sin offering before the LORD, for their error:
26 Jumuiya yote ya Kiisraeli pamoja na wageni waishio miongoni mwao watasamehewa, kwa sababu watu wote walihusika katika kosa lile lisilokusudiwa.
and all the congregation of the children of Israel shall be forgiven, and the stranger who lives as a foreigner among them; for in respect of all the people it was done unwittingly.
27 “‘Lakini kama mtu mmoja peke yake akitenda dhambi pasipo kukusudia, ni lazima alete mbuzi mke wa mwaka mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
"'If one person sins unwittingly, then he shall offer a female goat a year old for a sin offering.
28 Kuhani atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya yule aliyekosa kwa kufanya dhambi pasipo kukusudia, upatanisho utakapofanywa kwa ajili yake, atasamehewa.
The cohen shall make atonement for the soul who errs, when he sins unwittingly, before the LORD, to make atonement for him; and he shall be forgiven.
29 Sheria hiyo moja itamhusu kila mmoja ambaye ametenda dhambi pasipo kukusudia, awe Mwisraeli mzawa ama mgeni.
You shall have one law for him who does anything unwittingly, for him who is native-born among the children of Israel, and for the stranger who lives as a foreigner among them.
30 “‘Lakini yeyote ambaye amefanya dhambi kwa dharau awe mzawa au mgeni, anamkufuru Bwana, naye mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.
"'But the person who acts defiantly, whether he is native-born or a foreigner, the same blasphemes God, and that person is to be cut off from among his people.
31 Kwa sababu amelidharau neno la Bwana na kuvunja amri zake, mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali; hatia yake inabaki juu yake.’”
Because he has despised the word of the LORD, and has broken his commandment, that soul shall utterly be cut off; his iniquity shall be on him.'"
32 Waisraeli walipokuwa jangwani, mtu mmoja alikutwa akikusanya kuni siku ya Sabato.
While the children of Israel were in the wilderness, they found a man gathering sticks on the Sabbath day.
33 Wale waliomkuta akikusanya kuni wakamleta kwa Mose, Aroni na kusanyiko lote,
Those who found him gathering sticks brought him to Moses and Aaron, and to all the congregation.
34 nao wakamweka kifungoni, kwa sababu haikufahamika kwa wazi kwamba afanyiwe nini.
They put him in custody, because it had not been declared what should be done to him.
35 Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Huyo mtu ni lazima afe. Kusanyiko lote lazima limpige mawe nje ya kambi.”
The LORD said to Moses, "The man shall surely be put to death: all the congregation shall stone him with stones outside of the camp."
36 Hivyo kusanyiko likamtoa nje ya kambi na kumpiga mawe hadi akafa, kama Bwana alivyomwamuru Mose.
All the congregation brought him outside of the camp, and stoned him to death with stones; as the LORD commanded Moses.
37 Bwana akamwambia Mose,
The LORD spoke to Moses, saying,
38 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Kwa vizazi vyote vijavyo jifanyieni vifundo katika pindo za mavazi yenu vikiwa na uzi wa buluu kwenye kila kifundo.
"Speak to the children of Israel, and tell them that they should make themselves fringes in the borders of their garments throughout their generations, and that they put on the fringe of each border a cord of blue:
39 Mtakuwa mkivitazama vifundo hivyo ili mpate kukumbuka amri zote za Bwana, ili mpate kuzitii msije mkajitia uzinzi wenyewe kwa kuzifuata tamaa za mioyo yenu na za macho yenu.
and it shall be to you for a fringe, that you may look on it, and remember all the commandments of the LORD, and do them; and that you not follow after your own heart and your own eyes, after which you use to play the prostitute;
40 Ndipo mtakumbuka kuzitii amri zangu zote nanyi mtawekwa wakfu kwa Mungu wenu.
that you may remember and do all my commandments, and be holy to your God.
41 Mimi Ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewatoa Misri niwe Mungu wenu. Mimi Ndimi Bwana Mungu wenu.’”
I am the LORD your God, who brought you out of the land of Egypt, to be your God: I am the LORD your God."

< Hesabu 15 >