< Nehemia 11 >

1 Basi viongozi wa watu walikaa Yerusalemu, nao watu wale wengine walipiga kura ili kuleta mtu mmoja kati ya watu kumi aje kuishi Yerusalemu, mji mtakatifu, nao wengine tisa waliobaki wakae katika miji yao wenyewe.
The leaders of the people lived in Jerusalem, and the rest of the people cast lots to bring one of ten to live in Jerusalem, the holy city, and the other nine remained in other towns.
2 Watu waliwasifu wale wote waliojitolea kuishi Yerusalemu.
Then the people blessed all those who willingly offered to live in Jerusalem.
3 Hawa ndio viongozi wa majimbo waliokuja kuishi Yerusalemu (baadhi ya Waisraeli, makuhani, Walawi, watumishi wa Hekalu, na wazao wa watumishi wa Solomoni waliendelea kuishi katika miji ya Yuda, kila mmoja katika milki yake mwenyewe katika miji mbalimbali,
These are the provincial officials who lived in Jerusalem. However, in the towns of Judah everyone lived on his own land, including some Israelites, priests, Levites, temple servants, and descendants of Solomon's servants.
4 ambapo watu wengine kutoka Yuda na Benyamini waliishi Yerusalemu). Kutoka wazao wa Yuda: Athaya mwana wa Uzia, mwana wa Zekaria, mwana wa Amaria, mwana wa Shefatia, mwana wa Mahalaleli, mzao wa Peresi.
In Jerusalem lived some of the descendants of Judah and some of the descendants of Benjamin. The people from Judah included: Athaiah son of Uzziah son of Zechariah son of Amariah son of Shephatiah son of Mahalalel, a descendant of Perez.
5 Naye Maaseya mwana wa Baruku, mwana wa Kolhoze, mwana wa Hazaya, mwana wa Adaya, mwana wa Yoyaribu, mwana wa Zekaria, mzao wa Mshiloni.
There was Maaseiah son of Baruch son of Kol-Hozeh son of Hazaiah son of Adaiah son of Joiarib son of Zechariah, the son of the Shilonite.
6 Wazao wa Peresi walioishi Yerusalemu walikuwa 468, watu wenye uwezo.
All the sons of Perez who lived in Jerusalem were 468. They were outstanding men.
7 Kutoka wazao wa Benyamini: Salu mwana wa Meshulamu, mwana wa Yoedi, mwana wa Pedaya, mwana wa Kolaya, mwana wa Maaseya, mwana wa Ithieli, mwana wa Yeshaya
These are the descendants of Benjamin: Sallu son of Meshullam son of Joed son of Pedaiah son of Kolaiah son of Maaseiah son of Ithiel son of Jeshaiah,
8 na wafuasi wake, Gabai na Salai watu 928.
and those following him, Gabbai and Sallai, 928 men.
9 Yoeli mwana wa Zikri alikuwa afisa wao mkuu, naye Yuda mwana wa Hasenua alikuwa msimamizi juu ya Mtaa wa Pili katika mji.
Joel son of Zichri was their overseer, and Judah son of Hassenuah was second in command over the city.
10 Kutoka makuhani: Yedaya, mwana wa Yoyaribu, Yakini,
From the priests: Jedaiah son of Joiarib, Jakin,
11 Seraya mwana wa Hilkia, mwana wa Meshulamu, mwana wa Sadoki, mwana wa Merayothi, mwana wa Ahitubu, msimamizi katika nyumba ya Mungu,
Seraiah son of Hilkiah son of Meshullam son of Zadok son of Meraioth son of Ahitub, the chief official of the house of God,
12 pamoja na wenzao waliofanya kazi hekaluni: watu 822. Adaya mwana wa Yerohamu, mwana wa Pelalia, mwana wa Amsi, mwana wa Zekaria, mwana wa Pashuri, mwana wa Malkiya,
and their associates who did the work for the house, 822 men, along with Adaiah son of Jeroham son of Pelaliah son of Amzi son of Zechariah son of Pashhur son of Malchijah.
13 na wenzao, waliokuwa viongozi wa jamaa: watu 242. Amashisai mwana wa Azareli, mwana wa Azai, mwana wa Meshilemothi, mwana wa Imeri,
His brothers were heads of clans, 242 men; and Amashsai son of Azarel son of Ahzai son of Meshillemoth son of Immer,
14 na wenzao waliokuwa wenye uwezo: watu 128. Afisa wao mkuu alikuwa Zabdieli mwana wa Hagedolimu.
and their brothers, 128 courageous fighting men; their overseer was Zabdiel son of Haggedolim.
