< Nehemia 11 >

1 Basi viongozi wa watu walikaa Yerusalemu, nao watu wale wengine walipiga kura ili kuleta mtu mmoja kati ya watu kumi aje kuishi Yerusalemu, mji mtakatifu, nao wengine tisa waliobaki wakae katika miji yao wenyewe.
Et les principaux du peuple s'habituèrent a Jérusalem, mais tout le reste du peuple jeta le sort, afin qu'une des dix parties s'habituât à Jérusalem la sainte Cité, et que les neuf [autres] parties demeurassent dans les [autres] villes.
2 Watu waliwasifu wale wote waliojitolea kuishi Yerusalemu.
Et le peuple bénit tous ceux qui se présentèrent volontairement pour s'habituer à Jérusalem.
3 Hawa ndio viongozi wa majimbo waliokuja kuishi Yerusalemu (baadhi ya Waisraeli, makuhani, Walawi, watumishi wa Hekalu, na wazao wa watumishi wa Solomoni waliendelea kuishi katika miji ya Yuda, kila mmoja katika milki yake mwenyewe katika miji mbalimbali,
Or ce sont ici les principaux de la province qui s'habituèrent à Jérusalem; les autres s'étant habitués dans les villes de Juda, chacun dans sa possession, selon leurs villes, [savoir] les Israélites, les Sacrificateurs, les Lévites, les Néthiniens, et les enfants des serviteurs de Salomon.
4 ambapo watu wengine kutoka Yuda na Benyamini waliishi Yerusalemu). Kutoka wazao wa Yuda: Athaya mwana wa Uzia, mwana wa Zekaria, mwana wa Amaria, mwana wa Shefatia, mwana wa Mahalaleli, mzao wa Peresi.
Ceux de Juda et de Benjamin s'habituèrent donc à Jérusalem; des enfants de Juda Hathaja fils d'Huzija, fils de Zacharie, fils d'Amaria, fils de Séphatia, fils de Mahalaléel, d'entre les enfants de Pharès.
5 Naye Maaseya mwana wa Baruku, mwana wa Kolhoze, mwana wa Hazaya, mwana wa Adaya, mwana wa Yoyaribu, mwana wa Zekaria, mzao wa Mshiloni.
Et Mahaséja fils de Baruc, fils de Colhozé, fils de Hazaja, fils d'Hadaja, fils de Jojarib, fils de Zacharie, fils de Siloni.
6 Wazao wa Peresi walioishi Yerusalemu walikuwa 468, watu wenye uwezo.
Tous ceux-là étaient enfants de Pharès, qui s'habituèrent à Jérusalem, quatre cent soixante-huit, vaillants hommes.
7 Kutoka wazao wa Benyamini: Salu mwana wa Meshulamu, mwana wa Yoedi, mwana wa Pedaya, mwana wa Kolaya, mwana wa Maaseya, mwana wa Ithieli, mwana wa Yeshaya
Et ceux-ci étaient d'entre les enfants de Benjamin; Sallu, fils de Mésullam, fils de Johed, fils de Pédaja, fils de Kolaja, fils de Mahaséja, fils d'Ithiel, fils d'Esaïe;
8 na wafuasi wake, Gabai na Salai watu 928.
Et après lui Gabbaï, Sallaï, neuf cent vingt-huit.
9 Yoeli mwana wa Zikri alikuwa afisa wao mkuu, naye Yuda mwana wa Hasenua alikuwa msimamizi juu ya Mtaa wa Pili katika mji.
Et Joël fils de Zicri était commis sur eux; et Juda fils de Sénua était Lieutenant de la ville.
10 Kutoka makuhani: Yedaya, mwana wa Yoyaribu, Yakini,
Des Sacrificateurs: Jéhahia, fils de Jojarib, Jakin,
11 Seraya mwana wa Hilkia, mwana wa Meshulamu, mwana wa Sadoki, mwana wa Merayothi, mwana wa Ahitubu, msimamizi katika nyumba ya Mungu,
Séraja, fils de Hilkija, fils de Mésullam, fils de Tsadok, fils de Mérajoth, fils d'Ahitub, Conducteur de la maison de Dieu;
12 pamoja na wenzao waliofanya kazi hekaluni: watu 822. Adaya mwana wa Yerohamu, mwana wa Pelalia, mwana wa Amsi, mwana wa Zekaria, mwana wa Pashuri, mwana wa Malkiya,
Et leurs frères, qui faisaient le service de la maison, huit cent vingt-deux. Et Hodaja fils de Jéroham, fils de Pélalja, fils d Amtsi, fils de Zacharie, fils de Pashur, fils de Malkija.
13 na wenzao, waliokuwa viongozi wa jamaa: watu 242. Amashisai mwana wa Azareli, mwana wa Azai, mwana wa Meshilemothi, mwana wa Imeri,
Et ses frères, les Chefs des pères, deux cent quarante-deux. Et Hamassaï, fils d'Hazaréel, fils d'Ahzaï, fils de Mésillémoth, fils d'Immer;
14 na wenzao waliokuwa wenye uwezo: watu 128. Afisa wao mkuu alikuwa Zabdieli mwana wa Hagedolimu.
Et leurs frères, forts et vaillants, cent vingt-huit; et Zabdiel, fils de Guédolim, [était] commis sur eux.
15 Kutoka Walawi: Shemaya mwana wa Hashubu, mwana wa Azrikamu, mwana wa Hashabia, mwana wa Buni;
Et des Lévites: Sémahja, fils de Hasub, fils d'Hazrikam, fils de Hasabia, fils de Bunni.
