< Hesabu 14 >

1 Usiku ule watu wote wa jumuiya walipaza sauti zao na kulia kwa sauti kuu.
That night, all the Israeli people cried loudly.
2 Waisraeli wote wakanungʼunika dhidi ya Mose na Aroni, nalo kusanyiko lote wakawaambia, “Laiti tungekuwa tumefia humo nchi ya Misri! Au humu kwenye hili jangwa!
The next day they all complained to Aaron and Moses/me. All the men said, “We wish that we had died in Egypt, or in this desert!
3 Kwa nini Bwana anatuleta katika nchi hii ili tufe kwa upanga? Wake zetu na watoto wetu watachukuliwa kama nyara. Je, isingekuwa bora kwetu kurudi Misri?”
Why is Yahweh bringing us to this land, where we men will be killed with swords? And our wives and children will be taken away [to be slaves]. [Instead of going to Canaan]. It would be better for us to return to Egypt!”
4 Wakasemezana wao kwa wao, “Inatupasa kumchagua kiongozi na kurudi Misri.”
Then [some of] them said to each other, “We should choose a leader who will take us back to Egypt!”
5 Ndipo Mose na Aroni wakaanguka kifudifudi mbele ya kusanyiko lote la Kiisraeli lililokusanyika hapo.
Then Aaron and Moses/I bowed down [to pray] in front of all the Israeli people who had gathered there.
6 Yoshua mwana wa Nuni na Kalebu mwana wa Yefune, waliokuwa miongoni mwa watu wale waliokwenda kuipeleleza nchi, wakararua nguo zao,
Joshua and Caleb, two of the men who had explored the land, tore their clothes [because they were very dismayed].
7 wakasema na kusanyiko lote la Kiisraeli, wakawaambia, “Nchi tuliyopita katikati yake na kuipeleleza ni nzuri sana sana.
They said to the Israeli people, “The land that we explored is very good.
8 Ikiwa Bwana anapendezwa nasi, atatuongoza kuingia katika nchi ile, nchi itiririkayo maziwa na asali, naye atatupa nchi hiyo.
If Yahweh is pleased with us, he will lead us into that very fertile [IDM] land, and he will give it to us.
9 Ila tu msimwasi Bwana. Wala msiwaogope watu wa nchi hiyo, kwa sababu tutawameza. Ulinzi wao umeondoka, lakini Bwana yupo pamoja nasi. Msiwaogope.”
So do not rebel against Yahweh! And do not be afraid of the people in that land! We will (gobble them up/completely destroy them) [MET]! They do not have anyone who will protect them, but Yahweh will be with us [and help us]. So do not be afraid of them!”
10 Lakini kusanyiko lote likazungumza juu ya kuwapiga kwa mawe. Ndipo utukufu wa Bwana ukaonekana katika Hema la Kukutania kwa Waisraeli wote.
Then all the Israeli people talked about [killing Caleb and Joshua by] throwing stones at them. But [suddenly] Yahweh’s glory appeared to them at the Sacred Tent.
11 Bwana akamwambia Mose, “Watu hawa watanidharau mpaka lini? Wataendelea kukataa kuniamini mimi mpaka lini, ingawa nimetenda ishara za miujiza miongoni mwao?
Then Yahweh said to Moses/me, “How long will these people reject me [RHQ]? I am tired of them not believing in what I [can do], in spite of all the miracles I have performed among them [RHQ]!
12 Nitawapiga kwa tauni na kuwaangamiza, lakini nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa lenye nguvu kuliko wao.”
So I will cause a (plague/widespread sickness) to strike them and get rid of them. But I will cause your [descendants] to become a great nation. They will be a nation that is much greater and stronger than these people are.”
13 Mose akamwambia Bwana, “Ndipo Wamisri watasikia juu ya jambo hili! Kwa uweza wako uliwapandisha watu hawa kutoka miongoni mwao.
But Moses/I replied to Yahweh, “[Please do not do that, because] the people of Egypt will hear about it! You brought these Israeli people from Egypt by your great power,
14 Nao watawaambia wenyeji wa nchi hii jambo hili. Wao tayari wameshasikia kwamba wewe, Ee Bwana, upo pamoja na watu hawa, na kuwa wewe, Ee Bwana, umeonekana uso kwa uso, nalo wingu lako hukaa juu yao. Tena wewe unawatangulia kwa nguzo ya wingu mchana na kwa nguzo ya moto usiku.
and the people of Egypt will tell that to the [descendants of Canaan] who live in this land. Yahweh, they have already heard about you. They know that you have (been with/helped) these people and that they have seen you face-to-face. They have heard that your cloud is like a huge pillar that stays over them, and by using that cloud you lead them during the day, and the cloud becomes like a fire at night [to give them light].