15 Kutoka Walawi: Shemaya mwana wa Hashubu, mwana wa Azrikamu, mwana wa Hashabia, mwana wa Buni;
From the Levites: Shemaiah son of Hasshub son of Azrikam son of Hashabiah son of Bunni,
16 Shabethai na Yozabadi, viongozi wawili wa Walawi, ambao walisimamia kazi za nje za nyumba ya Mungu;
and Shabbethai and Jozabad, who were from the leaders of the Levites and were in charge of the outside work of the house of God.
17 Matania mwana wa Mika, mwana wa Zabdi, mwana wa Asafu, kiongozi aliyeongoza kutoa shukrani na maombi; Bakbukia aliyekuwa msaidizi wake kati ya wenzake; na Abda mwana wa Shamua, mwana wa Galali, mwana wa Yeduthuni.
There was Mattaniah son of Mika son of Zabdi, a descendant of Asaph, who was the director who began the thanksgiving in prayer, and Bakbukiah, the second among his brothers, and Abda son of Shammua son of Galal son of Jeduthun.
18 Jumla ya Walawi waliokaa katika mji mtakatifu walikuwa watu 284.
All the Levites in the holy city numbered 284.
19 Mabawabu: Akubu, Talmoni na wenzao, waliolinda malango: watu 172.
The gatekeepers: Akkub, Talmon, and their associates, who kept watch at the gates, 172 men.
20 Waisraeli waliosalia, pamoja na makuhani na Walawi, walikuwa katika miji yote ya Yuda, kila mmoja katika urithi wa baba yake.
The remainder of Israel and of the priests and the Levites were in all the towns of Judah. Everyone lived on his own inherited property.
21 Watumishi wa Hekalu waliishi katika kilima cha Ofeli. Siha na Gishpa walikuwa wasimamizi wao.
The temple workers lived in Ophel, and Ziha and Gishpa were in charge of them.
22 Afisa mkuu wa Walawi huko Yerusalemu alikuwa Uzi mwana wa Bani, mwana wa Hashabia, mwana wa Matania, mwana wa Mika. Uzi alikuwa mmoja wa wazao wa Asafu, waliokuwa waimbaji wenye kuwajibika kwa ajili ya huduma ya nyumba ya Mungu.
The chief officer over the Levites in Jerusalem was Uzzi son of Bani son of Hashabiah son of Mattaniah son of Mika, of the descendants of Asaph, singers over the work in the house of God.
23 Waimbaji walikuwa chini ya amri za mfalme, ambazo pia ziliratibu shughuli zao za kila siku.
They were under orders from the king, and firm orders were given for the singers as every day required.
24 Pethahia mwana wa Meshezabeli, mmoja wa wazao wa Zera mwana wa Yuda, alikuwa mwakilishi wa mfalme katika mambo yote kuhusu mahusiano na watu.
Then Pethahiah son of Meshezabel, a descendant of Zerah son of Judah, was at the king's side in all matters concerning the people.
25 Kuhusu vijiji na mashamba yake, baadhi ya watu wa Yuda waliishi Kiriath-Arba na makazi yaliyokizunguka, katika Diboni na makazi yake, katika Yekabzeeli na vijiji vyake,
As for the villages and their fields, some of the people of Judah lived in Kiriath Arba and its villages, and in Dibon and its villages, and in Jekabzeel and its villages,
26 katika Yeshua, katika Molada, katika Beth-Peleti,
and in Jeshua, Moladah, Beth Pelet,
27 katika Hasar-Shuali, katika Beer-Sheba na makazi yake,
Hazar Shual, and Beersheba and its villages.
28 katika Siklagi, katika Mekona na makazi yake,
Some of the people of Judah lived in Ziklag, Mekonah and its villages,
29 katika En-Rimoni, katika Sora, katika Yarmuthi,
Enrimmon, Zorah, Jarmuth,
30 Zanoa, Adulamu na vijiji vyake, katika Lakishi na mashamba yake, na katika Azeka na makazi yake. Hivyo walikuwa wakiishi kuanzia Beer-Sheba mpaka Bonde la Hinomu.
Zanoah, Adullam, and their villages, and in Lachish its fields and Azekah and its villages. So they lived from Beersheba to the Valley of Hinnom.
31 Wazao wa Wabenyamini kutoka Geba waliishi Mikmashi, Aiya, Betheli na makazi yake,
The people of Benjamin also lived from Geba onward, at Mikmash and Aija, at Bethel and its villages,
32 katika Anathothi, Nobu na Anania,
at Anathoth, Nob, Ananiah,
33 katika Hazori, Rama na Gitaimu,
Hazor, Ramah, Gittaim,
34 katika Hadidi, Seboimu na Nebalati,
Hadid, Zeboim, Neballat,
35 katika Lodi na Ono, na katika Bonde la Mafundi.
Lod, and Ono, the valley of craftsmen.
36 Baadhi ya makundi ya Walawi wa Yuda waliishi huko Benyamini.
Some of the Levites who lived in Judah were assigned to the people of Benjamin.

< Nehemia 11 >