16 Shabethai na Yozabadi, viongozi wawili wa Walawi, ambao walisimamia kazi za nje za nyumba ya Mungu;
Et Sabbethaï et Jozabad étaient commis sur le travail de dehors pour la maison de Dieu, [étant] d'entre les Chefs des Lévites.
17 Matania mwana wa Mika, mwana wa Zabdi, mwana wa Asafu, kiongozi aliyeongoza kutoa shukrani na maombi; Bakbukia aliyekuwa msaidizi wake kati ya wenzake; na Abda mwana wa Shamua, mwana wa Galali, mwana wa Yeduthuni.
Et Mattania, fils de Mica, fils de Zabdi, fils d'Asaph, était le principal [des chantres], qui commençait le premier à chanter les louanges dans la prière. Et Bakbukia était le second d'entre ses frères, puis Habda, fils de Sammuah, fils de Galal, fils de Jéduthun.
18 Jumla ya Walawi waliokaa katika mji mtakatifu walikuwa watu 284.
Tous les Lévites [qui s'établirent dans] la sainte Cité, étaient deux cent quatre-vingt-quatre.
19 Mabawabu: Akubu, Talmoni na wenzao, waliolinda malango: watu 172.
Et des portiers, Hakkub, Talmon, et leurs frères qui gardaient les portes, cent soixante et douze.
20 Waisraeli waliosalia, pamoja na makuhani na Walawi, walikuwa katika miji yote ya Yuda, kila mmoja katika urithi wa baba yake.
Et le reste des Israélites, des Sacrificateurs, et des Lévites fut dans toutes les villes de Juda, chacun en son héritage.
21 Watumishi wa Hekalu waliishi katika kilima cha Ofeli. Siha na Gishpa walikuwa wasimamizi wao.
Mais les Néthiniens habitèrent à Hophel; et Tsiha et Guispa étaient commis sur les Néthiniens.
22 Afisa mkuu wa Walawi huko Yerusalemu alikuwa Uzi mwana wa Bani, mwana wa Hashabia, mwana wa Matania, mwana wa Mika. Uzi alikuwa mmoja wa wazao wa Asafu, waliokuwa waimbaji wenye kuwajibika kwa ajili ya huduma ya nyumba ya Mungu.
Et celui qui avait la charge des Lévites à Jérusalem, était Huzi fils de Bani, fils de Hasabia, fils de Mattania, fils de Mica, d'entre les enfants d'Asaph, chantres, pour l'ouvrage de la maison de Dieu.
23 Waimbaji walikuwa chini ya amri za mfalme, ambazo pia ziliratibu shughuli zao za kila siku.
Car il y avait aussi un commandement du Roi qui les regardait, et il y avait un état assuré pour les chantres chaque jour.
24 Pethahia mwana wa Meshezabeli, mmoja wa wazao wa Zera mwana wa Yuda, alikuwa mwakilishi wa mfalme katika mambo yote kuhusu mahusiano na watu.
Et Péthahia, fils de Mésézabéel, d'entre les enfants de Zara, fils de Juda, était commissaire du Roi, dans tout ce qui était à faire envers le peuple.
25 Kuhusu vijiji na mashamba yake, baadhi ya watu wa Yuda waliishi Kiriath-Arba na makazi yaliyokizunguka, katika Diboni na makazi yake, katika Yekabzeeli na vijiji vyake,
Or quant aux bourgades avec leurs territoires, quelques-uns des enfants de Juda habitèrent à Kiriath-Arbah, et dans les lieux de son ressort; à Dibon, et dans les lieux de son ressort; à Jékabtséel, et dans les lieux de son ressort;
26 katika Yeshua, katika Molada, katika Beth-Peleti,
A Jésuah, à Molada, à Beth-Pélet.
27 katika Hasar-Shuali, katika Beer-Sheba na makazi yake,
A Hatsar-Sual, à Béer-Sébah, et dans les lieux de son ressort;
28 katika Siklagi, katika Mekona na makazi yake,
A Tsiklag, à Mécona, et dans les lieux de son ressort;
29 katika En-Rimoni, katika Sora, katika Yarmuthi,
A Hen-rimmon, à Tsorah, à Jarmuth,
30 Zanoa, Adulamu na vijiji vyake, katika Lakishi na mashamba yake, na katika Azeka na makazi yake. Hivyo walikuwa wakiishi kuanzia Beer-Sheba mpaka Bonde la Hinomu.
A Zanoah, à Hadullam, et dans leurs bourgades; à Lakis, et dans ses territoires; et à Hazeka, et dans les lieux de son ressort. Et ils habitèrent depuis Béer-Sébah jusqu'à la vallée de Hinnom.
31 Wazao wa Wabenyamini kutoka Geba waliishi Mikmashi, Aiya, Betheli na makazi yake,
Et les enfants de Benjamin [habitèrent] depuis Guébah, à Micmas, Haja, Bethel, et dans les lieux de son ressort;
32 katika Anathothi, Nobu na Anania,
A Hanathoth, Nob, Hanania,
33 katika Hazori, Rama na Gitaimu,
Hatsor, Rama, Guittajim,
34 katika Hadidi, Seboimu na Nebalati,
Hadid, Tsébohim, Néballat,
35 katika Lodi na Ono, na katika Bonde la Mafundi.
Lod, et Ono, la vallée des manœuvres.
36 Baadhi ya makundi ya Walawi wa Yuda waliishi huko Benyamini.
Et quelques-uns des Lévites [habitèrent] dans leurs partages de Juda et de Benjamin.

< Nehemia 11 >