15 Ikiwa utawaua watu hawa wote mara moja, mataifa ambayo yamesikia taarifa hii kukuhusu wewe watasema,
If you kill these people all at one time, the people-groups who have heard about your [power] will say,
16 ‘Bwana alishindwa kuwaingiza watu hawa katika nchi aliyowaahidi kwa kiapo; hivyo akawaua jangwani.’
‘Yahweh was not able to bring them into the land that he promised to give to them, so he killed them in the desert.’
17 “Basi sasa nguvu za Bwana na zionekane, sawasawa na vile ulivyosema:
“So Yahweh, now show that you are very powerful. You said,
18 ‘Bwana si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa upendo na mwenye kusamehe dhambi na uasi. Lakini haachi kumwadhibu mwenye hatia, huadhibu watoto kwa ajili ya dhambi ya baba zao hata kizazi cha tatu na cha nne.’
‘I do not quickly become angry; instead, I love people very much, and I forgive people for having sinned and having disobeyed my laws. But I will always punish [LIT] people who are guilty of doing what is wrong. When parents sin, I will punish them, but I will also punish their children and their grandchildren and their great-grandchildren and their great-great-grandchildren.’
19 Kwa kadiri ya upendo wako mkuu, usamehe dhambi ya watu hawa, kama vile ulivyowasamehe tangu wakati walitoka Misri mpaka sasa.”
So, because you love people like that, forgive these people for the sins that they have committed, just like you have continued to forgive them ever since they left Egypt.”
20 Bwana akajibu, “Nimewasamehe kama ulivyoomba.
Then Yahweh replied, “I have forgiven them, as you requested me to.
21 Hata hivyo, kwa hakika kama niishivyo, na kwa hakika kama utukufu wa Bwana uijazavyo dunia yote,
But, just as certainly as I live and that people all over the world [can see] my (glory/glorious power), [I solemnly declare this: ]
22 hakuna hata mmoja wa watu hawa ambao waliuona utukufu wangu na ishara za miujiza niliyotenda huko Misri na huko jangwani, lakini ambaye hakunitii na akanijaribu mara hizi kumi,
All these people saw my glory and all the miracles that I performed in Egypt and in the desert, but they disobeyed me, and many times they tested [whether they could continue to do evil things without my punishing them].
23 hakuna hata mmoja wao atakayeona nchi niliyowaahidi baba zao kwa kiapo. Hakuna hata mmoja ambaye amenidharau atakayeiona.
Because of that, not one of them will see the land that I promised their ancestors [that I would give to them]. No one who rejected me will see that land.
24 Lakini kwa sababu mtumishi wangu Kalebu ana roho ya tofauti na ananifuata kwa moyo wote, nitamwingiza katika nchi aliyoiendea, nao wazao wake watairithi.
But Caleb, who serves me [well], is different from the others. He obeys me completely. So I will bring him into that land that he has already seen, and his descendants will inherit/possess some of it.
25 Kwa kuwa Waamaleki na Wakanaani wanaishi katika mabonde, kesho geukeni mwelekee jangwani kwa kufuata njia iendayo Bahari ya Shamu.”
So, since the descendants of Amalek and Canaan who are living in the valleys [in Canaan are very strong], when you leave here tomorrow, [instead of traveling toward Canaan], go back along the road through the desert towards the Red Sea.”
26 Bwana akamwambia Mose na Aroni:
Then Yahweh said to Aaron and Moses/me,
27 “Jumuiya hii ovu itanungʼunika dhidi yangu hadi lini? Nimesikia malalamiko ya hawa Waisraeli wanaonungʼunika.
“How long will the wicked people of this nation keep complaining about me [RHQ]? I have heard everything that they have grumbled/complained against me.
28 Hivyo waambie, ‘Hakika kama niishivyo, asema Bwana, nitawafanyia vitu vilevile nilivyosikia mkisema:
So now tell them this: ‘Just as certainly as I, Yahweh, live, I will do exactly what you said would happen.
29 Kila mmoja wenu mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi ambaye alihesabiwa na amenungʼunika dhidi yangu, miili yenu itaanguka katika jangwa hili.
[I will cause] all of you to die here in this desert! Because you grumbled about me, none of you who are more than 20 years old and who were counted when Moses counted everyone
30 Hakuna hata mmoja wenu atakayeingia katika nchi niliyoapa kwa mkono ulioinuliwa kuwa makao yenu, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune, na Yoshua mwana wa Nuni.
will enter the land that I solemnly promised to give to you. Only Caleb and Joshua will enter that land.
