< Hesabu 10 >

1 Bwana akamwambia Mose:
Et l'Éternel parla à Moïse, en disant:
2 “Tengeneza tarumbeta mbili za fedha ya kufua, uzitumie kwa kuita jumuiya pamoja na wakati wa kuvunja makambi ili kuondoka.
Fais-toi deux trompettes d'argent; tu les feras façonnées au marteau; elles te serviront pour convoquer l'assemblée, et pour le départ des camps.
3 Tarumbeta zote mbili zikipigwa, jumuiya yote itakusanyika mbele yako katika ingilio la Hema la Kukutania.
Quand on en sonnera, toute l'assemblée se réunira vers toi, à l'entrée du tabernacle d'assignation.
4 Kama tarumbeta moja tu ikipigwa, viongozi, yaani wakuu wa koo za Israeli, ndio watakaokusanyika mbele yako.
Si l'on sonne d'une seule, les princes, les chefs des milliers d'Israël, se réuniront vers toi.
5 Wakati mlio wa kujulisha hatari ukipigwa, makabila yaliyo na makambi upande wa mashariki yataondoka.
Quand vous sonnerez d'un son éclatant, les camps qui sont à l'orient partiront.
6 Ukisikika mlio wa pili wa jinsi hiyo, walioko kwenye makambi ya kusini wataondoka. Mlio huo wa kujulisha hatari utakuwa ishara ya kuondoka.
Et quand vous sonnerez une seconde fois d'un son éclatant, les camps qui sont au midi partiront; on sonnera d'un son éclatant lorsqu'ils devront partir.
7 Ili kukusanya kusanyiko, piga tarumbeta zote, lakini siyo kwa mlio wa kujulisha hatari.
Quand on convoquera l'assemblée, vous sonnerez, mais non d'un son éclatant.
8 “Wana wa Aroni, makuhani, ndio watakaopiga hizo tarumbeta. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yenu na kwa vizazi vijavyo.
Or les fils d'Aaron, les sacrificateurs, sonneront des trompettes; et elles seront pour vous une ordonnance perpétuelle, d'âge en âge.
9 Wakati mtakapopigana vita katika nchi yenu wenyewe dhidi ya adui anayewaonea, piga tarumbeta kwa mlio wa kujulisha hatari. Ndipo utakumbukwa na Bwana Mungu wenu na kuokolewa kutoka kwa adui zenu.
Et quand vous irez à la guerre dans votre pays, contre l'ennemi qui vous attaquera, vous sonnerez des trompettes avec un son éclatant, et vous serez remis en mémoire devant l'Éternel votre Dieu, et vous serez délivrés de vos ennemis.
10 Pia nyakati za furaha yenu, yaani sikukuu zenu zilizoamriwa na sikukuu za Mwezi Mwandamo, mtapiga tarumbeta juu ya sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka zenu za amani, nazo zitakuwa ukumbusho kwa ajili yenu mbele za Mungu wenu. Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.”
Et dans vos jours de joie, dans vos solennités, et au commencement de vos mois, vous sonnerez des trompettes sur vos holocaustes, et sur vos sacrifices de prospérités, et elles vous serviront de mémorial devant votre Dieu. Je suis l'Éternel, votre Dieu.
11 Katika siku ya ishirini ya mwezi wa pili wa mwaka wa pili, wingu liliinuka kutoka juu ya maskani ya Ushuhuda.
Or il arriva, le vingtième jour du second mois de la seconde année, que la nuée se leva de dessus la Demeure du Témoignage.
12 Ndipo Waisraeli wakaondoka kutoka Jangwa la Sinai wakasafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine mpaka wingu lilipotua katika Jangwa la Parani.
Et les enfants d'Israël partirent, selon leur ordre de marche, du désert de Sinaï; et la nuée s'arrêta au désert de Paran.
13 Waliondoka kwa mara ya kwanza kwa agizo la Bwana kupitia kwa Mose.
Ils partirent donc, pour la première fois, sur l'ordre de l'Éternel, donné par le moyen de Moïse.
14 Vikosi vya kambi ya Yuda vilitangulia kwanza chini ya alama yao. Nashoni mwana wa Aminadabu alikuwa kiongozi wao.
La bannière du camp des enfants de Juda partit la première, selon leurs armées; Nahasshon, fils d'Amminadab, commandait l'armée de Juda.
15 Nethaneli mwana wa Suari alikuwa kiongozi wa kabila la Isakari,
Nathanaël, fils de Tsuar, commandait l'armée de la tribu des enfants d'Issacar.
16 naye Eliabu mwana wa Heloni alikuwa kiongozi wa kabila la Zabuloni.
Éliab, fils de Hélon, commandait l'armée de la tribu des enfants de Zabulon.
17 Ndipo Maskani iliposhushwa, nao wana wa Gershoni na wana wa Merari ambao waliibeba wakaondoka.
La Demeure fut démontée et les enfants de Guershon et les enfants de Mérari, qui portaient la Demeure, partirent.
18 Vikosi vya kambi ya Reubeni vilifuata, chini ya alama yao. Elisuri mwana wa Shedeuri alikuwa kiongozi wao.
Puis la bannière du camp de Ruben partit, selon leurs armées; et Elitsur, fils de Shedéur, commandait l'armée de Ruben.