31 Lakini watoto wenu ambao mlisema watachukuliwa kama mateka, nitawaingiza humo ili waifurahie nchi ambayo ninyi mmeikataa.
You said that your children would be taken from you [to become slaves], but I will take them into the land, and they will enjoy living in the land that you (rejected/said that you could not conquer).
32 Lakini ninyi, miili yenu itaanguka katika jangwa hili.
But as for you [adults], you will die here in this desert.
33 Watoto wenu watakuwa wachungaji wa mifugo hapa kwa miaka arobaini, wakiteseka kwa ajili ya kukosa uaminifu kwenu, hadi mwili wa mtu wenu wa mwisho ulale katika jangwa hili.
And like shepherds [wander around in the desert as they take care of their sheep], your children will wander around in this desert for 40 years. Because you adults were not loyal/faithful to me, your children will suffer until you all die in the desert.
34 Kwa miaka arobaini, mwaka mmoja kwa kila siku katika zile siku arobaini mlizoipeleleza nchi, mtateseka kwa ajili ya dhambi zenu, na kujua jinsi ilivyo vibaya kunifanya mimi kuwa adui yenu.’
You will suffer for your sins for 40 years. That will be one year for each of the 40 days that the twelve men explored Canaan land. And I will be like an enemy to you.’
35 Mimi Bwana nimesema, na hakika nitafanya mambo haya kwa jumuiya hii yote ovu, ambayo imefungamana pamoja dhidi yangu. Watakutana na mwisho wao katika jangwa hili; hapa ndipo watafia.”
[This will certainly happen because] I, Yahweh, have said it! I will do these things to every one in this group who conspired against me. They (conspired against/decided together to reject) me here in the desert, and they will all die right here in this desert!”
36 Hivyo watu wale ambao Mose alikuwa amewatuma kuipeleleza nchi, waliorudi na kuifanya jumuiya nzima kunungʼunika dhidi ya Mose kwa kueneza taarifa mbaya kuhusu hiyo nchi:
Then the ten men [who had explored Canaan and] who had urged the people to rebel against Yahweh by giving reports that discouraged the people
37 watu hawa waliohusika kueneza taarifa mbaya kuhusu hiyo nchi walipigwa na kuanguka kwa tauni mbele za Bwana.
were immediately struck with a plague/disease that Yahweh sent, and they died.
38 Miongoni mwa watu waliokwenda kuipeleleza hiyo nchi, ni Yoshua mwana wa Nuni, na Kalebu mwana wa Yefune peke yao waliosalia.
Of the twelve men who had explored Canaan, only Joshua and Caleb remained alive.
39 Mose alipotoa taarifa hii kwa Waisraeli wote, waliomboleza kwa uchungu.
When Moses/I reported to the Israeli people what Yahweh had said, many of them were very sad.
40 Mapema asubuhi siku iliyofuata walipanda juu kuelekea kwenye nchi ya vilima virefu, wakasema, “Tumetenda dhambi. Tutakwea mpaka mahali Bwana alipotuahidi.”
So the people got up early the next morning and started to go toward the hilly area in Canaan. They said, “[We know that] we have sinned, but now we [are ready to] enter the land that Yahweh promised to give to us.”
41 Lakini Mose akasema, “Kwa nini hamtii amri ya Bwana? Jambo hili halitafanikiwa!
But Moses/I said, “Yahweh commanded you [to return to the desert, so] why are you now disobeying him [RHQ]? It will not (succeed/be possible).
42 Msipande juu, kwa kuwa Bwana hayupo pamoja nanyi. Mtashindwa na adui zenu,
Do not try to enter the land now! [If you try], your enemies will defeat you, because Yahweh will not (be with/help) you.
43 kwa kuwa Waamaleki na Wakanaani watapambana nanyi huko. Kwa sababu mmemwacha Bwana, hatakuwa pamoja nanyi, ninyi mtaanguka kwa upanga.”
When you begin to fight the descendants of Amalek and Canaan, they will slaughter you! Yahweh will abandon you, because you have abandoned him.”
44 Hata hivyo, kwa kiburi chao walipanda juu kuelekea nchi ya vilima virefu, ijapokuwa Mose hakutoka kambini wala Sanduku la Agano la Bwana.
But even though Moses/I did not leave the camp, and the sacred chest that contained the Ten Commandments was not taken from the camp, the people began to go towards the hilly area in Canaan.
45 Ndipo Waamaleki na Wakanaani walioishi katika hiyo nchi ya vilima wakateremka na kuwashambulia, wakawapiga njia yote hadi Horma.
Then the descendants of Amalek and Canaan who lived in that hilly area came down and attacked them and chased them as far [south] as [the town of] Hormah.

< Hesabu 14 >