19 Shelumieli mwana wa Surishadai aliongoza kikosi cha kabila la Simeoni,
Et Shelumiel, fils de Tsurishaddaï, commandait l'armée de la tribu des enfants de Siméon.
20 naye Eliasafu mwana wa Deueli aliongoza kikosi cha kabila la Gadi.
Et Eliasaph, fils de Déhuël, commandait l'armée de la tribu des enfants de Gad.
21 Kisha Wakohathi wakaondoka, wakichukua vitu vitakatifu. Maskani ilikuwa isimamishwe kabla wao hawajafika.
Alors les Kéhathites, qui portaient le sanctuaire, partirent; or, on dressait la Demeure, en attendant leur arrivée.
22 Vikosi vya kambi ya Efraimu vilifuata, chini ya alama yao. Elishama mwana wa Amihudi alikuwa kiongozi wao.
Puis la bannière du camp des enfants d'Éphraïm partit, selon leurs armées; et Elishama, fils d'Ammihud, commandait l'armée d'Éphraïm.
23 Gamalieli mwana wa Pedasuri aliongoza kikosi cha kabila la Manase,
Et Gamaliel, fils de Pédahtsur, commandait l'armée de la tribu des enfants de Manassé.
24 naye Abidani mwana wa Gideoni alikuwa kiongozi wa kikosi cha kabila la Benyamini.
Et Abidan, fils de Guideoni, commandait l'armée de la tribu des enfants de Benjamin.
25 Mwishowe, kama kikosi cha nyuma cha ulinzi wa vikosi vyote, vikosi vya kambi ya Dani viliondoka chini ya alama yao. Ahiezeri mwana wa Amishadai alikuwa kiongozi wao.
Enfin la bannière du camp des enfants de Dan, qui formait l'arrière-garde de tous les camps, partit, selon leurs armées; et Ahiézer, fils d'Ammishaddaï, commandait l'armée de Dan.
26 Pagieli mwana wa Okrani aliongoza kikosi cha kabila la Asheri,
Et Paguiel, fils d'Ocran, commandait l'armée de la tribu des enfants d'Asser.
27 naye Ahira mwana wa Enani aliongoza kikosi cha kabila la Naftali.
Et Ahira, fils d'Enan, commandait l'armée de la tribu des enfants de Nephthali.
28 Huu ndio ulikuwa utaratibu wa kuondoka wa vikosi vya Waisraeli walipokuwa wanaondoka.
Tel était l'ordre de marche des enfants d'Israël, selon leurs armées; et ils partirent.
29 Basi Mose akamwambia Hobabu mwana wa Reueli, Mmidiani, mkwewe Mose, “Tunaondoka kwenda mahali ambapo Bwana amesema ‘Nitawapa ninyi mahali hapo.’ Twende pamoja nasi tutakutendea mema, kwa maana Bwana ameahidi mambo mema kwa Israeli.”
Or, Moïse dit à Hobab, fils de Réuel, le Madianite, beau-père de Moïse: Nous partons pour le lieu dont l'Éternel a dit: Je vous le donnerai; viens avec nous, et nous te ferons du bien; car l'Éternel a promis de faire du bien à Israël.
30 Akajibu, “Hapana, sitakwenda; nitarudi kwenye nchi yangu mwenyewe na watu wangu mwenyewe.”
Et Hobab lui répondit: Je n'irai point, mais j'irai dans mon pays, et dans le lieu de ma naissance.
31 Lakini Mose akasema, “Tafadhali usituache. Wewe unajua mahali ambapo yatupasa kupiga kambi jangwani, nawe unaweza kuwa macho yetu.
Et Moïse lui dit: Je te prie, ne nous laisse point; puisque tu connais les lieux où nous pouvons camper dans le désert, tu nous serviras de guide.
32 Ikiwa utafuatana nasi, tutashirikiana nawe mema yoyote tutakayopewa na Bwana.”
Et il arrivera, si tu viens avec nous et que ce bien que l'Éternel doit nous faire arrive, que nous te ferons aussi du bien.
33 Hivyo waliondoka kutoka mlima wa Bwana, nao wakasafiri kwa siku tatu. Sanduku la Agano la Bwana liliwatangulia kwa zile siku tatu ili kuwatafutia mahali pa kupumzika.
Ils partirent donc de la montagne de l'Éternel, et marchèrent pendant trois jours; et l'arche de l'alliance de l'Éternel allait devant eux, faisant trois journées de chemin, pour leur chercher un lieu de repos.
34 Wingu la Bwana lilikuwa juu yao wakati wa mchana walipoondoka kambini.
Et la nuée de l'Éternel était sur eux pendant le jour, quand ils partaient du camp.
35 Wakati wowote Sanduku lilipoondoka, Mose alisema, “Ee Bwana, inuka! Watesi wako na watawanyike; adui zako na wakimbie mbele zako.”
Et quand l'arche partait, Moïse disait: Lève-toi, Éternel, et que tes ennemis soient dispersés, et que ceux qui te haïssent s'enfuient devant ta face!
36 Wakati wowote Sanduku liliposimama, alisema, “Ee Bwana, rudi, kwa maelfu ya Waisraeli wasiohesabika.”
Et quand on la posait, il disait: Reviens, Éternel, aux dix mille milliers d'Israël!

< Hesabu 10 >